Like us on Facebook

Inaendeshwa na Blogger.

Tafuta katika Blogu Hii

Kumbukumbu la Blogu

Instagram

visitors

display number of visitors

Popular Posts

Pages

Flickr Images

Ijumaa, 15 Juni 2018

TAARIFA KWA UMMA


JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA
WIZARA YA AFYA, MAENDELEO YA JAMII, JINSIA, 
WAZEE NA WATOTO

TAHADHARI KWA UMMA KUHUSU UGONJWA WA HOMA YA BONDE LA UFA (RVF) HAPA NCHINI, ILIYOTOLEWA NA MHE. UMMY MWALIMU (MB); WAZIRI WA AFYA, MAENDELEO YA JAMII, JINSIA, WAZEE NA WATOTO, TAREHE 14 JUNI 2018 

Ndugu Wanahabari,
Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia Wazee na Watoto, inatoa tahadhari ya ugonjwa wa Homa ya Bonde la Ufa (Rift Valley Fever) kufuatia uwepo wa taarifa juu ya ugonjwa huo nchini Kenya. Mpaka sasa jumla ya wagonjwa 19 na vifo 6 (CFR 31.6%) vilivyosababishwa na ugonjwa huu vimeripotiwa na Wizara ya Afya nchini Kenya. Ugonjwa ulianzia katika Kaunti ya Wajir, Kaskazini mwa Kenya na hadi sasa ugonjwa huu umeripotiwa kuenea kwenye Kaunti za Marsabit na Tana River. 

Homa ya Bonde la Ufa ni ugonjwa unaosababishwa na virusi vinavyoitwa Phlebovirus unaoathiri wanyama na binadamu ambapo wanyama wanaoathirika zaidi ni pamoja na Ng’ombe, Kondoo, Mbuzi na Ngamia. Virusi vya ugonjwa wa homa ya bonde la ufa husambazwa kwa mnyama baada ya kuumwa na mbu aliyeambukizwa ugonjwa huu. Mbu aenezae ugonjwa huu ni wa aina ya Aedes ambao ni weusi na wana madoadoa meupe ya kung’aa.

Kwa binadamu ugonjwa huu huambukizwa kwa  kuumwa na mbu aina ya Aedes aliyeambukizwa na virusi hivi au kugusa damu,majimaji au mzoga wa  mnyamaaliyeathirika na ugonjwa huu. Binadamu anaweza kugusa damu au maji maji ya mnyama kwa njia ya Kuchinja, kula nyama, kuchuna ngozi au kunywa maziwa yasiochemshwa kutoka kwa mnyama aliyeambukizwa.

Ndugu Wanahabari,
Dalili za ugonjwa huu kwa wanyama ni pamoja na kuharibu mimba; kuwa na homa kali na kuzubaa; vifo vya ndama, watoto wa mbuzi na watoto wa kondoo; kuharisha na kutapika na wakati mwingine matapishi au kinyesi huchanganyika na damu. 

Kwa binadamu dalili za ugonjwa huu huanza kuonekana kati ya siku 2 hadi 5 baada ya maambukizi. Dalili za awali ni; homa kali, kuumwa na kichwa, maumivu ya mwili, kichefuchefu au kutapika, kizunguzungu na kupungua uzito. Aidha, kama mgonjwa hatapata matibabu ya haraka, mgonjwa anaweza kupata dalili za  kutokwa damu mdomoni, puani, masikioni na  kwenye ngozi.Vilevile mgonjwa anaweza kupata dalili za kutapika au  kuharisha damu, uvimbe wa ubongo au uvimbe kwenye macho na hatimaye kupoteza maisha. Endapo mgonjwa akiwahi kutibiwa,  wengi hupona wiki moja baada ya kuonyesha dalili za awali.  Watu wote wanaweza kuambukizwa ugonjwa huu lakini  watu ambao wako katika hatari zaidi ya kupata ugonjwa ni wanaojishughulisha na kuchinja wanyama, wachungaji wa mifugo pamoja na;  madaktari wa wanyama. .

