Like us on Facebook

Inaendeshwa na Blogger.

Tafuta katika Blogu Hii

Kumbukumbu la Blogu

Instagram

visitors

display number of visitors

Popular Posts

Pages

Flickr Images

Jumatano, 6 Juni 2018

WILAYA 93 NCHINI ZAFANIKIWA KUTOKOMEZA MATENDE NA MABUSHA.

Katibu Mkuu Wizara ya afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Mpoki Ulisubisya akihutubia mbele ya Wageni na Waandishi wa Habari katika uzinduzi wa mkutano wa kujadili, kupitia na kupanga utekelezaji wa mpango kazi katika kutokomeza magonjwa yaliyokuwa hayapewi kipaumbele jijini Dar es salaam.

Mratibu wa  Mpango wa Taifa wa Magonjwa yasiyopewa Kipaumbele Dk. Upendo Mwingira akisoma taarifa mbele ya mgeni rasmi Katibu Mkuu Wizara ya afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Mpoki Ulisubisya (Hayupo kwenye picha)

Picha ya pamoja ikiongozwa na Katibu Mkuu Wizara ya afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Mpoki Ulisubisya wakati wa uzinduzi wa mkutano wa kujadili, kupitia na kupanga utekelezaji wa mpango kazi katika kutokomeza magonjwa yaliyokuwa hayapewi kipaumbel.


Na WAMJW-DAR ES SALAAM
 
WILAYA 93 nchini yafanikiwa kutokomeza magonjwa yaliyokuwa hayapewi kipaumbele yakiwemo matende na mabusha ambapo wilaya hizo awali zilikua zikihitaji kingatiba lakini kwa sasa hazihitaji kinga hizo.
 
Hayo yamesemwa na Katibu mkuu Wizara ya afya Dkt. Mpoki Ulisubisya katika uzinduzi wa mkutano wa kujadili, kupitia na kupanga utekelezaji wa mpango kazi katika kutokomeza magonjwa yaliyokuwa hayapewi kipaumbele jijini Dar es salaam.
 
“Tumetoa dawa na tunaendelea kwa watanzania wapatao milioni 29 kati ya milioni 50 hivyo kupiga hatua kubwa katika kudhibiti magonjwa yaliyokuwa hayapewi kipaumbele hapa nchini kwetu” alisema Dkt. Ulisubisya.
 
Aidha Dkt. Ulisubisya amesema kuwa mkutano huo uliokutanisha wadau wa afya wa nje na ndani ya nchini unalenga kutoka na mkakati wa kupambana na magonjwa yaliyokuwa hayapewi kipaumbele hasa maeneo ya vijijini.
 
Kwa upande wake Mratibu wa Taifa wa mpango wa kutokomeza magonjwa yaliyokuwa hayapewi kipaumbele nchini Dkt. Upendo Mwingira amesema kuwa wananchi wanatakiwa wajitokeze kwenye mazoezi ya kupata dawa za kuzuia mabusha na matende.
 
“Tunatakiwa kujitokeza kila mwaka mara pindi itakapotangazwa kuwa ni kipindi cha kupata dawa hizo na mwaka huu dawa hizo zitatolewa Septemba kwa watanzania wote” alisema Dkt. Mwingira.
 
Aidha Dkt. Mwingira amesema kuwa mbali na mafanikio yaliyopatikana katika kampeni hiyo ya kutokomeza magonjwa hayo pia kuna changamoto za utoaji elimu na uhamasishaji katika matumizi ya dawa hizo.
 
Hata hivyo amesema kwa upande wa ugonjwa wa Vikope (Trakoma) wamefanikiwa kusitisha  kugawa dawa kwa wilaya 58 kati ya 71 nchini.
 
Mbali na hayo Dkt. Mwingira amesema kuwa katika kuhakikisha magonjwa hayo yanapotea nchini wamejidhatiti kuzindua kampeni ya kuwafanyia upasuaji watu 350  Kisarawe Mkoani Pwani.

MWISHO

0 on: "WILAYA 93 NCHINI ZAFANIKIWA KUTOKOMEZA MATENDE NA MABUSHA."