Like us on Facebook

Inaendeshwa na Blogger.

Tafuta katika Blogu Hii

Kumbukumbu la Blogu

Instagram

visitors

display number of visitors

Popular Posts

Pages

Flickr Images

Jumamosi, 23 Desemba 2017

SERIKALI YATARAJIA KUANZISHA BIMA YA AFYA KWA WATU WOTE

Naibu Waziri Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Faustine Ndugulile akisisitiza jambo mbele ya baadhi ya Watumishi(hawapo kwenye picha) wa Taasisi ya Kiuma inayomiliki chuo cha Uuguzi, Kituo cha Afya na Kanisa la Upendo wa Kristo Kiuma.

Mkurugenzi Mkuu wa chuo cha Uuguzi na Mwenyekiti wa Kanisa la Upendo wa Kristo Kiuma Dkt. Matomola akiwasilisha taarifa ya taasisi hiyo mbele ya Naibu Waziri wa Afya Dkt Faustine Ndugulile (Hayupo kwenye picha) wakati wa ziara yake katika Wilaya ya Tunduru.

Naibu Waziri wa Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Faustine Ndugulile akikagua daftari la baadhi ya Vifaa vya Maabala wakati alipofanya ziara katika Wilaya ya Tunduru Kituo cha Afya cha Kiuma.

Naibu Waziri wa Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Faustine Ndugulile akikagua baadhi ya vifaa katika chumba cha Kompyuta wakati alipofanya ziara katika Wilaya ya Tunduru Kituo cha Afya cha Kiuma.

Naibu Waziri wa Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt Faustine Ndugulile akipata maelezo kutoka kwa Msimamizi wa kike(Matroni) wa Kituo cha Afya cha Kiuma Maria Ntazama,  kulia ni Mkurugenzi Mkuu wa Hospitali ya Kiuma na Mwenyekiti wa Kanisa la Upendo wa Kristo Kiuma Dkt. Matomola.

Naibu Waziri wa Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Faustine Ndugulile akikagua moja ya darasa katika chuo cha Uuguzi Kiuma wakati alipofanya ziara katika Wilaya ya Tunduru Kituo cha Afya cha Kiuma.

Naibu Waziri wa Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Faustine Ndugulile akikagua vitabu katika maktaba ya chuo cha Uuguzi na ukunga Kiuma wakati alipofanya ziara katika Wilaya ya Tunduru.

Naibu Waziri wa Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Faustine Ndugulile (katikati) wakiwa katika ziara yake Wilayani  Tunduru, wakwanza ni Mkurugenzi wa Mafunzo Wizara Ya Afya Dkt. Otilia Gowele na kulia kwake ni Mkurugenzi Mkuu wa taasisi ya Kiuma ambae pia ni Mwenyekiti wa Kanisa la Upendo wa Kristo Dkt. Matomola.

Naibu Waziri wa Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Faustine Ndugulile akipata maelezo kutoka kwa Mkurugenzi Mkuu wa taasisi ya Kiuma ambae pia ni Mwenyekiti wa Kanisa la Upendo wa Kristo Dkt. Matomola, wakati akikagua  mabweni ya chuo cha Uuguzi na ukunga Kiuma kilichopo Wilaya ya Tunduru.

Baadhi ya wanafunzi wa Chuo cha uuguzi na ukunga Kiuma kilichopo Wilaya ya Tunduru wakifuatilia hotuba kutoka kwa Naibu Waziri wa Wizara ya Afya Dkt Faustine (hayupo kwenye picha),  wakati alipofanya ziara katika taasisi hiyo ya Kiuma Wilayani Tunduru.

Naibu Waziri wa Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Faustine Ndugulile akikagua kwa umakini Daftari la opokeaji Dawa pembeni yake ni Afisa wa Kliniki Hassan Miengende.

Naibu Waziri wa Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Faustine Ndugulile akikagua Kadi za dawa wakati alipofanya ziara katika kituo cha Afya Mkasale Wilayani Tunduru.

Wanchi wa Kijiji cha Mkasale wakifuatilia kwa makini agizo kutoka kwa Naibu Waziri wa Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Faustine Ndugulile juu ya usimamiaji wa rasilimali fedha katika kituo chao cha Afya.


Na WAMJWW, TUNDURU
Serikali ya awamu ya tano kupitia Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto imejipanga kuanzisha mfuko wa Bima ya Afya kwa watu wote nchini jambo litalosaidia kupunguza gharama za matibabu kwa kiasi kikubwa.

Hayo yamesemwa na Naibu Waziri wa Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Faustine Ndugulile wakati alipofanya ziara katika Wilaya ya Tunduru Mkoani Ruvuma katika Taasisi ya Kiuma inayomiliki Hospitali, Chuo cha Uuguzi na Kanisa la Upendo wa Kristo.

