Like us on Facebook

Inaendeshwa na Blogger.

Tafuta katika Blogu Hii

Kumbukumbu la Blogu

Instagram

visitors

display number of visitors

Popular Posts

Pages

Flickr Images

Jumamosi, 23 Machi 2019

VIFO VYA WAMAMA WAJAWAZITO VYAPUNGUA KWA ZAIDI YA 40%

Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu akikata utepe kuashiria ufunguzi wa jengo la wagonjwa wa kulipia hospitali ya CCBRT Jijini Dar es salaam.Kushoto kwake ni Mkurugenzi wa CCBRT Brenda Msangi

Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu akihoji kupata ufafanuzi wa kina kutoka kwa mtaalamu wa Maabara ya macho CCBRT wakati wa ufunguzi wa jengo la jengo la wagonjwa wa kulipia hospitali ya CCBRT Jijini Dar es salaam.

Baadhi ya wageni waliohudhuria hafla ya ufunguzi wa jengo la wagonjwa wa kulipia hospitali ya CCBRT Jijini Dar es salaam, ambapo mgeni rasmi alikuwa Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu (Hayupo kwenye picha)

Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu akisisitiza jambo wakati wa ufunguzi wa jengo la jengo la wagonjwa wa kulipia hospitali ya CCBRT Jijini Dar es salaam.

Picha ya pamoja ikiongozwa na Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu pamoja na Viongozi wa CCBRT na wajumbe wa bodi ya CCBRT baada ya ufunguzi wa jengo la wagonjwa wa kulipia hospitali ya CCBRT Jijini Dar es salaam.


VIFO VYA WAMAMA WAJAWAZITO VYAPUNGUA KWA ZAIDI YA 40%

Na WAMJW - DSM

SERIKALI kupitia Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto kwa kushirikiana na Wadau wa masuala ya Afya imefanikiwa kupunguza Vifo vya wamama wajawazito kwa zaidi ya 40% , hali inayotokana na uboreshwaji wa huduma za Afya kwa wananchi.

Hayo yamesemwa na Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu leo wakati wa ufunguzi wa jengo la wagonjwa wa kulipia hospitali ya CCBRT Jijini Dar es salaam.

Waziri Ummy amesema kuwa Serikali imejenga na kuboresha zaidi ya vituo vya kutolea huduma za afya zaidi ya 350 ambavyo vinatoa huduma za dharura ikiwemo huduma ya upasuaji wa kumtoa mtoto tumboni.

"Tumepunguza vifo vyakina mama wajawazito kwa zaidi ya 40% ndani ya miaka sita (2012-2018), na kazi hii haijafanywa na Serikali tu,  kwahiyo hongereni sana CCBRT " alisema Mhe. Ummy Mwalimu.

Pia, Waziri Ummy amesema kuwa sote tunatambua umuhimu wa mtu kuwa na afya njema ili kuweza kumudu kushiriki katika shughuli za kijamii na kiuchumi kuanzia ngazi ya kaya hadi taifa, hivyo hatuwezi kuendelea kutegemea watu wengine kushughulikia afya za Watanzania.

Aidha, Waziri Ummy alisema kuwa Serikali imekuwa ikitoa huduma za matibabu kwa gharama nafuu sana au bila malipo kwa baadhi ya magonjwa kama Fistula, Mdomo Wazi na watoto chini ya miaka mitano.

Mbali na hayo, Waziri Ummy amesema kuwa katika miaka ya hivi karibuni uchumi wa dunia umeyumba na kupelekea kupungua kwa wafadhali. Kujengwa kwa kliniki hii ambayo itasaidia kuziba pengo la kiasi kinachopungua kutoka kwa wafadhili ambao ni jambo la msingi na la kuigwa.

Aidha, Waziri Ummy amesema kuwa Serikali kwa kushirikiana na wadau kama CCBRT imeendelea kutekeleza miradi mbalimbali ya maendeleo kwenye Sekta ya Afya yenye lengo la kuboresha utoaji wa huduma za afya na kuimarisha afya za wananchi.

0 on: " VIFO VYA WAMAMA WAJAWAZITO VYAPUNGUA KWA ZAIDI YA 40%"