Like us on Facebook

Inaendeshwa na Blogger.

Tafuta katika Blogu Hii

Kumbukumbu la Blogu

Instagram

visitors

display number of visitors

Popular Posts

Pages

Flickr Images

Ijumaa, 15 Machi 2019

SERIKALI YAOKOA BILION 4.2 KWENYE MATIBABU YA UGONJWA WA FIGO

Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Faustine Ndugulile akisisitiza jambo wakati akitoa tamko la Siku ya Figo Duniani, lililotolewa leo katika Ofisi za Wizara ya Afya Jijini Dodoma.

Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Faustine Ndugulile akiongea na Waandishi wa Habari (Hawapo kwenye picha) wakati akitoa tamko la Siku ya Figo Duniani, lililotolewa leo katika Ofisi za Wizara ya Afya Jijini Dodoma. Wakwanza kulia ni Kaimu Mkurugenzi wa Tiba Wizara ya Afya Dkt. Grace Maghembe na wamwisho ni Mwenyekiti wa Chama cha Magonjwa ya Figo nchini Dkt. Kisanga




Waandishi wa Habari waliojitokeza kumsikiliza Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Faustine Ndugulile wakati akitoa tamko la Siku ya Figo Duniani, lililotolewa leo katika Ofisi za Wizara ya Afya Jijini Dodoma.



SERIKALI YAOKOA BILION 3.4 KWENYE MATIBABU YA UGONJWA WA FIGO

Na WAMJW-DOM.

Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Faustine Ndugulile amesema kuwa Serikali imefanukiwa kuokoa kiasi cha Shilingi Bilion 4.2 ambacho kingetumika katika matibabu kwa Wagonjwa wa Figo nje ya Nchi.

Dkt. Ndugulile ameyasema hayo leo Machi 14 wakati akiongea na Waandishi wa Habari katika Ofisi za Wizara ya Afya Jijini Dodoma ikiwa ni Siku ya Figo Duniani ambayo inaongozwa na kauli mbiu ya Afya ya figo kwa kila mmoja kila.

Dkt. Ndugulile amesema kuwa Serikali imeokoa kiasi cha shilingi bilioni 4.2 ambacho kingetumika katika matibabu ya wagonjwa 80 mpaka 100 ambao wangepelekwa nje ya nchi kwaajili ya matibabu.

“Wagonjwa waliokwishapandikizwa figo hapa nchini ni 42, kama tungewapeleka  wagonjwa nje ya nchi ingegharimu serikali kiasi cha shilingi bilioni 4.2 kwa idadi hiyo ya wagonjwa.  80 mpaka 100, wakati huduma hii hapa nchini inagharimu kiasi cha shilingingi milioni 21 kwa kila mgonjwa.” Alisema Dkt. Ndugulile

Aidha, Dkt, Ndugulile amesema kuwa miongoni mwa sababu zinazochangia magonjwa ya figo ni pamoja na uzito wa kupindukia (obesity), matumizi makubwa ya sigara, unywaji wa pombe, uvutaji wa sigara,kutokufanya mazoezi na kunywa madawa kiholela hasa dawa za kupunguza maumivu.

Aliendelea kusema kuwa, magonjwa ya kisukari na shinikizo la damu ni magonjwa yanayoongoza kwa kusababisha matatizo ya figo, magonjwa haya yakitambuliwa mapema yanaweza kudhibitiwa kwa matibabu na kuepusha madhara kwenye figo.

Kwa upande mwingine Dkt. Ndugulile amesema kuwa Kufikia Desemba mwaka 2018, jumla ya vituo 28 vyenye jumla ya wagonjwa 1050 vilikuwa vikitoa huduma ya usafishaji damu katika mikoa ya Dar es Salaam, Mwanza, Mbeya, Arusha, Kilimanjaro na Dodoma.

0 on: "SERIKALI YAOKOA BILION 4.2 KWENYE MATIBABU YA UGONJWA WA FIGO"