Like us on Facebook

Inaendeshwa na Blogger.

Tafuta katika Blogu Hii

Kumbukumbu la Blogu

Instagram

visitors

display number of visitors

Popular Posts

Pages

Flickr Images

Ijumaa, 22 Februari 2019

SERIKALI YAWAHASA WANANCHI KUWAPELEKA WATOTO KUPATA CHANJO

Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe.Ummy Mwalimu   akipokea vishikwambi (tablets) kwaajili ya kukusanyia taarifa katika vituo vya Afya hapa nchini, kutoka kwa Mkuu wa Masuala ya Afya UNICEF Kyaw Aung, (Wakwanza kushoto)  tukio limefanyika katika Ofisi ndogo za Wizara ya Afya jijini Dar es salaam. Pembeni kwa Waziri Ummy ni Meneja wa Mpango wa chanjo Taifa Dafrosa Lyimo.

Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe.Ummy Mwalimu  akielezea jambo mbele ya Waandishi wa Habari wakati akipokea majokofu ya kutunzia chanjo na vishikwambi (tablets) kwaajili ya kukusanyia taarifa katika vituo vya Afya hapa nchini, tukio limefanyika katika Ofisi ndogo za Wizara ya Afya jijini Dar es salaam. Wakatikati ni Mganga Mkuu wa Serikali Prof Muhammad Bakari Kambi, na Wakwanza kushoto ni Meneja wa Mpango wa chanjo Taifa Dafrosa Lyimo.

Mkuu wa Masuala ya Afya UNICEF Kyaw Aung akieleza jambo mbele ya Waandishi wa Habari katika mapokezi ya majokofu ya kutunzia chanjo na vishikwambi (tablets) kwaajili ya kukusanyia taarifa katika vituo vya Afya hapa nchini, yaliyofanywa na Waziri wa Afya Mhe. Ummy Mwalimu (wakatikati) tukio limefanyika katika Ofisi ndogo za Wizara ya Afya jijini Dar es salaam.

Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe.Ummy Mwalimu   akipokea majokofu ya kutunzia chanjo, kutoka kwa Mkuu wa Masuala ya Afya UNICEF Kyaw Aung (Watatu kushoto)  tukio limefanyika katika Ofisi ndogo za Wizara ya Afya jijini Dar es salaam. Kulia kwa Waziri Ummy ni Mganga Mkuu wa Serikali Prof Muhammad Bakari Kambi, Mkurugenzi wa Kinga Dkt. Leonard Subi na Meneja wa Mpango wa chanjo Taifa Dafrosa Lyimo.

Waandishi wa Habari wakimsikiliza Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe.Ummy Mwalimu  wakati akipokea majokofu ya kutunzia chanjo na vishikwambi (tablets) kwaajili ya kukusanyia taarifa katika vituo vya Afya hapa nchini, tukio limefanyika katika Ofisi ndogo za Wizara ya Afya jijini Dar es salaam.


SERIKALI YAWAHASA WANANCHI KUWAPELEKA WATOTO KUPATA CHANJO


Na WAMJW – DSM

WAZIRI wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu leo amewahasa Wazazi na Walezi nchini kuakikisha wanawapeleka watoto kupata huduma za chanjo ili kujikinga dhidi ya maradhi yanayozuilika kwa chanjo.

Waziri Ummy amesema haya leo wakati akipokea majokofu ya kutunzia chanjo na vishikwambi (Tablets) kwa ajili ya kukusanya taarifa za chanjo katika vituo vya kutolea huduma za afya hapa nchini.

Waziri Ummy alisema kuwa imethibitika kuwa yapo magonjwa zaidi ya 20 nambayo yanadhibitika kwa njia ya chanjo hivyo ni muhimu kwa wazazi na walezi ambao hawajawapeleka watoto kupata chanjo kuitumia fursa hii ili watoto wao wapate chanjo

“Sasa hivi imeshathibitika kuna magonjwa zaidi ya 20 ambayo yanadhibitika kupitia njia ya chanjo , ni lazima wahakikishe Wazazi ambao hawajawapeleka watoto wao kupata chanjo , ni lazima wapate tena dozi zote.” Alisema Waziri Ummy.

Waziri ummy, alisema kuwa serikali kwa kushirikiana na shirika la gavi, imefanikiwa kununua jumla ya majokofu 1,385 yenye thamani ya shilingi bilioni 13,991,270,300, huku ikichangia kwa 20% na gavi 80%, kwa ajili ya kuimarisha mnyororo baridi wa utunzaji wa chanjo katika vituo vya kutolea huduma za afya hapa nchini.

Aliendelea kusema kuwa Majokofu 1,190 yanatumia nishati ya jua na kila jokofu lina thamani ya shilingi milioni 10,879,000 na majokofu 195 yanatumia umeme, na kila jokofu lina thamani ya shilingi milioni 5,361,000.

Vilevile Waziri ummy alisema, Serikali na shirika la Gavi imenunua jumla ya vishikwambi (tablets) 1,249 vyenye gharama ya shilingi  bilioni 1,598,720,000 kwa ajili ya kukusanya na kuhifadhi taarifa za chanjo kwa njia ya mtandao, na kila kishikwambi kina thamani ya shilingi milioni 1,280,000.

Aidha, Waziri Ummy alisema kuwa mapema mwezi Mei tutapokea jumla ya vishikwambi 2100 venye thamani ya shilingi bilioni 2,688,000,000 na mwishoni mwa mwaka huu, tutapokea awamu nyingine ya majokofu yenye thamani ya shilingi bilioni 11,533,357,820 na kufikia asilimia zaidi 80 ya mahitaji ya majokofu na vishikwambi katika vituo vyote hapa nchini.

Mbali na hayo, Waziri Ummy amesema kuwa Halmashauri zote za Tanzania Bara pamoja na Wilaya za Zanzibar zitapokea majokofu haya kwa awamu kuu mbili, ambapo Awamu ya kwanza itahusisha mikoa 15 ambayo ni Dodoma, Geita, Kagera, Kigoma, Lindi, Tanga, Mara, Mbeya, Mtwara, Mwanza, Shinyanga, Songwe, Unguja, Pwani na Singida huku awamu ya pili itahusisha mikoa iliyobaki.

Hata hivyo, katika kuhakikisha ufanisi na ufuatiliaji wa utendaji kazi wa majokofu ya kuhifadhia chanjo, Wizara ya Afya kwa kushikiana na wadau wa shirika la JSI na Nexleaf kwa ufadhili wa Gavi, inatarajia kufunga vifaa vya kupima na kufuatilia halijoto katika vituo takribani 5,000 kati ya vituo zaidi ya 7,000 kote nchini. 

Waziri Ummy aliendelea kusema kuwa, Vifaa hivi vinamuwezesha Afisa Chanjo kujua utendaji kazi wa jokofu ikiwa ni pamoja na kujua halijoto ya jokofu katika vituo vya huduma za afya bila ya kulazimika kufika katika kituo husika, Vifaa hivi vinatuma ujumbe mfupi wa maneno (SMS) pindi halijoto inapopanda au kushuka. 

Mwisho.

0 on: " SERIKALI YAWAHASA WANANCHI KUWAPELEKA WATOTO KUPATA CHANJO"