Like us on Facebook

Inaendeshwa na Blogger.

Tafuta katika Blogu Hii

Kumbukumbu la Blogu

Instagram

visitors

display number of visitors

Popular Posts

Pages

Flickr Images

Jumatano, 13 Juni 2018

WAZIRI MKUU KASSIM MAJALIWA KUZINDUA KAMPENI YA FURAHA YANGU JUNI 19 DODOMA

Kaimu Mkurugenzi wa Huduma za Kinga Wizara ya Afya Dkt. Angera Ramadhan akihutubia mbele ya Wadau wa masuala mbali mbali ya VVU, ikiwa ni kuelekea katika uzinduzi wa kampeni ya kitaifa ya Furaha yangu,mkoani Dodoma Juni 19 mwaka huu,inayohusisha upimaji wa VVU na kuanza kutumia ARV

Wadau mbali mbali wa wa masuala mbali mbali ya VVU wakifuatilia kwa makini hotuba ya mgeni rasmi ambae ni Kaimu Mkurugenzi wa Huduma za Kinga Wizara ya Afya Dkt. Angera Ramadhan ikiwa ni kuelekea katika uzinduzi wa kampeni ya kitaifa ya Furaha yangu,mkoani Dodoma Juni 19 mwaka huu,inayohusisha upimaji wa VVU na kuanza kutumia ARV.


NA WAMJW-DAR ES SALAAM 

WAZIRI Mkuu Kassim Majaliwa,anatarajiwa kuzindua kampeni ya kitaifa ya Furaha yangu,mkoani Dodoma Juni 19 mwaka huu,inayohusisha upimaji wa VVU na kuanza kutumia ARV

Hayo yamezungumzwa na Kaimu Mkurugenzi wa Huduma za Kinga Wizara ya Afya Dkt. Angera Ramadhan,
Kampeni hiyo imetajwa kuhamasisha mkakati wa serikali wa upimaji wa VVU na kuanza kutumia ARV mapema kwa wale watakaokutwa na maambukizi.


"Asilimia 45 ya wanaume wanajijua kuwa wanaishi na maambukizi ya VVU na asilimia 55 hawajijui huku wanawake waliokuwa wanajijua kuwa wanamaambukizi  ni asilimia 56 na 44 bado hawako tayari" alisema Dkt. Angera

Dkt. Angera amesema kuwa Kuanza ARV mapema kutapunguza wingi wa  VVU  mwilini na kuimarisha kinga kwa wagonjwa,hivyo kampeni hii kwa wanaume itakuwa chachu ya kujua afya zao na wengi kuwa tayari kwa kuimarisha afya na kupunguza hatari ya kuambukiza wenza wao. 

Aidha Dkt. Angera amesema kuwa serikali itaendelea kubuni mbinu mbadala ili kufikia malengo ya dira ya taifa ya kutokomeza maambukizi ya Ukimwi iliyoridhia malengo ya UNAIDS ya 90-90-90 ambayo ni kuhakikisha asilimia 90 ya watu wote wanaoishi na VVU  wanatambua afya zao,wanaanza dawa na kupunguza maambukizi mapya.

Naye Mkurugenzi wa Tume ya Kudhibiti UKIMWI TACAIDS, Dkt. Leornad Maboko,alisema uzinduzi wa kampeni hiyo utakuwa na siku tano za kutoa huduma za afya bila malipo,ikiwemo upimaji wa VVU  na magonjwa sugu.

Aidha Dkt.  Maboko alisema kuwa  lengo la kuhamasisha kwa kauli ya Furaha yangu  Pima,Jitambur ,Ishi na mwanaume njoo kwenye huduma ni kutokana na kubaini kundi hilo kubwa halifikiwi na ili kumaliza maambukizi ni lazima kupewa hamasa.

"Hivyo tunatoa wito wakazi wa Dodoma,mikoa ya jirani na mikoa sita ambayo ipo katika awamu ya kwanza ya uzinduzi ikiwemo Njombe,Iringa na Mwanza kumuunga mkono Waziri Mkuu kwa kujitokeza kwa wingi kujua afya zao na ikigundulika kutumia dawa mapema ili kuiamrisha afya na kupunguza nguvu ya VVU," alisema Dkt.  Maboko. 

0 on: "WAZIRI MKUU KASSIM MAJALIWA KUZINDUA KAMPENI YA FURAHA YANGU JUNI 19 DODOMA"