Like us on Facebook

Inaendeshwa na Blogger.

Tafuta katika Blogu Hii

Kumbukumbu la Blogu

Instagram

visitors

display number of visitors

Popular Posts

Pages

Flickr Images

Jumanne, 26 Juni 2018

WAZIRI UMMY ATEMBELEA TAASISI YA SARATANI YA OCEAN ROAD NA KUWATAKA WAKAMILISHE HARAKA UFUNGAJI WA MASHINE MPYA ZA MIONZI ILI KUHAKIKISHA HUDUMA BORA ZAIDI KWA WAGONJWA WA SARATANI NCHINI

 Mkurugenzi wa taasisi ya Saratani ya Ocean Road Dkt Julius Mwaiselage akitoa maelezo kwa Waziri wa Afya Mhe. Ummy Mwalimu juu ya ufanisi wa mashine mpya na yakisasa ya mionzi iliyopo katika taasisi hiyo.

Mtaalamu wa masuala ya mionzi kutoka Taasisi ya Saratani Ocean Road Dkt. Hemed Myanza akitoa majibu ya moja ya swali lililoulizwa na Waziri wa Afya Mhe.Ummy Mwalimu pindi alipofanya ziara katika taasisi hiyo.

Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu akimsililiza ndugu wa moja kati ya wagonjwa waliofika Hospitalini hapo kupata huduma za matibabu ya Saratani.

Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu akisikiliza malalamiko ya mama aliekuwa akisubiri matibabu ya ugonjwa wa kansa katika taasisi hiyo ya Ocean Road. Wa katikati ni Mkurugenzi wa taasisi hiyo Dkt. Julius Mwaiselage.

Mashine ya Kisasa ya Linear Accelerator iliyounganishwa na CT simulator zote mbili zikiwa na gharama ya shilingi Bilion9.5 iliyojumuishwa  na mafunzo ya Wataalamu na matengenezo kinga ya miaka miwili.


WAZIRI UMMY ATEMBELEA TAASISI YA SARATANI YA OCEAN ROAD NA KUWATAKA WAKAMILISHE HARAKA UFUNGAJI WA MASHINE MPYA ZA MIONZI ILI KUHAKIKISHA HUDUMA BORA ZAIDI KWA WAGONJWA WA SARATANI NCHINI

Na WAMJW-Dar Es Salaam.

Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Mhe.Ummy Mwalimu (Mb), amefanya ziara ya kikazi katika Taasisi ya Saratani ya Ocean Road ili kukagua utoaji wa huduma za Matibabu katika Hospitali hiyo. 

Katika ziara hiyo, Mhe. Waziri alifahamishwa kwamba mashine zote za tiba ya mionzi ya nje inafanya kazi vizuri na huduma zinaendelea kutolewa kwa wagonjwa.

Pia wakati wa ziara hiyo, Mhe.Ummy alitumia fursa hiyo kuzungumza na wagonjwa mbalimbali waliokuwa wakipata huduma za tiba ya mionzi  hospitalini hapo, huku baadhi ya wagonjwa walitoa malalamiko kwa Waziri kuwa, wamekuwa wakitumia muda mrefu kusubiri kupata huduma hususani  huduma za mionzi ya nje. 

Kufuatia hali hiyo, mhe. Ummy alitoa maelekezo kwa uongozi wa Hospitali kuhakikisha wanaweka utaratibu mzuri ambao utapunguza muda kwa wagonjwa kusubiri huduma za mionzi ikiwemo kuwepo na ratiba ambayo kila mgonjwa atajua anafika saa ngapi kupata tiba hiyo.

Vile vile, mhe. Ummy alitembelea  kitengo cha utoaji wa huduma za mionzi ya ndani ambapo alijionea changamoto ya kutokufanya kazi kwa mashine hizo za utoaji wa mionzi ya ndani kutokana na kukosekana kwa vifaa vya 'transfer tubes' na 'gyn applicators'.

Kufuatia hali hiyo mhe.Ummy alitoa maelekezo kwa Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Ocean Road, Dkt.Julius Mwaiselage kuhakikisha kuwa mashine hizo zinafanya ndani ya siku 2 kwa kuazima hivyo vifaa hivyo kutoka Hospitali ya Bugando ili kurudisha huduma hizo kwa wagonjwa ambao wengi ni wanawake wenye tatizo la Saratani ya Mlango wa Kizazi.
 "Naelekeza kuwa fanyeni utaratibu wa kupata kifaa kilichoharibika mapema iwezekanavyo" alisema mhe.Ummy.

Naye Mkurugenzi wa Taasisi ya Saratani ya Ocean Road , Dkt.Julius Mwaiselage alimhakikishia mhe.Waziri kuwa atajitahidi ili vifaa vilivyoharibika vinapatikana ndani ya siku mbili kutoka Hospitali Bugando na pia wameagiza vifaa hvyo kutoka kiwandani nje ya nchi kwa gharama ya Euro 43,200.00

0 on: "WAZIRI UMMY ATEMBELEA TAASISI YA SARATANI YA OCEAN ROAD NA KUWATAKA WAKAMILISHE HARAKA UFUNGAJI WA MASHINE MPYA ZA MIONZI ILI KUHAKIKISHA HUDUMA BORA ZAIDI KWA WAGONJWA WA SARATANI NCHINI"