Like us on Facebook

Inaendeshwa na Blogger.

Tafuta katika Blogu Hii

Kumbukumbu la Blogu

Instagram

visitors

display number of visitors

Popular Posts

Pages

Flickr Images

Ijumaa, 8 Juni 2018

TAARIFA KWA UMMA



JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA
WIZARA YA AFYA, MAENDELEO YA JAMII, JINSIA, WAZEE NA WATOTO

  
TAARIFA KWA UMMA

 WATUMISHI WA AFYA 200 KUPATIWA MAFUNZO YA UTOAJI WA DAWA ZA USINGIZI (ANAESTHESIA) KWENYE VITUO VYA AFYA VYA UPASUAJI WA DHARURA KWA WAJAWAZITO

Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto kwa kushirikiana na Ofisi ya Rais-TAMISEMI inatekeleza mkakati wa kuhakikisha kwamba huduma za Afya kwa akina mama wajawazito zinakuwa za uhakika na salama kwa kuandaa rasilimali watu, miundombinu ya majengo na vifaa vitakavyowezesha kutoa huduma hizi ikiwemo huduma za upasuaji wa dharura   kwa akina mama wajawazito wakati wa kujifungua.

Mkakati huu una lengo la kupunguza vifo vitokanavyo na uzazi kutoka 556 kwa kila vizazi hai 100,000 hadi kufikia 290 mwaka 2020. Takribani, vituo vya afya (Health Centres) 288 vinavyomilikiwa na Serikali vilivyopo katika Halmashauri za Wilaya, Miji na Manispaa kote nchini vinaboreshwa ili kuviwezesha kutoa huduma za uzazi za dharura kwa akina mama wajawazito.
Uwepo wa Wataalam wa afya ikiwemo wataalam wa utoaji huduma ya dawa za usingizi (Anaesthesia) ni mojawapo ya mahitaji ya lazima katika utoaji wa huduma  hizi.

Ili kutimiza azma ya kupata wataalam wa utoaji wa huduma ya dawa za usingizi wakati wa upasuaji, Wizara kwa kushirikiana na wadau wa maendeleo wa Mfuko wa Pamoja wa Afya (Health Basket Fund) imepata fedha kiasi cha shilingi 1,079,200,000.00 kwa ajili ya kuwasomesha watumishi wa afya wa Serikali (Wauguzi na Matabibu) katika fani ya utoaji huduma ya dawa za usingizi (Anaesthesia). Fedha hizi zitasomesha watumishi wapatao 200, kati ya watumishi hao 100 watafanya mafunzo yao katika hospitali ya Taifa ya Muhimbili na MOI, Watumishi 50 watafanya mafunzo katika Hospitali ya KCMC na 50 watafanya mafunzo hayo katika Hospitali ya Bugando. Mafunzo haya yataanza kutolewa tarehe 15 Juni, 2018. MAJINA WA WATUMISHI WALIOCHAGULIWA KUFANYA MAFUNZO HAYA YANAPATIKANA KWENYE TOVUTI YA WIZARA YA AFYA (www.moh.go.tz) NA YA OFISI YA RAIS-TAMISEMI (www.tamisemi.go.tz)

Lengo la Serikali ni kuhakikisha kuwa ifikapo mwaka 2019 na kabla ya Mwaka 2020 vituo vyote vya afya vinavyomilikiwa na Serikali vinakuwa na watumishi maalum wa kutoa Huduma ya dawa ya Usingizi kwa ajili ya upasuaji wasiopungua wawili (2) kwa kila kituo. Aidha, watumishi wa afya wapatao 85 wamekwishahitimu mafunzo haya katika Hospitali ya KCMC na Bugando na tayari watumishi hao wako kwenye vituo vya afya vilivyokwisha kamilika kuanza kutoa huduma hizo za dharura kwa akina mama wajawazito.

Mafunzo haya ya mwaka mmoja ni ya mpito wakati Serikali ikiendelea kurasimisha mafunzo ya Shahada ya kwanza ya kutoa dawa ya usingizi kwa wauguzi yatakayotolewa na Chuo Kikuu cha Afya na Sayansi Shirikishi Muhimbili (MUHAS) kuanzia mwaka huu wa masomo 2018/19.


Imetolewa na


Nsachris Mwamwaja
MKUU KITENGO CHA MAWASILIANO SERIKALINI-AFYA
08 Juni, 2018

0 on: "TAARIFA KWA UMMA"