“Tunatambua kwamba si kila mtu anamudu gharama hizo, kwa bahati mbaya ugonjwa unakuja wakati hatuja jiandaa, serikali imeliona hilo, pamoja na mikakati tunayoendelea nayo ya Bima ya Afya ya NHIF na CHF, tunatarajia kuja na utaratibu wa bima ya afya kwa wote, suala la matibabu lisiwe la kuwaza” alisema Dkt. Faustine Ndugulile.

Dkt. Faustine aliendelea kusema kwamba, Serikali inaendelea kufanya vizuri barani Afrika na Dunia kwa ujumla kwa upande wa utoaji chanjo, kwani imefikia asilimia 97 ya walengwa  wote wanaohitaji chanjo nchini jambo linalosaidia kutunza Afya za watu katika jamii.

“Tumefkia hatua kubwa sana ya walengwa wote wanaohitaji kupata chanjo, jambo linaloifanya Tanzania kuwa moja kati ya nchi chache sana zilizofikia malengo hayo” alisema Dkt. Faustine

Aidha Serikali imetoa fedha kwa Vituo vya Afya 172 kwa lengo la kujenga thieta, Chumba cha Kujifungulia, Wodi ya Wazazi, nyumba ya Watumishi na Maabara, Huku Wilaya ya Tunduru ikifanikiwa kupata fedha hizo kwa vituo viwili, kikiwepo kituo cha Afya cha Mkasale.

Kwa upande mwingine  Dkt. Faustine ameupongeza uongozi wa Taasisi ya Kiuma kwa kazi kubwa na nzuri wanayoifanya ikiwemo kutoa huduma za afya kwa wananchi, kutoa ajira, jambo linalotokana na uwekezaji mkubwa uliofanywa na Taasisi hiyo hivyo kuipunguzia mzigo Serikali katika Nyanja hizo.

Nae Mkurugenzi Mkuu wa Chuo cha Uuguzi ambae pia ni Mwenyekiti wa Kanisa la Kanisa Upendo wa Kristo Kiuma Dkt. Matomola ameiomba Serikali kupitia Naibu Waziri wa Afya Dkt. Faustine Ndugulile itambue huduma inayotolewa chuoni hapo na kuwaongezea Watumishi, pia Serikali iwasaidie kuchangia mahitaji madogo madogo kama vitabu, maabara na vifaa.

Katika ziara hiyo Dkt. Ndugulile alifanikiwa kutembelea Kituo cha Afya Mkasale katika Wilaya hiyo ya Tunduru na kujiridhisha na hali ya upatikanaji wa dawa huku akiwasisitiza wananchi wasiuziwe dawa zote muhimu kwani hali ya upatikanaji wa Dawa ni nzuri maeneo yote na sasa ni wastani wa asilimia 80.

Aidha Dkt. Ndugulile amewahakikishia wanakijiji wa Mkasale kuwa kituo chao cha Afya kipo katika Vituo 172 vilivyopata mgao wa fedha za ujenzi wa maabara, chumba cha kujifungulia, Wodi ya wazazi, thieta, na kuwataka kusimamia vizuri fedha hizo ili kuweza kuboresha Zaidi huduma katika kituo hicho.

Nae Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa  Wilaya ya Tunduru Mhe. Chiza Marando wakati akiwasilisha taarifa ya Wilaya alisema kuwa Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru ina jumla ya vituo vya kutolea huduma za Afya 65 zikiwemo Hospitali 3 Vittuo vya Afya 5 na Zahanati 57 kati ya hizo 52 ni za serikali, 3 ni za mashirika ya dini na 2 zinamilikiwa na watu binafsi.

Mhe. Chiza Marando aliongeza kuwa Halmashauri ya Tunduru inakabiriwa na uhaba mkubwa wa watumishi wa kada ya Afya hali inayopelekea changamoto kubwa katika utoaji wa huduma kwa wananchi katika halmashauri hiyo.
“Tunduru ina jumla ya watumishi 339 wa Serikali sawa na asilimia 26.3 kati yawatumishi 1286 wanaohitajika na kufanya upungufu wa watumishi 974 sawa na asilimia 73.6, huku upungufu mkubwa ukiwa  katika kada ya madaktari, waganga, maafisa Afya na wauguzi.” Alisema Mhe. Chiza Marando

Kwa upande mwingine Mhe. Marando aliongeza kwa kusema hali ya utoaji huduma imeongezeka ikiwemo Huduma ya Chanjo kutoka 94 mwaka 2015 hadi kufikia asilimia 95 mwaka 2016 na kwa mwaka 2017 kiwango kimefikia asilimia 92.

Aidha Mhe. Chiza Marando alisema kuwa Wilaya hiyo inatoa huduma kwa makundi maalumu kwa kuzingatia Sera ya Wizara ya Afya kwa kutoa vitambulisho vya matibabu ya Wazee kwa baadhi ya kata zilizofanyiwa utambuzi, tayari vitambulisho 1234 vimetolewa kwa Wazee.

0 on: " SERIKALI YATARAJIA KUANZISHA BIMA YA AFYA KWA WATU WOTE"