Like us on Facebook

Inaendeshwa na Blogger.

Tafuta katika Blogu Hii

Kumbukumbu la Blogu

Instagram

visitors

display number of visitors

Popular Posts

Pages

Flickr Images

Ijumaa, 8 Desemba 2017

WATANZANIA WATAKIWA KUZINGATIA MATUMIZI YA VYOO BORA


Makamu wa Rais wa Jamhuri ya muungano wa Tanzania Mh. Samia Suluhu Hassan akisisitiza jambo mbele ya wadau na wakazi wa Chang’ombe Mkoa wa Dodoma katika Uzinduzi wa kampeni ya Usichukulie Poa Nyumba ni Choo iliyofanyika katika viwanja vya shule ya msingi Chang’ombe.

Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mh. Ummy Mwalimu akimkabidhi zawadi Makamu wa Rais wa Jamhuri ya muungano wa Tanzania Mh. Samia Suluhu Hassan baada ya kukabidhi zawadi kwa washindi wa usafi wa mazingira na vyoo bora kutoka halmashauri mbali mbali nchini Tanzania.

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya muungano wa Tanzania Mh. Samia Suluhu Hassan akiwa na Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mh. Ummy Mwalimu wakipiga makofi ishara ya kupongeza uzuri na usafi wa moja ya mfano wa choo bora.

Picha ya pamoja ikiongozwa na Makamu wa Rais wa Jamhuri ya muungano wa Tanzania Mh. Samia Suluhu Hassan wapili kutoka kushoto wakiwa mbele ya choo bora, tukio lililifanyika katika viwanja vya shule ya msingi Chang’ombe Mkoani Dodoma. Wakwanza ni Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mh. Ummy Mwalimu, watatu ni Elizabeth Arthur na wa mwisho ni Waziri wa TAMISEMI Suleiman Jaffo.

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya muungano wa Tanzania Mh. Samia Suluhu Hassan wapili kutoka kushoto akiwapungia mkono wakazi wa Chang'ombe na wadau wa masuala ya mazingira na usafi wa vyoo. akwanza ni Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mh. Ummy Mwalimu, watatu ni Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Dkt. Mahenge.

Timu ya viongozi wa serikali ikiongozwa na Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mh. Ummy Mwalimu wakiwa tayari kumpokea mgeni rasmi Makamu wa Makamu wa Rais wa Jamhuri ya muungano wa Tanzania Mh. Samia Suluhu Hassan.

Mratibu wa Kampeni ya kitaifa ya Usafi na Mazingira kutoka Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto  Anyitike Mwakitalima akitoa maelezo mbele ya Makamu wa Rais wa Jamhuri ya muungano wa Tanzania Mh. Samia Suluhu Hassan na Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mh. Ummy Mwalimu.

Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mh. Ummy Mwalimu akimuelekeza jambo Waziri wa TAMISEMI Suleiman Jaffo wakiwa katika banda la maonesho la Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto.

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya muungano wa Tanzania Mh. Samia Suluhu Hassan akipata maelezo kutoka kwa Meneja Mpango wa Simavi Thea Bongertman, wa kwanza ni Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mh. Ummy Mwalimu.

Kikundi cha Burudani kutoka eneo la Chang’ombe Mkoani Dodoma, kikionesha manjonjo mbele ya mgeni rasmi Makamu wa Raisi wa Jamhuri ya muungano wa Tanzania Mh. Samia Suluhu Hassan na viongozi wengine wa Serikali.

Katibu Tawala wa Mkoa wa Arusha akipokea zawadi ya Usafi bora ya gari kutoka kwa Makamu wa Rais wa Jamhuri ya muungano wa Tanzania Mh. Samia Suluhu Hassan.

Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mh. Ummy Mwalimu akiwa na Naibu wa Wizara hiyo Mh. Faustine Ndugulile wakimkabidhi zawadi ya Usafi bora Mwakilishi kutoka Halmashauri ya Wilaya ya Njombe Bi Eveline Kibenya.

Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mh. Ummy Mwalimu akiwa na Naibu wa Wizara hiyo Mh. Faustine Ndugulile na Elizabeth Arthur katika bango la kampeni ya “Usichukulie Poa Nyumba ni Choo”

Picha ya pamoja ikiongozwa na Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mh. Ummy Mwalimu akiwa na Naibu wa Wizara hiyo Mh. Faustine Ndugulile wakiwa pamoja na Washindi Usafi na vyoo bora kutoka Halmashauri mbali mbali nchini.

NA WAMJW-DODOMA.

WATANZANIA  wanapaswa kuzingatia mambo  ya msingi hususani matumizi ya vyoo bora  ili kuepuka magonjwa  ya kuambukiza na mlipuko kwa ajili ya kujenga Tanzania ya Viwanda pasipokuwa na adui mkubwa wa maradhi nchini.

Hayo yamesemwa na Makamu wa Rais wa Jamhuri  ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan wakati wa uzinduzi wa awamu ya pili ya kampeni ya taifa ya mazingira uliyofanyika mkoani leo Mkoani Dodoma.

“Watanzania tunapaswa kuzingatia mambo ya msingi ikiwemo kutumia vyoo bora ,kunawa mikono kwa maji safi yanayotiririka na sabuni pamoja na kuchemsha maji ya kunywa ili kuepuka magonjwa mlipuko nchini” alisema Mhe. Samia.

Aidha Mhe. Samia amesema kuwa watanzania tunatakiwa kuwa kipaumbele kwenye usafi wa mazingira kwa tumepoteza kiasi cha shilingi bilioni 440 kutokana na hali duni ya usafi wa hasa ukosefu wa huduma ya vyoo bora.

Kwa mujibu wa Makamu wa Rais Mhe. Samia Suluhu  Hassan amesema kuwa takwimu zinaonyesha watu wapatao elfu thelathini huugua magonjwa ya kuhara kila mwaka na baadhi yao hupoteza maisha hivyo tunatakiwa kuzingatia usafi wa mazingira  ili kuepuka idadi ya wastani wa watu 83 kwa siku.

“Taifa hatuna kuwekeza nguvu na rasilimali zetu katika suala la usafi wa mazingira ikiwemo matumizi ya maji safi na vyoo bora ili kufikia malengo yetu ya kitaifa pampja nay ale ya kidunia” alisema Mhe. Samia Suluhu.

Mbali na hayo  Mhe. Samia Suluhu Hassan amesema kuwa endapo watoto wataendlea kuishi kwenye  mazingira machafu ni hatarishi kwani kuna uwezekano wa kuwa na watoto waliodumaa kimwili na kiakili.

Kwa upande wake Waziri wa afya,Maendeleo ya Jamii,Jinsia,Wazee na Watoto Me. Ummy Mwalimu amesema kuwa Tanzania inaendelea kupambana na ugonjwa wa kipindupindu ambao ulirejea tena mwaka 2015 baada ya kupotea takribani miaka minne.

“ Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli ameonesha kusikitishwa kwake kutokana na uwepo wa kipindupindu nchini hivyo watanzania hatuna budi kuwa wasafi wa mazingira ili kuepuka mlipuko wa ugonjwa huo” alisema Waziri Ummy.

Aidha Waziri Ummy amewataka watanzania kupambana na adui wa afya kwa kutunza mazingira na kuepuka vishiria vya magonjwa mbalimbali  kuliko kulalamika ukosefu wa dawa kwani kinga ni bora kuliko tiba.

Kwa upande Waziri wa Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) Bw. Suleiman Jaffo amesema kuwa kupitia ofisi yake atahakikisha anasimamia na kuwaagiza watendaji wake  wa ngazi zote kusimamia  usafi wa mazingira kama alivyoagizwa na Makamu wa Rais Mhe. Samia Suluhu Hassan.

Kampeni iliyozinduliwa leo na Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan  jijini Dodoma ni ya awamu ya pili ya usafi wa mazingira ambayo imebeba ujumbe usemao “USICHUKULIE POA NYUMBA NI CHOO” imeenda sambamba na ugawaji wa zawadi na vyeti kwa waliofanya vizuri kwenye usafi wa mazingira ambapo Halmashauri ya Mji wa Njombe umeibuka kidedea na kupata zawadi ya Trekta.

0 on: "WATANZANIA WATAKIWA KUZINGATIA MATUMIZI YA VYOO BORA"