Like us on Facebook

Inaendeshwa na Blogger.

Tafuta katika Blogu Hii

Kumbukumbu la Blogu

Instagram

visitors

display number of visitors

Popular Posts

Pages

Flickr Images

Jumatatu, 4 Februari 2019

CHANJO YA MLANGO WA KIZAZI HAIHUSIANI NA UZAZI WA MPANGO

Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe.Ummy Mwalimu akisisitiza jambo leo wakati akiongea na Waandishi wa Habari katika siku ya Saratani Duniani, iliyofanyika katika Ukumbi wa Idara ya Habari Bunge jijini Dodoma.

Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe.Ummy Mwalimu akiteta jambo na Mkurugenzi wa Ubora kutoka Wizara ya Afya Dkt. Mohammed Mohammed ambaye alimwakilisha Katibu Mkuu Wizara ya Afya.

Mkurugenzi wa Ubora ambaye alimwakilisha Katibu Mkuu Wizara ya Afya Dkt. Mohammed Mohammed akiteta jambo na Kaimu Mkurugenzi wa Tiba Wizara ya Afya Dkt. Grace Maghembe leo katika  tamko la siku ya Saratani Duniani lililofanyika katika ukumbi wa Idara ya Habari Bunge jijini Dodoma.

Waandishi wa Habari wakimsikiliza kwa makini Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe.Ummy Mwalimu  wakati akitoa tamko la siku ya Saratani Duniani, leo jijini Dodoma


 Waandishi wa Habari wakifuatilia tamko la Saratani lililosomwa na Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu leo katika Ukumbi wa Idara ya habari Bungeni jijini Dodoma.

CHANJO YA MLANGO WA KIZAZI HAIHUSIANI NA UZAZI WA MPANGO.

Na WAMJW - DOM

WAZIRI wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe.Ummy Mwalimu amewatoa hofu Wananchi kwa kusisitiza kuwa chanjo ya kuwakinga wasichana na Saratani ya Mlango wa kizazi haihusiani na uzazi wa mpango wala kumzuia msichana kuja kupata uja uzito baadae.

Ameyasema hayo leo wakati akiongea na Waandishi wa Habari katika siku ya Saratani Duniani, iliyofanyika katika Ukumbi wa Idara ya Habari Bunge jijini Dodoma, huku kauli mbiu ya mwaka huu ikiwa ni "NITAFANYA JITIHADA ZOTE KUPUNGUZA JANGA LA SARATANI DUNIANI".

Waziri Ummy amesema kuwa Chanjo ya Mlango wa kizazi ni salama na imethibitishwa na Shirima la Afya Duniani kwaajili yakuwakinga Wasichana dhidi ya maambulizi ya Saratani ya Mlango wa kizazi.

" Chanjo ya kuwakinga wasichana na saratani ya mlango wa kizazi haihusiani na uzazi wa mpango, ni chanjo ambayo imethibitishwa na Shirika la Afya Duniani kwaajili yakuwakinga wasichana dhidi ya maambukizi ya Saratani ya mlango wa Kizazi" Alisema Waziri Ummy

Waziri Ummy amesema kuwa katika kila wagonjwa wa Saratani 100, takribani wagonjwa 31 ni wanawake wa Saratani ya Mlango wa kizazi, hivyo amewahasa wazazi na walezi nchini kuhakikisha wasichana wanaostahili kupata chanjo hii, wanaipata bila vikwazo vyovyote ili kutokomeza kabisa Saratani hii nchini.

"Katika kila wagonjwa wa Saratani 100, Wagonjwa takribani 31 ni wanawake wa Saratani hii ya Mlango wa kizazi, kwahiyo hatuna haja ya kuiogopa chanjo hii kwasababu ndio itayowakinga watoto wetu na maambukizi ya Saratani ya mlango wa kizazi" alisema Waziri Ummy.

Aidha, Waziri Ummy amesema kuwa  kwa mujibu wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Tafiti za Saratani (IARC), zinaonyesha kwamba kwa Tanzania kunatokea mgonjwa 1 wa Saratani kwa kila watu 1000, hivyo Tanzania inakua na wagonjwa wapya wa Saratani 55,000 kwa mwaka na takribani wagonjwa 28,610 hufariki kwa mwaka, ambapo ni vifo asilimia 52 ya wagonjwa wapya. 

Aliendelea kusema kuwa Taarifa kutoka Taasisi ya Saratani ya Ocean Road zinaonesha kwamba kumekuwa na ongezeko la wagonjwa wa Saratani mwaka hadi mwaka, huku akisema kuwa Mwaka 2015  wagonjwa wapya 5,764, huku mwaka 2016  wagonjwa wapya 6,338, na mwaka 2017  wagonjwa wapya 7,091, pia mwaka 2018 wagonjwa wapya 7,649.

Kwa upande mwingine Waziri Ummy amedai kuwa Serikali imeanzisha huduma kwenye vituo 624 vilivyopo katika Halmashauri mbalimbali nchini ambapo jumla ya wanawake 375,522 walifanyiwa uchunguzi wa saratani ya mlango wa kizazi na saratani ya matiti mnamo mwaka 2017, ukilinganisha na wanawake 416,841 waliofanyiwa uchunguzi huo mwaka 2018. Kati ya hao, wanawake 16,147 waligundulika kuwa na mabadiliko ya awali mwaka 2017, na wanawake 18,341 mwaka 2018.

0 on: "CHANJO YA MLANGO WA KIZAZI HAIHUSIANI NA UZAZI WA MPANGO"