Like us on Facebook

Inaendeshwa na Blogger.

Tafuta katika Blogu Hii

Kumbukumbu la Blogu

Instagram

visitors

display number of visitors

Popular Posts

Pages

Flickr Images

Jumatatu, 4 Februari 2019

WAUGUZI WATAKIWA KUZINGATIA MAADILI KATIKA SEHEMU ZAO ZA KAZI


Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu akiwa ameshika bango kuashiria uzinduzi wa Kampeni ya Kimataifa ya Uuguzi Sasa Kampeni inayolenga kuinua hadhi na muonekano wa kada ya uuguzi nchini.

Wadau wa Kampeni ya Uuguzi Sasa wakiwa wameinua mabango kuashiria kampeni hiyo kuzinduliwa rasmi.

Wauguzi wakisikiliza kwa umakini yanayoendela kwenye uzinduzi wa Kampeni ya Uuguzi Sasa

Picha ya wadau wa kampeni ya uuguzi sasa waliojitokeza kwenue uzinduzi wa kampeni hiyo inayokenga kuinua hadhi na muonekano wa kada ya uuguzi nchini.

Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu (kushoto) akimpongeza Mwalimu Mstaafu wa Kada ya Uuguzi  Mwl. justina Venant (kulia) kwa kumpatia cheti cha utumishi ulitukuka wakati wa uzinduzi wa Kampeni ya Uuguzi Sasa.

Picha ya pamoja ya Viongozi na Watendaji wa Serikali pamoja na wadau wa Sekta ya Afya wakati wa uzinduzi wa kampeni ya Uuguzi Sasa.


Na WAMJW - Dodoma.

Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu amewataka wauguzi kutimiza wajibu wao na kutoa huduma bora wakati wa kazi kulingana na miongozo na maadili ya kazi ya uuguzi na ukunga.

Waziri Ummy ametoa agizo hilo leo Jijini Dodoma wakati wa uzinduzi wa Kampeni ya Kimataifa ya Uuguzi Sasa inayolenga kuinua hadhi na muonekano wa kada ya Uuguzi.

“Nataka kuona wauguzi wanafanya kazi kwa kuzingatia miongozo na maadili ya taaluma ya kada ya uuguzi na kuwa na heshima na utu kwa wagonjwa” alisema Waziri Ummy na kuendela “Nimefurahi kuona kwenye kampeni hii mmejipanga kuondoa changamoto zilizopo”

Aidha Waziri Ummy amewataka viongozi kuwatambua wauguzi ambao wamekuwa hawana kauli nzuri na kuwachukulia hatua ili kuondokana na vitendo vya wauguzi kutoa kauli za kebehi kwa wateja na kuwaasa wauguzi kuacha lugha za kebehi na zisizowafurahisha wateja kwani kufanya hivyo kuwachafua taswira ya wauguzi nchini.

Licha ya changamoto zilizopo Waziri Ummy hakusita kutoa pongezi kwa wauguzi ambao wamekuwa na mchango mkubwa katika utoaji wa huduma za afya nchini. “Napenda kuwapongeza wauguzi wote kwa kazi mnayofanya, Kazi ya wauguzi wanne inafanywa na muuguzi mmoja, Kazi ya wakunga watano, inafanywa na mkunga mmoja” alisema Waziri Ummy.

Naye Rais wa Chama cha Wauguzi nchini Tanzania (TANNA) Bw. Paul Magesa amekiri kuwepo kwa baadhi ya wauguzi wasio na maadili katika kazi amabo wamekuwa wakitoa kauli mbaya kwa wagonjwa huku akiahidi kuwa kupitia chama anachoongoza changamoto hizo zitatatuliwa ndani ya muda mfupi.

Aidha Bw. Magesa alitumia nafasi hiyo kuipongeza Serikali kwa kuongeza bajeti ya dawa nchini ambapo sasa dhana ya wauguzi kuwa ndio wezi wa dawa inaanza kufutika katika jamii.

“Hapo awali tulionekana sisi wauguzi ndio wezi wa dawa, tunaotumia vibaya dawa lakini ukweli ni kwamba dawa hazikuwepo, kitendo cha Serikali kuongeza bajeti ya dawa kimetusafisha sisi wauguzi” alisema Bw. Paul Magesa.

Kwa upande wake Mkurugenzi wa Idara ya Uuguzi kutoka Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia Wazee na Watoto Bw. Gustav Moyo amesema kuwa Kampeni ya Uuguzi Sasa imekuja wakati mwafaka kuja kutatua changamoto zilizopo muda mrefu ambazo zimekuwa zikikwamisha utendaji kazi wa wauguzi nchini.

Bw. Gustav amesema kuwa Uuguzi sasa ni kampeni ya kimataifa inayokusudia kuongeza hadhi na muonekano wa kada ya uuguzi nchini ambayo inalenga kuwawezesha wauguzi na wakunga kufikia na kumudu malengo ya afya ya karne ya 21 pamoja na changamoto zake.

0 on: "WAUGUZI WATAKIWA KUZINGATIA MAADILI KATIKA SEHEMU ZAO ZA KAZI"