Like us on Facebook

Inaendeshwa na Blogger.

Tafuta katika Blogu Hii

Kumbukumbu la Blogu

Instagram

visitors

display number of visitors

Popular Posts

Pages

Flickr Images

Jumatano, 6 Desemba 2017

WAZIRI UMMY ATAKA UTARATIBU WA UONGOZI KWENYE VITUO VYA AFYA UFATWE


Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mh. Ummy Mwalimu akisisitiza jambo mbele ya Viongozi na Wananchi wa Wilaya ya Chamwino wakati alipotembelea kujionea Usafi wa mazingira na matumizi ya Choo katika Wilaya hiyo.


Mkuu wa Wilaya ya Chamwino  Mh. Vumilia Nyamonga akiongea na wananchi wake (hawapo kwenye picha) juu ya Usafi wa mazingira na matumizi ya choo, katika ziara ya Waziri wa Afya katika Wilaya hiyo mjini Dodoma, kushoto ni Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii,Jinsia, Wazee na Watoto Ummy Mwalimu na kulia kwake ni Mganga Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Dkt. James Charles.

Mganga Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Dkt. James Charles akijibu hoja ya mwananchi wa Kijiji cha Humekwa mbele ya Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mh. Ummy Mwalimu (hayupo kwenye picha) kuhusu upatikanaji wa kadi za matibabu ya wazee wilayani hapo.

 Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mh. Ummy Mwalimu akiteta jambo na Elizabeth Arthur wakati alipotembelea kujionea Usafi wa mazingira na matumizi ya Choo katika Wilaya hiyo.

 Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mh. Ummy Mwalimu akiongea na mkazi wa Kijiji cha Humekwa Wilaya ya Chamwino Bi Cesilliah Isaya aliyefanikiwa kujenga choo chenye ubora kwa gharama ndogo ya shiringi 55,000 tu.

 Kikundi cha ngoma kutoka Kijiji cha Humekwa kikitoa Burudani mbele ya Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mh. Ummy Mwalimu wakati alipofanya ziara ya kujionea Usafi wa mazingira na matumizi ya Choo katika Wilaya hiyo ya Chamwino Mkoani Dodoma.

 Wanafunzi wa Shule ya Msingi na Wakazi wa Kijiji cha Humekwa waliojumuika katika kuunga mkono ziara ya Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mh. Ummy Mwalimu (hayupo kwenye picha) ili kujionea Usafi wa mazingira na matumizi ya Choo katika Wilaya hiyo ya Chamwino Mkoani Dodoma.

 Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mh. Ummy Mwalimu akifuatilia kwa ukaribu ratiba  katika kituo kidogo cha Afya Kijiji cha Humekwa wakati wa ziara yake katika Wilaya ya Chamwino Mkoani Dodoma.

 Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mh. Ummy Mwalimu akikagua moja ya choo wakati alipofanya ziara katika Kijiji cha Humekwa Wilaya ya Chamwino Mkoani Dodoma ili kuhamasisha usafi wa mazingira na choo.

 Mwanakijiji wa Kijiji cha Humekwa Bi Evaline Gidore akisoma risala mbele ya mgeni rasmi Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mh. Ummy Mwalimu (hayupo kwenye picha) wakati alipofanya ziara ya kujionea Usafi wa mazingira na matumizi ya Choo katika kijiji hicho mapema leo.

 Diwani wa kata ya Aneti Mh. Peter Chidawali akitoa mapendekezo mbele ya Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mh. Ummy Mwalimu (hayupo kwenye picha) kuhusu maboresho katika huduma za Afya kijijini hapo.

 Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mh. Ummy Mwalimu akiteta jambo na Mganga Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Dkt. James Charles wakati wa ziara ya kujionea Usafi wa mazingira na matumizi ya Choo katika Wilaya hiyo, wa katikati ni Mkuu wa Wilaya ya Chamwino  Mh. Vumilia Nyamonga.


