Like us on Facebook

Inaendeshwa na Blogger.

Tafuta katika Blogu Hii

Kumbukumbu la Blogu

Instagram

visitors

display number of visitors

Popular Posts

Pages

Flickr Images

Jumamosi, 16 Machi 2019

WATUMISHI TUISHI KWA UPENDO

Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt Faustine Ndugulile akisisitiza jambo wakati akiongea na Watumishi wa Sekta ya Afya, katika mkutano wa Baraza la Wafanyakazi kujadili bajeti ya Wizara ya Afya uliofanyika katika ukumbi wa Mipango Jijini Dodoma

Katibu Mkuu Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto ambae pia ni Mwenyekiti wa Baraza la Wafanyakazi Wizara ya Afya Dkt. Zainab Chaula akiongea na Watumishi wa Sekta ya Afya (Hawapo kwenye picha) wakati wa mkutano wa Baraza la Wafanyakazi kujadili bajeti ya Wizara ya Afya uliofanyika katika ukumbi wa Mipango Jijini Dodoma 

Naibu Katibu Mkuu TUGHE Taifa Eng. Amani Msuya akiwasilisha hoja za Wafanyakazi mbele ya Mgeni rasmi wa Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt Faustine Ndugulile na Katibu Mkuu Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto ambae pia ni Mwenyekiti wa Baraza la Wafanyakazi Wizara ya Afya Dkt. Zainab Chaula.

Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt Faustine Ndugulile akiteta jambo na Katibu Mkuu Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto ambae pia ni Mwenyekiti wa Baraza la Wafanyakazi Wizara ya Afya Dkt. Zainab Chaula

Meza Kuu ikiongozwa na Mgeni rasmi Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt Faustine Ndugulile (Watatu kutoka kushoto) wakati wakiimba wimbo wa kuhamasisha umoja na mshikamano wakati wa mkutano wa Baraza la Wafanyakazi kujadili bajeti ya Wizara ya Afya uliofanyika katika ukumbi wa Mipango Jijini Dodoma.

Baadhi ya Watumishi wa Sekta ya Afya ambao pia ni Wanachama wa TUGHE Taifa wakishikana mikono huku wakiimba wimbo wa kuhamasisha umoja na mshikamano, wakati wa mkutano wa Baraza la Wafanyakazi kujadili bajeti ya Wizara ya Afya uliofanyika katika ukumbi wa Mipango Jijini Dodoma.


Baadhi ya Watumishi wa Sekta ya Afya ambao pia ni Wanachama wa TUGHE wakifuatilia maelekezo kutoka kwa Mgeni rasmi ambae ni Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt Faustine Ndugulile(Hayupo kwenye picha) wakati wa mkutano wa Baraza la Wafanyakazi kujadili bajeti ya Wizara ya Afya uliofanyika katika ukumbi wa Mipango Jijini Dodoma.

Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto ambae pia ni mgeni rasmi wa Mkutano huo Dkt Faustine Ndugulile akiteta jambo na Katibu Mkuu Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto ambae pia ni Mwenyekiti wa Baraza la Wafanyakazi Wizara ya Afya Dkt. Zainab Chaula katika mkutano wa Baraza la Wafanyakazi kujadili bajeti ya Wizara ya Afya uliofanyika katika ukumbi wa Mipango Jijini Dodoma

Picha ya pamoja ikiongozwa na Mgeni rasmi Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Faustine Ndugulile na Katibu Mkuu Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto ambae pia ni Mwenyekiti wa Baraza la Wafanyakazi Wizara ya Afya Dkt. Zainab Chaula wakiwa na baadhi ya Wajumbe wa TUGHE Taifa akati wa mkutano wa Baraza la Wafanyakazi kujadili bajeti ya Wizara ya Afya uliofanyika katika ukumbi wa Mipango Jijini Dodoma.


WATUMISHI TUISHI KWA UPENDO

Na WAMJW – Dodoma.
Watumishi watakiwa kudumisha upendo, umoja na mshikamano katika mahala pa kazi na kufanya kazi kwa bidii ili kutoa huduma iliyo bora.

Hayo yamesemwa na Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt Faustine Ndugulile alipokuwa akizungumza na watumishi wa Sekta ya afya wakati wa ufunguzi wa Baraza la Wafanyakazi lililofanyika jijini hapa

Dkt. Ndugulile amesema anaamini kuwa Wizara ya Afya itafika mbali zaidi ikiwa watumishi watafanya kazi kwa bidii kwa kuzingatia maadili ya utumishi wa umma na kuheshimiana bila kujali utofauti wa vyeo baina ya watumishi.

“Kila mmoja amuheshimu mwenzake kwa sababu ana mchango katika haya yote tunayoyafanya na tunategemeana sana kwenye kazi zetu za kila siku” amesema Dkt. Ndugulile.

Aidha, Dkt. Ndugulile amewataka watumishi kuziheshimu nafasi za uongozi walizonazo sasa kwa kuzienzi na kuhakikisha wanafanya kazi ili kuthibitisha kuwa kweli wanastahili kuwa kwenye nafasi hizo.

“Bado kuna watumishi wengine hawajajitafakari katika nafasi zao, lugha tunazozitoa, kutojituma, tuache kufanya kazi kwa mazoea” alisema Dkt. Ndugulile.

Awali akizungumza na wajumbe wa mkutano, Mwenyekiti wa Baraza hilo ambaye pia ni Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya, Dkt. Zainab Chaula amesisitiza watumishi kufanya kazi kwa umoja na kujitolea ili wote kwa pamoja kufikia malengo yaliyokusudiwa.

Katika Mkutano huo wajumbe walipitia na kujadili masuala kadha wa kadha kuhusiana na Wizara ya Afya ikiwemo bajeti ya Wizara, mabadiliko ya sheria ya mifuko ya hifadhi ya jamii, Sera ya Afya, Bima ya Afya pamoja na masuala ya utendaji ndani na nje ya Wizara.

Mwisho




0 on: "WATUMISHI TUISHI KWA UPENDO"