Like us on Facebook

Inaendeshwa na Blogger.

Tafuta katika Blogu Hii

Kumbukumbu la Blogu

Instagram

visitors

display number of visitors

Popular Posts

Pages

Flickr Images

Jumatano, 20 Juni 2018

PICHA ZA MATUKIO MBALI MBALI WAKATI WA UZINDUZI WA KAMPENI YA FURAHA YANGU-DODOMA

Waziri wa afya,Maendeleo ya Jamii,Jinsia,Wazee na watoto Mhe. Ummy Mwalimu akiongea na hadhira ya watu (hawapo kwenye picha) waliojitokeza katika kampeni ya Furaha yangu iliyofanyika katika viwanja vya Jamhuri jijini Dodoma, Kampeni hiyo ilizinduliwa na Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Kasim Majaliwa.

Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa (wa tatu kulia) akiwa ameambatana na viongozi wengine wakikagua mabanda ya watoa huduma za afya wakati wa uzinduzi wa Kampeni ya Kitaifa ya Kupima VVU na kuanza kutumia dawa mapema inayojulikana kama Furaha Yangu iliyofanyika katika uwanja wa Jamhuri, jijini Dodoma leo.


Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa (wa pili kushoto) akiwa ameambatana na Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge, Kazi, Ajira, Vijana na Watu wenye Ulemavu) Mhe Jenista Mhagama (wa pili kushoto) wakipokea maelezo kutoka kwa mtaaalam wa Afya wakati wa uzinduzi wa Kampeni ya Kitaifa ya Kupima VVU na kuanza kutumia dawa mapema inayojulikana kama Furaha Yangu iliyofanyika katika uwanja wa Jamhuri, jijini Dodoma leo. 
 
Wakazi mbalimbali wa maeneo ya Dodoma wakiingia katika baadhi ya mabanda kupata huduma za kupima VVU pamoja na kupata ushauri nasaha katika viwanja vya Jamhuri kwenye uzinduzi wa kampeni ya Furaha yangu leo Mjini Dodoma.

Kundi la wanafunzi waliojitokeza kupata  huduma  za kupima VVU pamoja na ushauri nasaha katika viwanja vya Jamhuri kwenye uzinduzi wa kampeni ya Furaha yangu leo Mjini Dodoma.

Wakazi mbalimbali wa maeneo ya Dodoma waliojitokeza kwenye viwanja vya Jamhuri kushuhudia uzinduzi na  kupata  huduma  za kupima VVU pamoja na ushauri nasaha katika viwanja vya Jamhuri kwenye uzinduzi wa kampeni ya Furaha yangu leo Mjini Dodoma.

Waziri wa afya,Maendeleo ya Jamii,Jinsia,Wazee na watoto Mhe. Ummy Mwalimu kushoto akijadili jambo pamoja na Waziri wa TAMISEMI Mhe. Suleiman Jaffo  katika viwanja vya Jamhuri kwenye uzinduzi wa kampeni ya Furaha yangu leo Mjini Dodoma.
 
Picha ya pamoja ikiongozwa na Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Kasim Majaliwa wakati akikata utepe ikiwa ni ishara ya ufunguzi rasmi wa kampeni ya Furaha yangu aliyoifungua katika viwanja vya Jamhuri jijini Dodoma.


0 on: "PICHA ZA MATUKIO MBALI MBALI WAKATI WA UZINDUZI WA KAMPENI YA FURAHA YANGU-DODOMA"