Like us on Facebook

Inaendeshwa na Blogger.

Tafuta katika Blogu Hii

Kumbukumbu la Blogu

Instagram

visitors

display number of visitors

Popular Posts

Pages

Flickr Images

Jumatatu, 11 Desemba 2017

DKT. NDUGULILE AMPA MAAGIZO DMO MPWAPWA.

Naibu Waziri akimuuliza maswali mmoja kati ya wauguzi anayehusika na stoo hiyo ya dawa kwenye kituo cha afya kibakwe.

Dkt.Ndugulie akiongea na baadhi ya wakazi wa Kibakwe waliofika kituoni hapo kuwajulia hali wagonjwa wao.Dkt.Ndugulile aliwasisitiza wakazi hao kusimamia matumizi ya fedha na dawa kwani kituo hicho kimetengewa shilingi milioni 500 kwa ajili ya ujenzi wa chumba cha upasuaji wa dharura,nyumba za watumishi pamoja na ununuzi wa vifaa tiba kituoni hapo.

 Dkt.Ndugulile akiongea na watumishi wa kituo cha afya Kibakwe nje ya kituo hicho

Dkt.Faustine Ndugulile Naibu Waziri wa Afya,Maendeleo ya Jamii,Jinsia,Wazee na Watoto akikagua fomu ya orodha ya dawa iliyofanywa na kituo hicho kwa mnunuzi wa nje na ile ya MSD kwenye stoo ya dawa ya kituo cha afya cha kibakwe.


Picha ya pamoja ya Naibu Waziri wa Afya,Maendeleo ya Jamii,Jinsia,Wazee na Watoto pamoja na watumishi wa kituo cha afya Kibakwe wilayani Mpwapwa.



Na WAMJW-DODOMA
NAIBU Waziri wa Afya,Maendeleo ya Jamii,Jinsia ,Wazee na Watoto Dkt. Faustine Ndugulile amemuagiza Mganga Mkuu wa Wilaya ya Mpwapwa  Dkt. Said Mawjji kuandaa maoteo ya mahitaji ya dawa mapema na kupeleka Bohari kuu ya Dawa (MSD) kwa ajili ya upatikanaji huo na sio kununua dawa kiholela.
Hayo ameyasema wakati wa ziara yake kwa ajili ya kuangalia miundo mbinu pamoja na upatikanaji wa dawa na huduma za afya zitolewazo katika wilaya ya Mpwapwa mkoani Dodoma aliyoifanya jana.
“Katika milioni 57 ya kununua dawa laki saba tu ndo imeenda MSD zilizobaki zimeenda kwa mshitiri mwingine ambapo ni uagizaji dawa kiholela kwani mmeshindwa kufuata taratibu za uagizaji dawa wakati dawa hizo zinapatikana MSD” alisema Dkt. Ndugulile.
Aidha Dkt. Ndugulile alimuagiza Dkt. Mawjji kuhakikisha upanikaji wa dawa zote muhimu zinapatikana kwa asilimia 80 katika vituo vya afya wilayani hapo kama ilivyofikiwa na MSD katika kusambaza dawa hapa nchini ili kuondokana na tatizo la uhaba wa dawa ambapo ni kipaumbele cha Serikali kwa uapande wa sekta ya afya nchini.
Dkt. Ndugulile alimuagiza DMO wa Mpwapwa mpaka kufikia Desemba 13 mwaka huu awe tayari amewasilisha nyaraka za uagizaji dawa zote kuanzia Julai 2017mpaka Septemba mwaka huu ili kujiridhisha na utaratibu wao wa uagizaji dawa.
Mbali na hayo Dkt. Ndugulile amemuagiza DMO huyo kujitahidi kuongeaa baadhi ya watumishi katika kituo cha afya cha Kibakwe kilichopo katika tarafa ya Kibakwe Wilayani Mpwapwa kwani wanahitajika watumishi akiwemo mtaalam wa maabara na mfamasia wa kituo ili kuleta ufanisi katika huduma za afya kituoni hapo.
Aidha Dkt. Ndugulile ameumbia uongozi wakituo cha afya Kibakwe na pamoja na wanakijiji kuwa Serikali imetenga milioni 500 kwa ajili ya ujenzi na  ukarabati wa jengo la upasuaji wa dharura kwa akina mama wajawazito,nyumba za watumishi pamoja na ununuzi wa  vifaa tiba ili kuokoa maisha ya akina mama wanapopata uzazi tata wakati wa kujifungua
Katika kituo hicho cha afya Kibakwe Naibu Waziri huyo alikutana na changamoto ya tofauti ya dawa kwenye fomu za kuagiza dawa MSD na zile za kununua dawa hizo kwa mshitiri wa nje hali iliyomlazimu Dkt.Ndugulile kuanza kuhakikia fomu moja kwa dawa moja hadi nyingine na kugundua ubadilishaji wa aina za dawa zilizoagizwa MSD na baadae kwa mnunuzi wa nje.
Hata hivyo Dkt.Ndugulile aliwakanya watumishi wa stoo ya dawa ya kituo hicho kuacha kufanya mchezo huo wa kubadilisha mahitaji ya dawa pale wanapokosa MSD na kiruhusiwa kununua nje kwani Serikali ya awamu ya tano imejipanga na kuhakikisha upatikanaji wa dawa katika vituo vya afya kote nchi ni zaidi ya asilimia 80 na hivyo kuwataka wakazi wa Kibakwe kusimamia kwa makini matumizi ya dawa kituoni hapo.

0 on: "DKT. NDUGULILE AMPA MAAGIZO DMO MPWAPWA."