Like us on Facebook

Inaendeshwa na Blogger.

Tafuta katika Blogu Hii

Kumbukumbu la Blogu

Instagram

visitors

display number of visitors

Popular Posts

Pages

Flickr Images

Jumatano, 20 Februari 2019

DKT. NDUGULILE APOKEA UGENI KUTOKA IRELAND





Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Faustine Ndugulile akielezea jambo katika kikao na ugeni kutoka Ireland (haupo katika picha), uliofika kujadili namna gani Serikali hizo mbili zinaweza kushirikiana katika kuleta maendeleo nchini hususani katika Sekta ya Afya.

Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Faustine Ndugulile akiwa katika kikao na ugeni kutoka Ireland ulioongozwa na Balozi wa Ireland nchini Tanzania Mhe. Paul Sherlock (Wakwanza Kushoto), uliofika kujadili namna gani Serikali hizo mbili zinaweza kushirikiana katika kuleta maendeleo nchini hususani katika Sekta ya Afya.


Na WAMJW - DSM


Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Faustine Ndugulile amekutana na Balozi wa Ireland nchini Tanzania Mhe. Paul Sherlock ambaye pia aliongozana na wajumbe wengine kutoka Ireland.

Katika Mkutano huo masuala mbalimbali yameongelewa ikiwemo masuala ya ushirikiano baina ya nchi ya Tanzania na Ireland katika shughuli za Maendeleo hususan katika Sekta ya Afya katika masuala ya Lishe, Hifadhi ya Jamii na masuala ya uongozi bora.

Dkt. Ndugulile ameishukuru Serikali ya Ireland kwa kuisaidia Serikali ya Tanzania katika shughuli za Maendeleo hususan katika Sekta ya Afya kupitia Mashirika yasiyo ya kiserikali (NGO's).

Dkt. Ndugulile aliendelea kusema kuwa Serikali ya Ireland na Serikali ya Tanzania zimeingia makubaliano ya  kuleta Wataalamu wa Afya ili kuwajengea uwezo Wataalamu wa Tanzania

"Tangu 2007 Ireland ina mahusiano ya muda mrefu na Tanzania kupitia Hospitali ya CCBRT, huku Wataalamu wake  wakitoa huduma za upasuaji wa Fistula na upasuaji wa mifupa" alisema Dkt. Ndugulile

Mbali na hayo Dkt. Ndugulile aliweka wazi vipaumbele vya Serikali ili kuimarisha Sekta ya Afya, ikiwemo masuala ya Afya ya uzazi,Mama na Mtoto, Afya ya vijana balehe, kuboresha miundombinu, matumizi ya mifumo ya takwimu na huduma za dharura.

Mwisho ameishukuru Serikali ya Ireland kwa msaada wanaoipatia Tanzania na ameahidi kuwa Serikali ya Tanzania itaendelea kushirikiana na Serikali ya Ireland katika kuimarisha Maendeleo hususan katika Sekta ya Afya.

#TunaboreshaAfya

0 on: "DKT. NDUGULILE APOKEA UGENI KUTOKA IRELAND"