Like us on Facebook

Inaendeshwa na Blogger.

Tafuta katika Blogu Hii

Kumbukumbu la Blogu

Instagram

visitors

display number of visitors

Popular Posts

Pages

Flickr Images

Jumamosi, 9 Desemba 2017

HOSPITALI YA SARATANI YA OCEAN ROAD YATOA HUDUMA YA UCHUNGUZI WA SARATANI KWA WATU WENYE ALBINO

 





Hospitali ya Saratani ya Ocean Road imefanikisha kutoa huduma za uchunguzi wa Saratani kwa watu wenye albino.

Hayo yamesemwa na Mkurugenzi wa huduma za jamii hospitali ya Saratani ya Ocean Road Dkt. Cyrpian katika ziara yake Mkoani Simiyu.

Dkt. Cyrpian alibainisha kuwa Uchunguzi huo umefanywa kwa kushirikiana na Taasisi ya Albino nchini huku likijumuisha kuwafundisha wataalamu wa Afya na kuanzisha Kliniki za kutoa huduma  hizi.

“tumefanyia uchunguzi albino 16 Kati ya hao 2 wana saratani, watu 12 wenye dalili za awali za saratani tumewatibu papo hapo kwa tiba baridi huku wawili wakiwa vizuri” alisema Dkt. Dkt. Cyrpian.

Dkt. Cyrpian alibainisha kuwa zoezi hili limeanza tangu Desemba 3 mpaka Desemba 9 Wilayani Misungwi liliwalenga wanafunzi 65 kutoka shule ya msingi Misungwi Mitindo huku wanafunzi 50 wakipewa mafuta ya albino yakujikinga na jua. Wanafunzi 2 walikuwa na dalili za aratani ya ngozi na walitibiwa kwa tiba baridi (cryotherapy) na 13 walikuwa hawana shida.

Dkt. Cyrpian alikiri kuwafundisha madaktari katika hospitali ya wilaya  ya Misungwi, hospital ya shinyanga na Simiyu.

0 on: "HOSPITALI YA SARATANI YA OCEAN ROAD YATOA HUDUMA YA UCHUNGUZI WA SARATANI KWA WATU WENYE ALBINO"