Ndugu Wanahabari, 
Wizara inaendelea kusisitiza jukumu la kila mmoja wetu kuhakikisha kuwa anajilinda dhidi ya kupata maambukizi ya ugonjwa huu wa Homa ya Bonde la Ufa. Aidha Wizara inawasihi wananchi kushirikiana  na Halmashauri pamoja na Mikoa yote ya Tanzania katika juhudi za kupambana na kuzuia ugonjwa huu ili usiingie  kwenye maeneo yao kwa kufanya  yafuatayo; 
Kutokugusa damu, majimaji kutoka mwilini au mzoga wa mnyamaanayehisiwa  kuwa na ugonjwa huu.
Kutochinja mnyama ambaye anahisiwa kuwa na ugonjwa huu. 
Kutokunywa maziwa na kula nyama ya mnyama ambaye anahisiwa kuwa na ugonjwa huu.
Kutokulala na wanyama kwenye nyumba moja, wanyama watengwe sehemu mbali na makazi ya watu.
Ikiwa mtu yeyote yule atalazimika kushika mizoga pengine kutokana na taaluma au kazi yake, anatakiwa avae vifaa kinga kama vile glovu (gloves), mabuti na mask.
Kunawa mikono kwa sabuni na maji safi.
Wahudumu wa afya na wafanyakazi wa machinjioni wanashauriwa kuchuku hatua za tahadhari dhidi ya maambukizi kwa kuvaa vifaakinga. 
Jamii hasa za wafugaji au zinazojishughulisha na shughuli za mifugo na uchinjaji wa mifugo watoe taarifa mapema kwa mamlaka husika pale waonapo dalili za ugonjwa huu katika mifugo yao.
Kuzuia mazalia ya mbu  kwa kufunika maji yaliyotuama, kufukia  madimbwi,  kufyeka vichaka na kuondoa takataka zinazosabisha maji kutuama ikiwemo vifuu vya nazi, makopo na matari ya gari.
Kuchukua hatua za kujilinda  kuumwa na mbu kwa kutumia chandarua, kuvaa nguo ndefu na kutumia dawa za kujipaka ili kuzuia kuumwa na mbu.   

Ndugu Wanahabari,
Wizara yangu imechukua hatua zifuatazo kufuatia tishio la mlipuko wa ugonjwa huu wa Homa ya Bonde la Ufa nchini;  

Kutoa taarifa ya tahadhari ya ugonjwa kwa Waganga Wakuu wote wa Mikoa na Wilaya kwa Tanzania Bara kupitia Makatibu Tawala na Wakurugenzi wa Halmashauri. 
Kuimarisha ufuatiliaji wa magonjwa nchini kwa kutumia mfumo wa Integrated Diseases Surveillance and Response IDSR ambapo tunaendelea kupata taarifa za kila siku juu ya mwenendo wa ugonjwa huu na mkazo umewekwa zaidi katika maeneo ya mipakani.
Wizara ipo katika hatua za mwisho kuanzisha mfumo wa ufuatiliaji wa ugonjwa wa RVF kwa kuanzisha vituo maalum ‘Sentinel Surveillance Sites’ katika Mikoa ya Arusha, Manyara, Tanga na Kilimanjaro 
Kufanya mkutano wa pamoja wa kisekta (Afya ya binadamu na  wanyama) kuhusu ufuatiliaji na udhibiti wa magonjwa "Cross border Surveillance” kwa Mikoa ya Arusha, Manyara, Dodoma na Kilimanjaro
Kuimarisha Utambuzi wa ugonjwa katika maabara  ambapo sasa, tuna uwezo wa kupima na kuthibitisha ugonjwa huu hapa nchini 

 Hitimisho
Wizara inaendelea kufuatilia kwa karibu mwenendo wa ugonjwa huu wa Homa ya Bonde la Ufa nchini Kenya. Aidha, wananchi wanashauriwa kutokuwa na hofu kwani hadi sasa hakuna mgonjwa aliyegundulika kuugua ugonjwa huu hapa nchini. Juhudi zinaendelea kuchukuliwa kuimarisha mawasiliano ya sekta husika ili kubaini kwa haraka ugonjwa huu pale utakapotokea. 

Wizara yangu inashauri wananchi kuwahi kwenda katika kituo cha kutolea huduma za afya mara moja pale waonapo dalili za awali za ugonjwa huu. Aidha, Wizara inaendelea kushirikiana na wadau wa sekta na mashirika mbalimbali kufuatilia na kujiandaa kudhibiti mlipuko wa ugonjwa huu endapo utatokea.

1 on: "TAARIFA KWA UMMA "
  1. All the provisions of this chapter shall be liberally construed for the accomplishment of these purposes. When quantity of} claims are filed within the trigger the trigger shall be tried upon the issues made thereby with the petition for forfeiture with any affirmative defenses being deemed denied with out additional pleading. Trial of all such causes shall be utilizing a|with no} jury, except in such circumstances as a trial by jury additionally be} assured by the State Constitution and in such 메리트카지노 circumstances trial by jury shall be deemed waived until demanded within the declare filed. Seats most likely not|will not be} held or reserved by a corporation or person concerned within the conduct of any bingo recreation for players not current, nor may any cards be put aside, held, or reserved from one session to another for any participant. Numbers on the profitable cards or sheets shall be introduced and verified within the presence of another participant.

    JibuFuta