Like us on Facebook

Inaendeshwa na Blogger.

Tafuta katika Blogu Hii

Kumbukumbu la Blogu

Instagram

visitors

display number of visitors

Popular Posts

Pages

Flickr Images

Ijumaa, 15 Februari 2019

"TUMEWEKA MBELE MASLAHI YA WANACHAMA WETU" - Mkurugenzi Mkuu NHIF

Mkurugenzi Mtendaji Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya Bw. Bernard Konga akisema jambo wakati wa ufunguzi wa Mkutano wa Baraza la Pili la Wafanyakazi wa Mfuko huo Jijini Dodoma.

Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Dkt Binilith Mahenge akisema jambo wakati wa ufunguzi wa Mkutano wa Baraza la Pili la Wafanyakazi wa Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya.

Na NHIF - Dodoma

Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya, Bw. Bernard Konga amesema kuwa mikakati yote inayowekwa na Mfuko huo inazingatia maslahi ya wanachama na wananchi kwa ujumla katika uimarishaji wa huduma za matibabu nchini.

Hayo ameyasema mbele ya Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Dkt. Bilinith Mahenge wakati wa ufunguzi wa Baraza la Wafanyakazi la Mfuko ambalo limeketi leo kwa lengo la kujadili masuala mbalimbali yakiwemo ya uimarishaji wa huduma na mikakati ya kuwafikia wananchi katika maeneo yote.

“Nikuhakikishie Mkuu wa Mkoa kuwa timu iliyoko hapa ya Wajumbe wa Baraza itahakikisha inaweka mipango inayozingatia maslahi ya wanachama wetu lakini pia utekelezaji wa azma ya Serikali ya kuhakikisha kila mwananchi anakuwa kwenye utaratibu wa kupata matibabu kwa bima ya afya,” alisema Bw. Konga.

Alisema kuwa mikakati iliyopo kwa sasa ni kuyafikia makundi yote yakiwemo ya wakulima, wavuvi, wafugaji, wakwezi na makundi mengine na hili litafanikiwa kupitia uanzishwaji wa vifurushi vipya ambavyo vina gharama nafuu kwa kila mwananchi.

Mkurugenzi Mkuu alisema kuwa, Mfuko unatarajia kuzindua rasmi mpango wa vifurushi vipya mwezi Machi mwaka huu ambavyo vimeandaliwa kwa kuzingatia mahitaji halisi ya wananchi katika huduma za matibabu.

Akifungua baraza hilo, Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Dkt. Mahenge alisisitiza juu ya uwekaji wa mikakati ya kuwafikia wananchi wa ngazi zote ili kuwezesha kila mtanzania kuwa na uhakika wa kupata matibabu yenye wakati wowote anapopatwa na maradhi.

Alitumia fursa hiyo pia kuupongeza Mfuko kwa jitihada mbalimbali za uimarishaji wa huduma za matibabu nchini ikiwemo uwekezaji katika  ujenzi wa Hospitali ya Benjamin Mkapa na maeneo mengine ambayo Mfuko umekuwa na mchango mkubwa katika kuboresha miundombinu.

“Wajumbe wa kikao hiki hakikisheni mnatumia muda wenu vizuri kwa kuweka mikakati ambayo ni imara itakayoufanya Mfuko uhudumie watanzania wote lakini pia vizazi na vizazi,” alisema Mkuu wa Mkoa.

Mwisho.

0 on: ""TUMEWEKA MBELE MASLAHI YA WANACHAMA WETU" - Mkurugenzi Mkuu NHIF"