Like us on Facebook

Inaendeshwa na Blogger.

Tafuta katika Blogu Hii

Kumbukumbu la Blogu

Instagram

visitors

display number of visitors

Popular Posts

Pages

Flickr Images

Alhamisi, 14 Februari 2019

Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Faustine Ndugulile akikata utepe, ishara ya ufunguzi rasmi wa uzinduzi wa kambi ya upasuaji kwa watu wenye ugonjwa wa Mabusha, uliofanyika katika Hospitali ya Vijibweni Kigamboni, wakwanza kushoto ni Mkurugenzi wa NIMRI Prof. Yunus Mgaya.

Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Faustine Ndugulile akiwajulia hali wagonjwa waliokwisha fanyiwa upasuaji wa Mabusha baada ya kufanya uzinduzi wa kambi ya upasuaji kwa watu wenye ugonjwa wa Mabusha, uliofanyika katika Hospitali ya Vijibweni Kigamboni.

Wananchi waliojitokeza kumsikiliza Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Faustine Ndugulile (jayupo kwenye picha) wakati wa uzinduzi wa kambi ya upasuaji kwa watu wenye ugonjwa wa Mabusha, uliofanyika katika Hospitali ya Vijibweni Kigamboni.

Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Faustine Ndugulile akisisitiza jambo mbele ya Wananchi waliojitokeza kumsikiliza (hawapo kwenye picha) wakati wa uzinduzi wa kambi ya upasuaji kwa watu wenye ugonjwa wa Mabusha, uliofanyika katika Hospitali ya Vijibweni Kigamboni.

Mratibu wa Mpango wa taifa wa kudhibiti Magonjwa yaliyokuwa hayapewi kipaumbele, Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Upendo Mwingira akitabasamu, baada yakupata pongezi kutoka kwa Naibu Waziri wa Afya Dkt Faustine Ndugulile, kwa  kazi nzuri anayoifanya ya kutokomeza Matende na Mabusha.

Madaktari kutoka Hospitali ya Vijibweni Kigamboni wakifanya upasua wa kutoa busha leo, katika uzinduzi wa kambi ya upasuaji kwa watu wenye ugonjwa wa Mabusha, uliofanywa na Naibu Waziri wa Afya Dkt. Faustine Ndugulile (Hayupo kwenye Picha)



HALMASHAURI ZATAKIWA KUWEKA MIKAKATI THABITI  ILI KUTOKOMEZA UGONJWA WA MABUSHA.


Na WAMJW – DSM

NAIBU Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Faustine Ndugulile ameziagiza Halmashsuri zote nchini kuhakikisha zinaweka mikakati thabiti ili kutokomeza Magonjwa ya Matende na Mabusha nchini.

Ameyasema hayo leo wakati wa Uzinduzi wa kambi ya upasuaji kwa watu wenye tatizo la ugonjwa wa Mabusha na kuangalia hali ya utoaji Huduma za Afya katika Hospitali ya Vijibweni Manispaa ya Kigamboni Mkoa wa Dar es salaam.

Dkt. Ndugulile amesema kuwa Halmashsuri zote nchini wakati zinaandaa Vipaumbele ni lazima watenge bajeti kwaajili ya mipango endelevu ili kuhakikisha kwamba zinaweza kupambana na Magonjwa haya yaliyokuwa hayapewi kipaumbele bila kuwategemea Wafadhili.

“Niwaombe sana, Wakati mnaandaa Mipango hii, tusiweke masuala mengi ya Semina, tuelekeze nguvu katika intervention, tuweke vitu ambavyo vitaleta mabadiliko, tutenge fedha kwaajili ya mipango endelevu, kwaajili yakuhakikisha kwamba tunaanza kujisimamia katika Magonjwa haya, haipendezi kama nchi kwenda kulia kwa Wafadhili kwa mambo ambayo tunaweza kuyafanya” Alisema Dkt. Ndugulile.

Mbali na hayo, Dkt. Ndugulile amesema kuwa, kati ya Wilaya 120 ambazo zilikuwa na uambukizo wa magonjwa haya, Wilaya  96 zimeweza kupunguza maambukizi kwa asilimia 80, hivyo kufikia kiwango cha kusimamisha ugawaji wa Kingatiba kwa jamii katika Wilaya hizo.

Dkt ndugulile aliendelea kuwahasa wakazi wa Mkoa wa Dar es Salaam kushiriki kikamilifu pindi yanapotokea mazoezi kama haya ili tuweze kutokomeza ugonjwa wa Matende na Mabusha, kwani bado Mkoa wa Dar es Salaam, maambukizi yapo juu kwa kiwango cha asilimia 10. 

Aidha, Dkt ndugulile amesema kuwa Watu wapatao 206,708 sawa na asilimia 87.47 katika Manispaa ya Kigamboni walipatiwa Kingatiba, na kwa Manispaa ya Ubungo Watu wapatao 997,632 sawa na asilimia 87.36 walipatiwa Kingatiba, huku manispaa zote za Mkoa wa Dar es Salaam, jumla ya watu wapatao 5,127, 596 sawa na asilimia 87.63 walipatiwa Kingatiba hiyo. 

Kwa upande mwingine Dkt. Ndugulile amesema kuwa Serikali kupitia uhisani wa CNTD, inatarajia kuwafanyia upasuaji watu 400 wakazi wa Manispaa za Kigamboni na Ubungo huku akiwaomba Wananchi wa Manispaa hizo kujitokeza ili kutumia vizuri fursa hii adimu.

Nae Mratibu Mpango wa Taifa wa Kudhibiti Magonjwa yaliyokuwa hayapewi kipaumbele Dkt. Upendo Mwingira amesema kuwa Serikali kupitia Mpango huu kwa kushirikiana na Wadau  inatoa huduma hii ya upasuaji kwa wagonjwa hawa bila malipo, hivyo kuwahasa watu wenye ugonjwa huu kujitokeza ili kupata huduma hii.

Nae Shuhuda aliyepata huduma hii ya upasuaji Bw. Ahmed Abrahaman amewahasa Watu wengine walio na ugonjwa huu kujitokeza kupata huduma hii ya upasuaji ili kuondokana na aibu hii kwa jamii, huku akisisitiza kuwa upasuaji huu unafanyiwa kwa njia za kisasa na wa muda mfupi sana.

0 on: " "