Like us on Facebook

Inaendeshwa na Blogger.

Tafuta katika Blogu Hii

Kumbukumbu la Blogu

Instagram

visitors

display number of visitors

Popular Posts

Pages

Flickr Images

Ijumaa, 22 Juni 2018

MAGONJWA YASIYO YA KUAMBUKIZA YAONGEZEKA

Waziri wa Afya,Maendeleo ya jamii,Jinsia,Wazee na watoto Mhe. Ummy Mwalimu katikati akikagua vifaa vipya vilivyowekwa kwenye chumba cha upasuaji katika Hospitali ya Benjami Mkapa wakati wa uzinduzi wa Bodi ya udhamini na chumba cha uchujaji damu Hospitalini hapo leo jijini Dodoma.

Waziri wa Afya,Maendeleo ya jamii,Jinsia,Wazee na watoto Mhe. Ummy Mwalimu kushoto akikagua chumba cha kusafishia maji ya wagonjwa wa figo katika Hospitali ya Benjamin Mkapa wakati wa uzinduzi wa Chumba cha uchujaji damu kwa wagonjwa wa figo leo jijini Dodoma, Kulia mwenye koti jeupe ni Daktari Bingwa wa Figo Dkt. Kessy Shija.

Waziri wa Afya,Maendeleo ya jamii,Jinsia,Wazee na watoto Mhe. Ummy Mwalimu kushoto akipata maelezo kutoka kwa Mkurugenzi Mtendaji wa Hospitali ya Benjamin Mkapa kulia Dkt. Alponce Chandika  kuhusu kengere za kuitia wauguzi katika wodi ya wagonjwa wa figo wanaochujwa damu kwenye Hospitali hiyo wakati wa uzinduzi wa Bodi ya udhamini na chumba cha uchujaji damu leo jijini Dodoma.

Waziri wa Afya,Maendeleo ya jamii,Jinsia,Wazee na watoto Mhe. Ummy Mwalimu akikata utepe kuashiria kuzindua rasmi miongozo ya Bodi ya udhamini katika Hospitali ya Benjamin Mkapa iliyozinduliwa leo jijini Dodoma.

Waziri wa Afya,Maendeleo ya jamii,Jinsia,Wazee na watoto Mhe. Ummy Mwalimu akikata utepe kuashiria kuzindua rasmi jengo la kuchuja damu kwa wenye matatizo ya figo katika Hospitali ya Benjamin Mkapa jijini Dodoma leo.


Waziri wa Afya,Maendeleo ya jamii,Jinsia,Wazee na watoto Mhe. Ummy Mwalimu kulia akimkabidhi vitendea kazi Mwenyekiti wa Bodi ya Udhamini ya Hospitali ya  Benjamin Mkapa Dkt. Deodatus Mtasiwa kushoto baada ya kuzinduliwa rasmi kwa bodi hiyo leo jijini Dodoma.

Na WAMJW-Dodoma
Magonjwa yasiyo ya kuambukizwa kama moyo,figo na mengineyo yanaongezeka kwa kasi duniani kote na hapa nchini yamekua yakigharimu Serikali  kiasi cha shilingi Bilioni 36.6 kwa mwaka.
Hayo yamesemwa na Waziri wa Afya,Maendeleo ya Jamii,Jinsia,Wazee na Watoto Mhe.Ummy Mwalimu wakati wa uzinduzi wa bodi ya wadhamini ya Hospitali ya Benjamin Mkapa leo Jijini Dodoma.
Waziri Ummy amesema hapa nchini kwa takwimu za Julai 2013 hadi Juni 2016 magonjwa ya Moyo na Figo ndiyo yalikuwa yakiongoza kwa idadi kubwa ya wagonjwa   kutibiwa nje ya nchi na kugharimu  Serikali kiasi hicho cha fedha.
“Kati ya wagonjwa 560 waliosafirishwa na Serikali  wagonjwa 430 walienda kutibiwa moyo na wagonjwa 160 walienda kupandikizwa figo ”alisema Mhe.Ummy.
Aidha, Waziri Ummy alisema kuwa kwa takwimu za Shirika la Afya Duniani (WHO) magonjwa yasiyoambukiza yanachangia vifo kati ya watu mia moja  watu sitini hufa kwa magonjwa hayo na kati ya wagonjwa 100 watu 47 wanaugua magonjwa yasiyoambukiza
Waziri Ummy aliongeza kuwa kwa kuanzishwa hospitali ya Benjamin Mkapa kutaokoa kiasi kikubwa cha fedha na kuipunguzia Serikali mzigo mkubwa  wa gharama na badala yake fedha hizo zitatumika kuimarisha miundombinu ya hospitali za hapa nchini.
Hata hivyo aliitaka bodi hiyo ya wadhamini kuongeza kasi  ya utekelezaji wa mikakati ya kuboresha huduma za afya ili kuvutia wagonjwa wengi zaidi kutibiwa hospitalini hapo na kupunguza rufaa za wagonjwa wanaopelekwa nje ya nchi kwa matibabu.
“Nawaomba mkachape kazi  bila kuchoka ili hospitali hii ikawe na tija katika kuwahudumia watanzania na hata ndugu zetu wa nchi jirani hasa za  Jumuiya ya Afrika Mashariki katika huduma za matibabu ya Kibingwa”,Alisisitiza Waziri Ummy.
Kwa upande wake Mkurugenzi Mtendaji wa Hospitali hiyo Dkt. Alponce Chandika alisema kuwa lengo la kuanzishwa kwa hospitali hiyo ni kutoa huduma za afya maalum za Kibingwa ikiwemo uchunguzi wa magonjwa ya Moyo,Figo,Macho,Damu, Saratani pamoja na kutoa  huduma za upasuaji kwa kutumia matundu madogo(endoscope).
“Mbali na huduma hizo hospitali yetu inatumika kwa ajili ya kufundisha wataalamu wa kada za afya,kufanya tafiti na huduma za kliniki tembezi” alisema Dkt.Chandika.
Dkt.Chandika alisema kuwa wanatarajia mwezi Agosti kufanya tena upandikizaji  wa figo kwa wagonjwa watatu pia wanatarajia kufanya upasuaji wa matundu madogo kuanzia mwezi Julai mwaka huu
Naye Mwenyekiti wa Bodi hiyo Dkt.Deodatus Mtasiwa alisema kuwa Serikali na wananchi wanatarajia huduma nzuri katika hospitali hiyo hivyo hawanabudi kushirikiana na hospitali mbalimbali zinazotoa huduma za Kibingwa ili kutoa huduma stahili hapa nchini.
Sambamba na uzinduzi wa bodi hiyo yenye wajumbe sita Waziri Ummy  alizindua kitengo cha kuchuja damu katika hospitali ya Benjamin Mkapa.


0 on: "MAGONJWA YASIYO YA KUAMBUKIZA YAONGEZEKA"