Like us on Facebook

Inaendeshwa na Blogger.

Tafuta katika Blogu Hii

Kumbukumbu la Blogu

Instagram

visitors

display number of visitors

Popular Posts

Pages

Flickr Images

Jumanne, 5 Desemba 2017

TANZANIA KUNUFAIKA NA MPANGO WA KINGA YA SARATANI YA SHINGO YA KIZAZI


Waziri wa Afya Mendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Ummy Mwalimu Leo ametembelewa na ujumbe wa  pamoja wa umoja wa Mataifa wa Mpango wa Kinga ya Saratani ya shingo ya Kizazi Duniani.

Waziri Ummy  ameushukuru ujumbe huko kwa kufika nchini na kwa kuichagua Tanzania kuwa Moja ya nchi sita duniani zitakazo nufaika na Mpango huu

Tanzania ni mojawapo wa nchi duniani zenye Tatizo ya saratani ya shingo ya kizazi.katika wanawake 100,000  kuna wanawake 54 wenye tatizo hilo na Vifo 32 katika wanawake 100,000 hiki ni kiwango kikubwa kwa nchi za afrika mashariki(Globocan,2014)

Katika hatua za  kujikinga na hali hii Wizara ya afya inafanya kazi na wadau mbalimbali wakiwemo Tanzania Youth Alliance (TAYOA),Medical Women Association of Tanzania, Wanawake na Maendeleo (WAMA) ,Tanzania Network for women living with HIV(TWN), Mbeya HIV network, T-Marc Tanzania na vyombo vya habari vya kitaifa na kijamii katika kuhamasisha kuishirikisha Jamii katika suala hili.

Wizara inafanya kila jitihada kuhakikisha Mgonjwa aliyethibitishwa kuwa na kansa anapata matibabu ya kibingwa maalum ya mionzi katika Hosipiali za Ocean Road na Bugando

0 on: "TANZANIA KUNUFAIKA NA MPANGO WA KINGA YA SARATANI YA SHINGO YA KIZAZI"