Like us on Facebook

Inaendeshwa na Blogger.

Tafuta katika Blogu Hii

Kumbukumbu la Blogu

Instagram

visitors

display number of visitors

Popular Posts

Pages

Flickr Images

Jumatatu, 11 Juni 2018

MAKAMU WA RAIS AHAIDI MILIONI 600 KUPAMBANA NA CHANGAMOTO ZA DAWA MLOGANZILA.

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe.Samia Suluhu Hassan akizungumza na wafanyakazi wa hospitali ya Taaluma na Tiba ya Chuo Kikuu cha Afya na Sayansi shirikishi Muhimbili (MAMC), Kampasi ya Mloganzila wakati wa ziara yake iliyofanyika leo.

Waziri wa Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu akizungumza kutolea machache ufafanuzi.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan  (mwenye kilemba cha bluu) akipata maelezo kutoka kwa Waziri wa Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu (kulia) wakati wa ziara yake katika hospitali ya Taaluma na Tiba ya Chuo Kikuu cha Afya na Sayansi Shirikishi Muhimbili (MAMC), Kampasi ya Mloganzila jijini Dar es Salaam. Pembeni kushoto ni Naibu Makamu Mkuu wa Chuo, Huduma za Hospitali, Prof. Said Aboud.

NA WAMJW-MLOGANZILA

MAKAMU wa Rais wa Jamhuri ya muungano wa Tanzania Bi. Samia Suluhu Hassan amehaidi  kuiongezea fedha za dawa hospitali Mloganzila Sh. milioni 600 mpaka kufikia Sh. milioni 900 ili kukabiliana na changamoto ya upungufu wa dawa hospitalini hapo.

Hayo ameyasema wakati alipofanya ziara yake ya kuangalia hali ya utoaji huduma katika Hospitali ya Mloganzila iliyopo nje kidogo ya jiji la Dar es salaam leo alipoambatana na Waziri wa Afya,Maendeleo ya jamii,Jinsia ,Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu.

“Tatizo hata fedha mliyopewa awali mkichukua dawa MSD hamrudishi tena fedha kule, hakikisheni hizi fedha tunazowaongeza mlipe bili MSD ili iweze kuleta dawa nyingi zaidi angalau nusu ya fedha muirejeshe tena huko,” alisema.Mhe. Samia.

Aidha Mhe. Samia ameiagiza pia hospitali hiyo kufungua duka la dawa ili kuweza kuweka aina ya dawa ambazo wamekuwa wakizikosa Bohari ya Dawa.

Mbali na hayo Mhe.  Samia alikagua na kushangazwa na Wakala wa Ujenzi Tanzania (TBA kwa kitendo cha kusuasua ujenzi wa mabweni katika Hospitali ya Taaluma na Tiba Mloganzila.

Kwa upande wake  Waziri wa Afya,Maendeleo ya Jamii,Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu  aliwataka  wananchi kuchangia huduma za matibabu kupitia bima za afya ili waweze kupata matibabu ya kibingwa ngazi za juu bila vikwazo vya kifedha 


“ Mloganzila ni miongoni mwa Hospitali saba  zinazomilikiwa na serikali zinazotoa matibabu ya kibingwa ngazi ya juu na uwepo wake umeleta unafuu katika kuongeza wigo wa huduma na mafunzo kwa wataalamu wa afya” alisema Mhe. Ummy.
Naye, Naibu Makamu Mkuu wa Chuo huduma za hospitali, Profesa Said Abood, alisema wamekuwa wakipata asilimia 24 pekee ya dawa wanazozihitaji kutoka MSD na dawa zingine wamekuwa wakizinunua kupitia wakala mbalimbali.

0 on: "MAKAMU WA RAIS AHAIDI MILIONI 600 KUPAMBANA NA CHANGAMOTO ZA DAWA MLOGANZILA."