Like us on Facebook

Inaendeshwa na Blogger.

Tafuta katika Blogu Hii

Kumbukumbu la Blogu

Instagram

visitors

display number of visitors

Popular Posts

Pages

Flickr Images

Alhamisi, 14 Februari 2019

SERIKALI YAAHIDI KUANZA KUJENGA VITUO VYA UTENGAMAO KWA AJILI YA WATOTO WENYE ULEMAVU NCHINI


Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Ummy Mwalimu akihutubia wananchi, wadau, wazazi na walezi wa watoto wenye ulemavu (hawapo pichani) wakati wa ufunguzi wa kituo kipya cha utengamao wa watoto wenye ulemavu cha Kila Siku kilichopo Kawe Jijini Dar Es Salaam.

Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Ummy Mwalimu akifungua jiwe la msingi lililowekwa katika ujenzi wa kituo kipya cha utengamao wa watoto wenye ulemavu kilichopo Kawe Jijini Dar Es Salaam. Kushoto ni Balozi wa Italia nchini Tanzania Bw. Roberto Mengoni na katikati ni Mkuu wa Shirika la Comunita Solidali nel Mondo Bw. Michelangelo Chiurchiu.


Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Ummy Mwalimu akisikiliza jambo alilokua akielezwa na Mkuu wa Shirika la Comunita Solidali nel Mondo Bw. Michelangelo Chiurchiu wakati wa ufunguzi wa kituo kipya cha Utengamao wa Watoto wenye ulemavu kilichopo Kawe Jijini Dar Es Salaam.

Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Ummy Mwalimu akikata utepe kuashiria ufunguzi wa kituo kipya cha utengamao wa watoto wenye ulemavu cha Kila Siku kilichopo Kawe Jijini Dar. Kushoto ni Mkuu wa Shirika la Comunita Solidali nel Mondo Bw. Michelangelo Chiurchiu na Kulia ni Balozi wa Italia nchini Tanzania Bw. Roberto Mengoni.
Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Ummy Mwalimu akisalimiwa na mmoja wa watoto wenye ulemavu wakati alipotembelea maeneo wanapofundishwa utengamao katika kituo cha utengamao cha Kila Siku kilichopo Kawe Jijini Dar Es Salaam.

Baadhi ya wadau, wazazi na walezi wa watoto wenye ulemavu wakifuatilia hotuba mbalimbali zilizotolewa katika ufunguzi wa kituo kipya cha utengamao wa watoto wenye ulemavu cha Kila Siku kilichopo Kawe Jijini Dar Es Salaam.

SERIKALI YAAHIDI KUANZA KUJENGA VITUO VYA UTENGAMAO KWA AJILI YA WATOTO WENYE ULEMAVU NCHINI

Na WAMJW-DAR

Serikali kupitia Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto imetangaza nia ya kuanza kujenga vituo vya utengamao kwa watoto wenye ulemavu nchini (Rehabilitation Centers).

Hayo yamesemwa leo na Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu wakati wa ufunguzi wa kituo kipya cha utengamano wa watoto wenye ulemavu cha Kila Siku( Community Based Rehabilitation Centre) kilichopo Kawe Jijini Dar Es Salaam.

“Ninaahidi kwenye kila kituo cha afya cha serikali ni lazima tuanze kujenga majengo ya utengamao kwa ajili ya watoto wenye ulemavu, tuna takribani vituo vya afya 510 nchini tunaweza tusijenge kwenye vituo vyote kwa wakati mmoja lakini naamini tunaweza tukaanza na vituo vya afya 50”. Amesema Waziri Ummy.

Waziri Ummy amesema kuna changamoto za kupata takwimu sahihi za watu wenye ulemavu ambapo kupitia sensa ya watu na makazi ya mwaka 2012 inaonesha watu wenye ulemavu nchini ni asilimia 5.8 na kati ya hao asilimia 60 ni watoto chini ya miaka 18.

Kufuatia hali hiyo Waziri Ummy ameomba wadau mbalimbali wa Afya waweze kusaidiana na Serikali katika kutekeleza azma ya kujenga vituo hivyo, lengo likiwa ni kuwafikia wanawake na walezi wengi wenye watoto wenye ulemavu nchini. 

Waziri Ummy amesema kuna uhaba mkubwa wa vituo vya Utengamao nchini huku akitoa mfano wa Jiji la Dar Es Salaam lenye vituo visivyozidi 6 lakini idadi ya watu ikiwa ni zaidi ya Milioni 5. Hata hivyo Waziri Ummy ameupongeza uongozi wa Kituo hicho cha Kila Siku Community Based Rehabilitation kwa kuanzisha huduma za utengamao kwa watoto wenye ulemavu na kuwataka wazazi na walezi kuwapeleka watoto wenye ulemavu kwenye vituo hivyo kuliko kuwafungia ndani.

Aidha, Waziri Ummy ameagiza Maafisa Ustawi wa Jamii kuhakikisha wanatoa elimu kwa wazazi na walezi wenye watoto wenye ulemavu kwenye maeneo yao ili kuondoa dhana potofu ya kufungia ndani watoto na kuwanyima haki zao za msingi.

Kwa upande wake Mkuu wa Shirika la Comunita Solidali nel Mondo kutoka nchini Italia Bw. Michelangelo Chiurchiu amesema lengo la kuanzishwa kituo hicho ni ujumuishwaji kwa wote wenye lengo la kuboresha maisha ya watu wenye ulemavu kupitia uboreshaji wa huduma za utengamao kijamii, kujenga uwezo wa kiuchumi kwa watu wenye ulemavu pamoja na ujumuishwaji wa watoto wenye ulemavu katika elimu ndani ya mkoa wa Dar Es Salaam.

1 on: "SERIKALI YAAHIDI KUANZA KUJENGA VITUO VYA UTENGAMAO KWA AJILI YA WATOTO WENYE ULEMAVU NCHINI"
  1. The position of zero on the horizontal axis reveals that you're extra more likely to|prone to} lose cash than to generate income, regardless of which guess you choose. In each histograms, lower than 50% of the realm is to the proper of zero. The operate split_winnings takes a pocket as its argument and returns 17 if the 빅카지노 pocket is either zero or 00. The distributions above gave us an image of the whole random pattern. But typically we're just excited about one or two quantities computed based mostly on the pattern. At this level, this other team the sport designers hand their work off to applies a weighted average to this listing of outcomes.

    JibuFuta