Like us on Facebook

Inaendeshwa na Blogger.

Tafuta katika Blogu Hii

Kumbukumbu la Blogu

Instagram

visitors

display number of visitors

Popular Posts

Pages

Flickr Images

Jumamosi, 23 Februari 2019

HOSPITALI ZOTE NCHINI ZATAKIWA KUWA NA ICU YA WATOTO WACHANGA





Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe.Ummy Mwalimu akimtazama mtoto njiti, aliyepakatwa na mamaye,  wakati alipofanya ziara ya kukagua hali ya utoaji huduma za Afya katika Hospitali teule ya Rufaa ya Mkoa wa Pwani Tumbi.

Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe.Ummy Mwalimu akiongea na mama Mjamzito wakati alipofanya ziara ya kukagua hali ya utoaji huduma za Afya katika Hospitali teule ya Rufaa ya Mkoa wa Pwani Tumbi.

Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe.Ummy Mwalimu akieleza Waandishi wa Habari (hawapo kwenye picha) umuhimu wa kifaa kinacho rekodi mahudhurio na muda wa watumishi kufika ofisini (Biometric)  wakati alipofanya ziara ya kukagua hali ya utoaji huduma za Afya katika Hospitali teule ya Rufaa ya Mkoa wa Pwani Tumbi.

Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe.Ummy Mwalimu akimjulia hali mama aliyetoka kujifungua, wakati alipofanya ziara ya kukagua hali ya utoaji huduma za Afya katika Hospitali teule ya Rufaa ya Mkoa wa Pwani Tumbi.


Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe.Ummy Mwalimu akitoa maelekezo kwaMganga Mfawidhi, wakati wa ziara yake ya kukagua hali ya utoaji huduma za Afya katika Hospitali hiyo.

Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe.Ummy Mwalimu akiwa katika picha ya pamoja na Madaktari Bingwa wa Hospitali teule ya Mkoa wa Pwani Tumbi, baada ya kumaliza ziara yake ya kukagua hali ya utoaji huduma za Afya katika Hospitali hiyo.



HOSPITALI ZOTE  NCHINI ZATAKIWA KUWA NA ICU YA WATOTO WACHANGA


NA WAMJW - PWANI

WAZIRI wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu ameziagiza Hospitali za rufaa zote nchini kuwa na ICU kwaajili ya watoto wachanga ili kupunguza vifo vifo vyao.

Waziri Ummy amesema hayo wakati wa ziara yake ya kukagua hali ya utoaji wa huduma za Afya katika Hospitali teule ya Rufaa ya Mkoa wa Pwani Tumbi.

Waziri Ummy  ameagiza hayo kupitia kwa Mganga Mfawidhi wa Hospitali hiyo kuwa ahakikishe watoto wachanga lazima wawe na ICU yao ili kuhakikisha vifo vya Watoto wachanga vinapungua nchini.

"Watoto wachanga wagonjwa, wawe na ICU yao, lengo letu kama Serikali ni kupunguza Vifo vya Watoto wachanga, kwasababu tukipunguza vifo vya Watoto wachanga, tutakuwa tumepunguza vifo vya Watoto wanye umri wa chini ya miaka mitano" alisema Waziri Ummy.

Waziri Ummy aliendelea kusema kuwa karibu 40% ya vifo vya watoto ni watoto wachanga na katika kila Watoto 100, Watoto 40% ni Wachanga, hivyo Serikali inaendelea kuchukua jitihada za makusudi ili kupunguza vifo hivi, ikiwemo kusisitiza kila Hospitali nchini kuwa na ICU.

"Karibu 40% ya vifo vya watoto ni watoto wachanga na katika kila Watoto 100, Watoto 40% ni Wachanga, kwahiyo Daktari ni lazima tulifanyie kazi agizo hilo" alisema Waziri Ummy.

Licha ya changamoto alizokutana nazo Waziri Ummy amesema kuwa Serikali inatarajia kujenga jengo mahususi kwaajili ya huduma za Dharura katika Hospitali zote za Rufaa za Mikoa nchini ili kuokoa maisha ya wagonjwa, hasa waliopata ajali.

"Nafurahi kusema, Serikali imeahapata fedha kwahiyo tutakuwa na jengo mahususi kwaajili ya huduma za Dharura na wagonjwa wa ajali, na hii tunataka iwe katika Hospitali za Rufaa za Mikoa zote ili mgonjwa aweze kuokolewa maisha muda mfupi anapofika Hospitali" alisema Waziri Ummy.

Pia, Waziri Ummy ameridhishwa kwa kiasi kikubwa juu ya hali ya upatikanaji wa dawa nchini, huku akiwatoa hofu Mwananchi kuwa Serikali kupitia Bohari ya Dawa (MSD) ina dawa zakutosha.

Aliendelea kusema kuwa Serikali imeainisha fani nane nane za kipaumbele ili kuwa na madaktari Bingwa wawili katika kila fani ikiwemo, Daktari Bingwa wa Watoto, Daktari Bingwa wa magonjwa yakina mama na uzazi, Daktari Bingwa wa upasuaji wajumla, Bingwa wa upasuaji wa mifupa, Daktari Bingwa wa magonjwa ya ndani (Physician) n.k

Mbali na hayo Waziri Ummy amesema kuwa katika Mkoa wa Pwani Serikali imejenga na kuboresha vituo vya Afya zaidi ya 16, Hospitali za Wilaya 3, na kuboresha Hospitali ya Mikoa ili kuwa na huduma za wagonjwa mahututi na wagonjwa wa Dharura.

Mbali na hayo Waziri Ummy amewahasa Mwananchi kujiunga na mfuko wa Bima ya Afyà ili kujihakikishia matibabu wakati wa ugonjwa, jambo litalosaidia kuokoa gharama kubwa za matibabu pindi Mwananchi anapopata ugonjwa.

"Nitoe Wito kwa Wananchi kujenga utaratibu wakujiunga na Bima ya Afya, kwasababu ndio njia ya uhakika yakujihakikishia matibabu kabla hawajaugua" alisema Waziri Ummy.

Mwisho.

0 on: " HOSPITALI ZOTE NCHINI ZATAKIWA KUWA NA ICU YA WATOTO WACHANGA"