Like us on Facebook

Inaendeshwa na Blogger.

Tafuta katika Blogu Hii

Kumbukumbu la Blogu

Instagram

visitors

display number of visitors

Popular Posts

Pages

Flickr Images

Ijumaa, 29 Machi 2019

CHANJO YA MLANGO WA KIZAZI NI SALAMA

Makamu wa Rais Samia Suluhu Hassan akihutubia wakati wa hafla ya uzinduzi wa Jengo na mashine za tiba ya saratani.

Makamu wa Rais Mhe. Samia Suluhu Hassan akizungumza na Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu (kushoto) wakati wa hafla ya uzinduzi wa Jengo na mashine za tiba ya saratani katika taasisi ya Saratani Ocean Road

 Baadhi ya Wakurugenzi na viongozi kutoka Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto wakifuatilia kwa makini ujumbe kutoka kwa Makamu wa Rais Mhe. Samia Suluhu Hassan wakati wa hafla ya uzinduzi wa Jengo na mashine za tiba ya saratani katika taasisi ya Saratani Ocean Road.
 Makamu wa Rais Mhe. Samia Suluhu Hassan akikata utepe, ishara ya uzinduzi rasmi wa mashine mpya za tiba ya mionzi, Wakwanza kushoto ni Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu

Makamu wa Rais Samia Suluhu Hassan akipata maelezo juu ya mashine ya kisasa ya tiba ya saratani kwa mionzi kutoka kwa Mkurugenzi Mtendaji  wa Taasisi ya Saratani Ocean Road Dkt. Julius Maiselage wakati hafla ya uzinduzi wa Jengo na mashine za tiba ya saratani. (Picha na Ofisi ya Makamu wa Rais)

Mashine mpya za kisasa za tiba ya saratani za Linac ( Linear Accelerator) ambazo zimezinduliwa leo katika Taasisi ya Saratani Ocean Road. 

Picha ya pamoja ikiongozwa na Makamu wa Rais Mhe. Samia Suluhu Hassan pamoja na Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu wakati wa hafla ya uzinduzi wa Jengo na mashine za tiba ya saratani katika taasisi ya Saratani Ocean Road


Na WAMJW - DSM
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan amewaasa wananchi wote hususan Wazazi kuwapeleka mabinti  wao kupata chanjo ya mlango wa kizazi (HPV) ili kuwakinga dhidi ya Saratani ya hiyo.

Ameyasema hayo leo wakati wa uzinduzi wa mashine mpya za tiba ya mionzi (linear accelerators) katika Taasisi ya Saratani Ocean Road Jijini Dar es salaam.

Mhe. Samia amesema kuwa Chanjo ya mlango wa kizazi ni salama  na inatumika katika nchi mbali mbali Afrika ikiwemo nchi za Uganda, Rwanda,Afrika Kusini, Zambia na Lesotho, hivyo kuwataka wazazi na walezi kuwapeleka mabinti wao kupata chanjo hiyo inayopatikana bila malipo.

"Kwa maelezo ya Wataalamu wametuhakikishia chanjo hii haina madhara, hivyo basi nawasihi Wazazi na Walezi wenye watoto kuhakikisha binti zetu ambao wengi wapo mashuleni, wanapata chanjo hii " alisema Mhe Samia.

Aidha, Mhe Samia amesema kuwa takribani wasichana 507,720 hapa nchini, wamepatiwa chanjo hii ya mlango wa kizazi, huku lengo likiwa ni kuwafikia wasichana 616,734 hadi Disemba 2018,

Mhe. Samia amesema kuwa nchi ya Tanzania inaripotiwa kuwa na Wagonjwa wa Saratani takribani 42,060, huku wagonjwa 28,610 hupoteza maisha kila mwaka kutokana na ugonjwa huo.

Mhe. Samia aliendelea kusema kuwa takwimu za 2018 za hospitali zinazotibu ugonjwa wa Saratani hapa nchini zinaonesha kuwa ni wagonjwa 14,000 sawa na 33.4% ndio wanaofika katika Hospitali ya Ocean road kupata huduma, ambao ni takribani wagonjwa 7600 kwa mwaka.

"Takwimu za hospitali zinazotibu ugonjwa wa Saratani hapa nchini za 2018, zinaonesha wagonjwa 14,000 sawa na asilimia 33.4 ndio wanaofika katika Hospitali yetu ya Ocean kupata huduma , ambao kwa mwaka ni 7600, Bugando ni wagonjwa 2790, KCMC 1050, Muhimbili 1321 na Mbeya Rufaa ni 218" alisema Mhe Samia Suluhu.

Aidha, Mhe Samia amesema kuwa inakadiriwa wagonjwa 1000 wanapata huduma katika Hospitali binafsi nchini,  huku 75% ya wagonjwa wengi wanafika katika hatua ya mwisho ya ugonjwa hali inayopelekea ugumu kuutibu ugonjwa huu.

Naye, Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu amesema kuwa idadi ya wagonjwa wanaopata ugonjwa huu, inaendelea kuongezeka nchini na Duniani huku ripoti ya 2018 ya Shirika la Umoja wa taifa la utafiti wa Saratani ikionesha kwamba takribani wagonjwa 28,610 hufariki katika wagonjwa wapya 42,060, huku vifo hivyo vikitarajia kufika Milioni 24 ifikapo 2035

Mbali na hayo, Waziri Ummy amesema kuwa kwa wanawake Saratani ya matiti inaongoza kwa kuwa na wagonjwa 24.2%, ikifuatiwa na Saratani ya utumbo mpana 9.6%, huku Saratani ya mapafu ni 8.4% na Saratani ya mlango wa kizazi ikiwa ni 6.6%

Aliendelea kusema kuwa kwa wanaume Saratani ya mapafu inaongoza kwa asilimia 14.5% ikifuatiwa na Saratani ya tezi dume ambayo ni asilimia 13.5%, Saratani ya utumbo mpana asilimia 10.9% na Saratani ya tumbo ni 7.2%.

Kwa upande wake Mkurugenzi wa Taasisi ya Saratani ya Ocean Road Dkt. Julius Mwaiselage amesema kuwa taasisi imefanikiwa kupunguza muda wa kuwahudumia wagonjwa tangu kufungwa kwa mashine hizo kutoka wiki sita mpaka kufikia wiki tatu,  na ifikapo mwezi Mei itafikia wiki mbili tu.

Naye, Shuhuda aliewahi kupata matibabu kupitia mashine hizo katika taasisi ya Saratani Ocean Road Bw. Frank  Ameishukuru Serikali ya Tanzania kupitia Rais wake Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli kwa juhudi wanazofanya za kuboresha Sekta ya Afya hususan katika huduma za kibingwa.

Mwisho.

0 on: "CHANJO YA MLANGO WA KIZAZI NI SALAMA "