Like us on Facebook

Inaendeshwa na Blogger.

Tafuta katika Blogu Hii

Kumbukumbu la Blogu

Instagram

visitors

display number of visitors

Popular Posts

Pages

Flickr Images

Jumatano, 20 Juni 2018

UMMY MWALIMU AWEKA JIWE LA MSINGI KITUO CHA AFYA MUNDEMU

Waziri wa Afya,Maendeleo ya Jamii,Jinsia,Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu kushoto akiweka jiwe la msingi Mradi wa ukarabati na uboreshwaji katika Kituo Cha Afya Mundemu kilichopo Wilaya ya Bahi Mkoani Dodoma leo.kulia ni Mwakilishi wa Mganga Mkuu wa Mkoa Dkt. Mzee na Mbunge wa Bahi Bw. Omari Baduel.



Waziri wa Afya,Maendeleo ya Jamii,Jinsia,Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu kushoto akiweka jiwe la msingi Mradi wa ukarabati na uboreshwaji katika Kituo Cha Afya Mundemu kilichopo Wilaya ya Bahi Mkoani Dodoma leo.kulia ni Mwakilishi wa Mganga Mkuu wa Mkoa Dkt. Mzee na Mbunge wa Bahi Bw. Omari Baduel.


Waziri wa Afya,Maendeleo ya Jamii,Jinsia,Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu akiwasalimia wanakijiji waliojitokeza  wakati wa uwekaji wa jiwe la msingi katika kituo cha Afya Mundemu kilichopo wilayani Bahi mkoa wa Dodoma .

Waziri wa Afya,Maendeleo ya Jamii,Jinsia,Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu akiongea na wanakijiji wa kata ya Mundemu hawapo pichani wakati wa uwekaji jiwe la msingi katika kituo cha Afya Mdemu wilayani Bahi  jijini Dodoma.

Mbunge wa Jimbo la Bahi Bw. Omari Baduel akiongea na wanakijiji wa kata ya Mdemu hawapo pichani wakati wa uwekaji jiwe la msingi katika kituo cha Afya Mundemu wilayani Bahi  jijini Dodoma, kushoto waliokaa ni Waziri wa Afya,Maendeleo ya Jamii,Jinsia,Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu na anayefuata ni Mkuu wa Wilaya ya Bahi Bi. Elizabeth Kitundu 


Baadhi ya wanakijiji waliojitokeza kumsikiliza na kushuhudia uwekaji wa jiwe la msingi katika Kituo cha afya Mundemu uliofanywa na Waziri wa Afya,Maendeleo ya Jamii,Jinsia,Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu hayupo pichani wilayani Bahi  jijini Dodoma.

Mafundi wakiwa katika hatua ya mwisho ya kumalizia jengo la Mochwari lilipo katika Kituo cha Afya Mundemu Wilayani Bahi Mkoa Dodoma .

NA WAMJW-DODOMA

WAZIRI wa Afya,maendeleo ya Jamii,Jinsia,Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu ameweka jiwe la msingi katika Kituo cha Afya Mdemu kilichopo Wilayani Bahi Jijini Dodoma baada ya kuridhishwa na ujenzi huo.
Akizungumza wakati wa kuweka jiwe hilo la msingi Waziri Ummy alisema kuwa Serikali ya awamu ya tano chini ya Rais John Pombe Magufuli imefanya kipaumbele maboresho mbalimbali hususan katika sekta ya afya nchini.
“Nilipofika hapa mwaka 2016 niliona wanawake wajawazito wanalala kwa kubanana na wengine wanafariki kwa uzazi pingamizi hivyo nikaona tuanze kujenga vyumba vya upasuaji wa dharura nchini ikiwemo  wodi ya wanawake wajawazito ili kuokoa Maisha ya mwanamke na mtoto anapojifungua ” alisisitiza Waziri Ummy.
Aidha, Waziri Ummy alisema kuwa mpaka sasa wilaya ya Bahi imefikia asilimia 98 ya wanawake wajawazito kujifungulia katika vituo vya afya amabapo Kitaifa inaonesha katika kila wanawake 100  wanawake  51 ndo hijifungilia kwenye vituo vya afya.
Vilevile Waziri Ummy amesema kuwa Juhudi za Serikali katika kuokoa vifo vya wakina mama wajawazito  Kijijini Mundemu atawapatia gari ya kubebea wagonjwa kwa ajili ya rufaa kutoka kituo kituoni hapo kwenda Hospitali ya Rufaa ya Mkoa.
Kwa upande wake Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Bahi Bi. Benadertha Januari amesema kuwa wamefanikiwa kupunguza vifo vitokanavyo na uzazi kutoka vifo 4 mwaka 2015 mpaka vifo 3 mwaka 2017 na vifo vya watoto chini ya miaka 5 kutoka 50 mwaka 2015 mpaka kufikia vifo 12 2017.
Aidha Bi. Januari amesema kuwa wamefanikiwa kukusanya chupa za damu salama 1640 kati ya chupa 2216 ya malengo waliojiwekea ambayo ni sawa na asilimia 74 kwa kipindi cha mwezi Januari hadi Juni mwaka huu.
Kwa upande wake Kaimu Mtendaji Kata ya Mundemu Bw. Reuben Ntiruka amesema kuwa Kituo cha afya Cha Mundemu kinapokea rufaa ya kutoka Zahanati 21 za vijiji vitatu ambayo idadi ya walengwa wake ni wananchi 9103.
Mbali na hayo Bw. Ntiruka ameiomba Serikali kuijengea Kituo hicho Uzio ,nyumba za watumishi, kuongeza idadi ya watumishi  pamoja gari ya kubebea wagonjwa kwani ndio changamoto kubwa zinazoikumba Kituo hicho cha afya.

0 on: "UMMY MWALIMU AWEKA JIWE LA MSINGI KITUO CHA AFYA MUNDEMU"