Like us on Facebook

Inaendeshwa na Blogger.

Tafuta katika Blogu Hii

Kumbukumbu la Blogu

Instagram

visitors

display number of visitors

Popular Posts

Pages

Flickr Images

Jumatano, 13 Machi 2019

WATOA HUDUMA ZA TIBA ASILI NA TIBA MBADALA WATAKIWA KUFUATA UTARATIBU WA KUTOA HUDUMA HIYO

Mtaalamu kutoka Sekretarieti ya Baraza la Tiba Asili na Tiba Mbadala Dkt. Marko Hingi akikagua vyeti vya kuruhusu huduma za Tiba Asili kutoka kwa mmoja wa wauzaji wa dawa hizo wakati alipofanya ziara ya kushtukiza katika mtaa wa Kariakoo.




Picha mbalimbali zikionesha wataalamu kutoka Sekretarieti ya Baraza la Tiba Asili na Tiba Mbadala walipofanya ziara ya ukaguzi wa vibali vinavyoruhusu kufanyika biashara kwenye maduka na wauzaji ya Tiba Asili na Tiba Mbadala katika maeneo tofauti Jijini Dar Es Salaam.

Moja ya maduka yaliyofungwa na wataalam kutoka Sekretarieti ya Baraza la Tiba Asili na Tiba Mbadala baada ya kukaguliwa na kubainika kukosa vigezo vya kuendesha biashara hiyo.



Na WAMJW-DSM

Watoa huduma za tiba asili na tiba mbadala wametakiwa kufuata taratibu zilizowekwa na Serikali kupitia Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto ili kulinda afya ya watumiaji wa dawa na huduma hizo.

Hayo yamebainika baada ya timu ya wataalam kutoka Baraza la Tiba Asili na Tiba Mbadala lililo chini ya Wizara ya Afya kufanya ukaguzi wa kushtukiza katika maduka yanayouza dawa za asili na kutoa huduma za tiba mbadala katika maeneo mbalimbali jijini Dar Es Salaam.

Katika ukaguzi huo imebainika baadhi ya maduka kufanya shughuli hiyo bila ya kuwa na vibali vikiwemo kibali cha mtoa huduma, Kibali cha duka pamoja na kibali cha usajili wa dawa, ambapo vibali hivyo vinatolewa na Baraza la Tiba Asili na Tiba Mbadala.

Dkt. Ruth Suza msajili wa Baraza la Tiba Asili na Tiba Mbadala amewataka watoa huduma hizo kufuata taratibu zilizowekwa na Wizara ili kuepuka usumbufu wa kufungiwa na kulipa faini kwa mujibu wa kanuni zilizowekwa na Baraza la Tiba Asili na Tiba Mbadala.

“Ninawataka watoa huduma za Tiba Asili na Tiba Mbadala nchini kote kuhakikisha wanafuata taratibu zilizowekwa na Baraza ili kuweza kuendesha biashara zao, vinginevyo tukipita kukagua na tukikuta duka lina kasoro kwa kukosa vibali basi tutapiga faini na ikishindikana kulipa faini  tutalifunga duka hilo mpaka muhusika afuate utaratibu unaotakiwa wa kufanya biashara hiyo”. Amesema Dkt. Ruth.

Katika ukaguzi huo uliochukua takribani wiki mbili katika wilaya zote za Jiji la Dar Es Salaam, jumla ya maduka 70 yamekaguliwa, maduka 10 yamefungwa kutokana na sababu mbalimbali ikiwemo maduka na wauzaji wa dawa kutokua na vibali kutoka baraza la tiba asili na tiba mbadala.
Zoezi hili lenye lengo la kulinda afya ya watumiaji wa dawa za asili na tiba mbadala ni endelevu ambapo linategemea kuendelea katika mikoa yote nchini kukagua uhalali wa usajili wa dawa za asili, vibali vya maduka na watoa huduma pamoja kuhakikisha ubora wa dawa zinazotolewa.











0 on: "WATOA HUDUMA ZA TIBA ASILI NA TIBA MBADALA WATAKIWA KUFUATA UTARATIBU WA KUTOA HUDUMA HIYO"