Like us on Facebook

Inaendeshwa na Blogger.

Tafuta katika Blogu Hii

Kumbukumbu la Blogu

Instagram

visitors

display number of visitors

Popular Posts

Pages

Flickr Images

Jumapili, 31 Desemba 2017

TANGAZO KWA UMMA



JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA
WIZARA YA AFYA, MAENDELEO YA JAMII, JINSIA, WAZEE NA WATOTO


Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto anawatangazia wanafunzi wote walioko vyuoni wanaosoma masomo ya Shahada za Uzamili (Masters Degree) katika fani za Afya kwamba Wizara imepata fedha zitakazowezesha ufadhili (Sponsorship) kwa baadhi ya Wanafunzi, na kwa baadhi ya maeneo, kwa mwaka wa masomo 2017/2018.
Hivyo, kwa Tangazo hili, wale wote wenye nia ya kuomba ufadhili wanatakiwa kuwasilisha maombi yao.
Ufadhili huu ni kwa ajili ya kulipiwa ada ya mafunzo (Tuition fee), pamoja na posho ya utafiti pindi mwanafunzi anapokuwa kwenye kipindi cha kufanya utafiti kama sehemu ya mafunzo yake (Dissertation allowance).
Vigezo vitakavyotumika kuchagua watakaowasilisha maombi yao ni hivi vifuatavyo :

1. Kuwasilishwa kwa maombi rasmi ya ufadhili
2. Mwombaji kuwa Raia wa Tanzania.
3. Awe amedahiliwa Chuoni kuanza masomo kwa mwaka wa kwanza 2017/2018
4. Kipau mbele kitatolewa kwa:
a. Watumishi wa Serikali waliomo kwenye sekta ya Afya wanaofanya kazi katika vituo vilivyoko Wilayani/Mikoani ambao baada ya mafunzo watarudi kuendelea kufanya kazi katika vituo vyao vya awali, au watapangiwa vituo vya kazi sehemu nyingine yeyote nchini
b. Waombaji waliodahiliwa katika fani ambazo ni za msingi katika utoaji wa huduma za rufaa katika Hospitali za Rufaa za Mikoa. Nyanja hizo ni Anaesthisiology, Surgery, Neurosurgery, Obstetrics and Gynaecology, Orthopaedics Surgery, Emergency Medicine, Paediatrics, Internal Medicine, Critical Care in Nursing na Midwifery and Womens Health
c. Waombaji waliodahiliwa katika nyanja za Ubingwa/Ubingwa wa Juu (Specialities na Super-specialities) zenye umuhimu mkubwa katika Hospitali za Kitaifa (kama Cardiology, Nephrology, na Oncology) ili kujenga uwezo wa ndani ya nchi katika jitihada za kupunguza wagonjwa wa rufaa wanaotibiwa nje ya nchi.
5. Aidha, mwombaji atatakiwa awe:
a. na barua ya ruhusa ya masomo kutoka kwa mwajiri wake (iambatanishwe)
b. Tayari kuingia mkataba wa kuitumikia Serikali kwa muda usiopungua miaka 5 baada ya kuhitimu mafunzo.
c. Hana ufadhili mwingine wa masomo yake

Tangazo hili linafuta ufadhili uliokuwa umetolewa awali kwa wanafunzi wa mwaka wa kwanza wanaosoma masomo ya Shahada za Uzamili katika Chuo Kikuu cha Afya na Sayansi Shirikishi Muhimbili (MUHAS) na Chuo Kikuu Dodoma (UDOM). Hivyo wanafunzi waliokuwa wamechaguliwa watapaswa kuomba upya kwa kuzingatia vigezo vilivyowekwa kwenye tangazo hili.
Aidha kwa kuwa wanafunzi wamekwisha ripoti vyuoni wahakikishe barua za maombi zinapitishwa kwa Wakuu wa Vyuo ili kuthibitisha kuwa mwanafunzi yuko chuoni.
Tangazo hili linahusu wale walioko vyuoni kwa mwaka wao wa kwanza wa masomo wa 2017/2018 tu.
Mwisho wa kupokea maombi haya ni tarehe 12/01/2018.
Maombi yote yaelekezwe kwenye anuani ifuatayo;

Katibu Mkuu,
Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto
Chuo Kikuu Dodoma,
Kitivo cha Sanaa na Sayansi ya Maendeleo ya Jamii
S.L.P 743
DODOMA

0 on: "TANGAZO KWA UMMA"