Like us on Facebook

Inaendeshwa na Blogger.

Tafuta katika Blogu Hii

Kumbukumbu la Blogu

Instagram

visitors

display number of visitors

Popular Posts

Pages

Flickr Images

Jumatano, 20 Desemba 2017

WAUGUZI NI CHACHU YA HUDUMA BORA NCHINI

Mkurugenzi wa Idara ya Uuguzi na Ukunga kutoka Wizara ya Afya Gustav Moyo akiwasilisha mada wakati wa mafunzo ya maadili kwa wauguzi wakuu wa Mikoa na hospitali za Kitaifa na za Rufaa za kanda unaoendelea chuo cha Uuguzi Mirembe Mkoani Dodoma

Wauguzi wakuu toka mikoa mbalimbali wakifuatilia mada zinazowasilishwa kwenye mafunzo hapo.mafunzo hayo yana lenga kuwakumbusha uadilifu na maadili ya uuguzi wakati wa utoaji huduma za afya nchini.

Baadhi ya wauguzi wa mikoa wakijadili kwenye makundi mikakati ya nini kifanyike katika kutekeleza majukumu yao ili kuondokana na malalamiko ya taaluma yao kutoka kwa wananchi.

 Wauguzi wakuu wakiendelea na kazi kwenye makundi.

Mkurugenzi wa Uuguzi na Ukunga Gustav Moyo akiongea na wauguzi wakuu wa mikoa kwenye mafunzo hayo.



Na WAMJW-Dodoma

Wauguzi wakuu wa Mikoa na hospitali za Taifa na Rufaa za Kanda wametakiwa kusimamia maadili ili kupunguza malalamiko toka kwa wananchi.

Hayo yamesemwa  jana na Katibu Mkuu Wizara ya Afya,Maendeleo ya Jamii,Jinsia,Wazee na Watoto Dkt.Mpoki Ulisubisya wakati wa mafunzo juu ya maadili kwa wauguzi wakuu yanayoendelea mjini hapa kwenye chuo cha uuguzi na ukunga Mirembe

Dkt.Mpoki alisema  hivi sasa kumekua na malalamiko kutoka kwa wananchi juu ya huduma wanazozitoa hivyo kupitia mafunzo hayo wanapaswa kusimamia ipasavyo maarifa na mikakati watakayojiwekea ili kuleta mabadiliko makubwa na kuondoka malalamiko hayo.

"Jamii na Serikali inawategemea sana katika usimamizi wa huduma bora nchini,naamini kwamba ninyi mna nguvu,nia na maarifa katika kuboresha maadili ya wauguzi wote nchini,hivyo ni muhimu mkasimamie"alisema Dkt.Mpoki

Aidha, alisema wizara yake inatambua umuhimu wa kuboresha maadili hususani kwa wauguzi,hivyo kuwapatia mafunzo kama ni muhimu kwa taaluma yao.

"Kumekuwepo na malalamiko na ongezeko kubwa la vitendo visivyo vya kiadilifu kwa watumishi wa afya ikiwa ni pamoja na kauli mbovu kwa wagonjwa,naamini kwa mafunzo haya changamoto zote mtazijadili na kusaidia kuondokana na malalamiko toka kwa wananchi"

Naye Mkurugenzi wa huduma za Uuguzi na Ukunga wizara ya afya Gustav Moyo alisema lengo kuu la mafunzo hayo ni kuwajengea uwezo wa namna gani ya kuboresha uadilifu na maadili ya sehemu zao za kazi wauguzi nchini

Aidha,ametoa wito kwa wauguzi wote nchi kuzingatia Iadilifu,utu,upendo na maadili yao ya kwa kuipatia thamani stahiki taaluma yao kwani wauguzi ndio wanaokuwepo muda wote mahali pa kazi.
"Serikali ya awamu ya tano inasisitiza suala la uadilifu hivyo wananchi wanahimizwa kuwabaini na kuwasema ili kuwabaini baadhi ya  wanaokiuka maadaili au kufanya vitendo visivyozingatia maadili ili tuwachukulie hatua ama kurekebisha na tuweze kutoa huduma yenye viwango na inayokubalika na salama kwa wananchi".

0 on: " WAUGUZI NI CHACHU YA HUDUMA BORA NCHINI"