Like us on Facebook

Inaendeshwa na Blogger.

Tafuta katika Blogu Hii

Kumbukumbu la Blogu

Instagram

visitors

display number of visitors

Popular Posts

Pages

Flickr Images

Alhamisi, 14 Juni 2018

DKT. NDUGULILE HAIMIZA UTUNZAJI MZURI WA DAWA.

Naibu Waziri wa Afya,Maendeleo ya Jamii,Jinsia,Wazee na Watoto Dkt. Faustine Ndugulile akiongea na Wafamasia hawapo pichani wakati wa maadhimisho ya wiki ya Famasia yaliyofanyika leo jijini Dar es salaam.

Naibu Waziri wa Afya,Maendeleo ya Jamii,Jinsia,Wazee na Watoto Dkt. Faustine Ndugulile wa kwanza kushoto akipata maelezo juu ya dawa aliyoishika kutoka kwa Mkurugenzi wa kiwanda cha kutengeneza dawa Gullin Bw. Ashok Pandey kulia wakati wa maadhimisho ya wiki ya Famasia yaliyofanyika leo jijini Dar es salaam.

Naibu Waziri wa Afya,Maendeleo ya Jamii,Jinsia,Wazee na Watoto Dkt. Faustine Ndugulile kushoto akionesha juu Bango Kitita la famasia baada ya kulizindua wakati  wa maadhimisho ya wiki ya Famasia yaliyofanyika leo jijini Dar es salaam. Kulia ni Msajili wa Baraza la Famasia Bi. Elizabeth Shekirego 



Naibu Waziri wa Afya,Maendeleo ya Jamii,Jinsia,Wazee na Watoto Dkt. Faustine Ndugulile akiwakabidhi zawadi baadhi ya wadau wa Famasi kwa mchango wao katika sekta hiyo wakati wa maadhimisho ya wiki ya Famasia yaliyofanyika leo jijini Dar es salaam.


NA WAMJW-DAR ES SALAAM


NAIBU Waziri wa Afya,Maendeleo ya Jamii,Jinsia,Wazee na Watoto Dkt. Faustine Ndugulile amewaagiza wafamasia wa Hospitali za serikali kutunza dawa vizuri na mahali panapostahili ili kuweza kuepuka uharibifu wa dawa hizo.
Hayo ameyazungumza wakati wa maadhimisho ya wiki ya Famasia duniani yaliyofanyika leo jijini Dar es salaam yakiwa na lengo la kuimarisha na kuboresha fani hiyo nchini.
“Licha ya kutunza dawa  mahali salama wafamasia wanapaswa kutunza kumbukumbu za dawa hizo zinapoingia,zinapopokelewa ,zinapotolewa kwa wagonjwa na matumizi ili kuondoa uhaba wa dawa na kuthibitisha matumizi yake” alisema Dkt. Ndugulile.
Aidha Dkt. Ndugulile amesema kuwa wafamasia wanatakiwa kuwa waaminifu kazini kwani kuna badhi ya wafamasia wana tabia ya kuiba dawa  kwenye  vituo vyao vya kazi na kwenda kuuza nje ya kituo cha kutolea huduma za afya.
Mbali na hayo Dkt. Ndugulile amewaagiza Mganga Mkuu wa Serikali na Mfamasia Mkuu wa serikali kukaa pamoja na kujadili na kuwatengenezea mazingira wezeshi wazalishaji wa Dawa nchini ili waweze kutengeneza dawa kwa kuzingatia ubora na usalama wa mtumiaji .
“Asilimia 90 ya dawa zinanunuliwa nje ya nchi hivyo lazima tukae na kutengeneza mazingira wezeshi kwa wazalishaji wa ndani ili kuweza kutengeneza dawa hapa nchini na tuweze kuokoa fedha nyingi zinazokwenda nje ya nchi” alisema dkt. Ndugulile.
Kwa upande wake Msajili wa Baraza la wafamasia Bi. Elizabeth Shekirego amewasisitiza wanawake kujiunga na fani hiyo kwani wapo wachache ambapo ni asilimia 30 kuliko wanaume.
Aidha Bi. Shekirego amesema Baraza la wafamasia wamejidhatiti kuleta matokeo chanya kwa kuhakikisha dawa zinazotengenezwa nchini zinaboreshwa kwa mahitaji ya watanzania.
Wiki ya Famasia nchini imeadhimishwa leo jijini Dar es salaam ambapo imebeba kauli mbiu isemayo “TAALUMA YA FAMASI KUELEKEA TANZANIA YA UCHUMI WA VIWANDA” ambapo ulienda na uzinduzi wa bango kitita kitakachotumika kutoa elimu na wajibu wa mfamasia.

0 on: "DKT. NDUGULILE HAIMIZA UTUNZAJI MZURI WA DAWA."