Waziri wa Afya, maendeleo ya jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mh. Ummy Mwalimu akiongoza  ziara katika kijiji cha Humekwa Wilaya ya Chamwino mapema leo Mkoani Dodoma.






NA WAMJW-DODOMA

SERIKALI kupitia Wizara ya Afya,Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto imedhamiria kuhakikisha kuwa kila Kituo cha Afya au Zahanati yoyote inaongozwa na kusimamiwa na mganga na sio mhudumu wa afya au nesi kama inavyofanyika kwenye baadhi ya vituo vya afya .

Hayo yamesemwa na Waziri wa afya ,Maendeleo ya Jamii Jinsia Wazee na watoto Mheshimiwa Ummy Mwalimu wakati wa ukaguzi wa usafi wa mazingira  leo Mkoani Dodoma Wilaya ya Chamwino kata ya aneti Kijiji cha humekwa  kuelekea uzinduzi  wa awamu ya pili ya kampeni ya kitaifa ya usafi wa mazingira iliyobeba ujumbe wa nipo tayari  ambapo Makamuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan anatarajia kuwa mgeni rasmi.

"Hatua ya kuimarisha  upatikanaji wa dawa, upatikanaji wa vifaa na vifaa tiba hususani vya dharura na upasuaji sanjari na kuweka mazingira safi ya upatikanaji wa maji na vyoo safi na salama ili kupunguza magonjwa na vifo vitokanavyo na kutokuwepo kwa huduma bora za  maji na afya kwa wakati ndiyo lengo letu" alisema Waziri Ummy.


 Aidha Waziri Ummy amesema kuwa kabla ya Serikali ya Mhe. Rais John Pombe Magufuli haijaingia madarakani bajeti ya dawa ya wilaya ya chamwino ilikuwa milioni 113 lakini mwaka jana bajeti ya dawa  ilikuwa milioni 436 ambapo katika mwaka wa pili wametengewa milioni 505 hali inayoonesha jitihada za dhati za serikali ya awamu ya tano kuboresha hali ya  afya ya wananchi hususani waliokuwa Vijijini.

Mbali na hayo Waziri Ummy amewataka wananchi wa kijiji cha Humekwa kukata kadi ya matibabu za CHF kwani zinarahisha upatikanaji wa huduma za afya kwa urahisi na kupunguza gharama .

Aidha Waziri Ummy amesema kuwa wananchi ambao wana ugonjwa kifua kikuu hawana  budi kuwahi hospitali na vituo vya kutolea huduma za afya kwa ajili ya kupata dawa ili kuokoa maisha yao kwani dawa hizo hazilipiwi gharama yoyote.

Kwa upande wake Diwani wa Kata ya Aneti  Peter Chidawali ameiomba Serikali kuwasaidia Wananchi wa Humekwa katika hatua iliyofikiwa kwenye ujenzi wa jengo la upasuaji ambalo wananchi wanajitolea michango yao kujenga ili likamilike kwa matumizi yaliyokusudiwa.

Kwa upande wake Msomarisala wa Kijiji cha Homekwe Evaline Gidore amebainisha kuwa kampeni ya usafi wa mazingira na ujenzi  wa vyoo bora imeasaidia kupunguza idadi ya wagonjwa walioathiriwa na magonjwa  yatokanayo na uchafuzi wa mazingira .

"Kampeni hii imechangia kuepuka magonjwa hatari kama vile kuhara damu, typhoid na minyoo kutoka wagonjwa138 mwezi  disemba 2015 hadi kufikia wagonjwa 26 Novemba Mwaka huu kwa vile tumejitahidi kuzingatia usafi wa mazingira na matumizi ya vyoo bora"Alisema Bi Eveline.


0 on: " WAZIRI UMMY ATAKA UTARATIBU WA UONGOZI KWENYE VITUO VYA AFYA UFATWE"