Like us on Facebook

Inaendeshwa na Blogger.

Tafuta katika Blogu Hii

Kumbukumbu la Blogu

Instagram

visitors

display number of visitors

Popular Posts

Pages

Flickr Images

Ijumaa, 15 Februari 2019

SEKTA YA AFYA ISIWE KIKWAZO KWA WANANCHI KUPATA MATANGAZO YAO MAPEMA

Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Faustine Ndugulile akiangalia daftari la matibabu kutoka kwa moja kati ya wazazi waliopeleka watoto wao kupata huduma katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa ya Mwananyamala, wakati wa ziara yake ya kukagua hali ya utoaji huduma za Afya katika Hospitali hiyo.

Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Faustine Ndugulile akimsalimia moja Kati ya Wazee waliofika kupata huduma za Afya katika  Hospitali ya Rufaa ya Mkoa ya Mwananyamala, wakati alipofanya ziara ya kukagua hali ya utoaji huduma za Afya katika Hospitali hiyo.

Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Faustine Ndugulile akifanya ukaguzi katika chumba cha kuhifadhia Dawa wakati alipofanya ziara ya kukagua hali ya utoaji huduma za Afya katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa ya Mwananyamala.

Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Faustine Ndugulile akipata maelezo kutoka kwa Mtaalamu wa Maabara katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa ya Mwananyamala, wakati wa ziara yake ya kukagua hali ya utoaji huduma za Afya katika Hospitali hiyo.
Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Faustine Ndugulile akiongea na moja kati ya wazazi waliopeleka watoto wao kupata huduma katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa ya Mwananyamala, wakati wa ziara yake ya kukagua hali ya utoaji huduma za Afya katika Hospitali hiyo.
SEKTA YA AFYA ISIWE KIKWAZO KWA WANANCHI KUPATA MATANGAZO YAO MAPEMA.

Na WAMJW - DSM

NAIBU Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Faustine Ndugulile ameagiza Sekta ya Afya kutokuwa kikwazo kwa wananchi kupata Matangazo ya kuzaliwa kwa watoto kwa ajili ya kupata cheti cha kuzaliwa kwa muda mfupi.

Ameyasema hayo leo, wakati alipofanya ziara ya kukagua hali ya utoaji huduma za Afya katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa Mwananyamala jijini Dar ea salaam.

Dkt. Ndugulile amesema kuwa Hospitali hiyo ni lazima ichukue juhudi za makusudi, ikiwemo kuongeza wafanya kazi ili kuhakikisha kwamba Watoto wote wanaweza kupata matangazo yao ndani ya Wiki moja, jambo litaloepusha usumbufu kwa Mwananchi ambao unaweza kuepukika.

" Sisi kama sekta ya Afya, tusiwe kikwazo, vya Mwananchi kupata haya matangazo, na hili nimeliona nimeshatoa maelekezo juu ya hili, na ndani ya wiki moja nategemea kwamba tatizo hili litakuwa limetatuliwa" Alisema Dkt. Ndugulile

Dkt. Ndugulile akiongeza kuwa Matangazo haya ni ya muhinu sana katika mchakato wa kupata vyeti vya kuzaliwa, hivyo Mganga Mfawidhi ni lazima aweke mikakati thabiti ikiwemo kuongeza watu ili kuhakikisha kuanzia sasa matangazo yawe yanatoka ndani ya masaa 24. 

Kwa upande mwingine Dkt. Ndugulile amesema kuwa katika kupambana na changamoto ya msongamano wa watu katika Hospitali hiyo, Serikali imeboresha zaidi ya vituo vya Afya 350, huku zikijengwa Hospitali za Wilaya 67, na Hospitali za mikoa 2, ili wananchi waweze kupata huduma katika ngazi ya chini kabla yakufikia katika Hospitali za Rufaa.

"Kama Serikali tunachofanya ni kuboresha vituo vya Afya karibia 350, tunajenga Hospitali za Wilaya 67, na Hospitali za Rufaa za Mikoa 2, hivyo tunatarajia hizi Hospitali zinkianza kufanya kazi na huduma za upasuaji zikianza kupatikana kule, huu msongamano utaamia kule" alisema Dkt. Ndugulile

Mbali na hayo Dkt. Ndugulile amewapongeza watu wote wenye VVU kujitokeza kupata matibabu, huku lengo la Serikali ni kufikia 909090, yaani 90 watu wote walio na Virusi vya Ukimwi waweze kufikiwa na kupimwa, 90 ya pili ni kuhakikisha waliopimwa waweze kuanzishiwa dawa papo kwa papo, na 90 ya tatu ya walioanzishiwa dawa waweze kufubaza virusi vyao vya Ukimwi, yote ni kuhakikisha ifikapo 2030 pasiwe na maambukizi mapya ya virusi vya Ukimwi.

Nae Mganga Mfawidhi wa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa ya Mwananyamala Dkt. Mkungu Daniel mesema kuwa Hospitali hiyo inapokea Mwananchi zaidi ya 2000, huku akisisitiza kuwa Hospitali hiyo ipo katika hatua yakujenga jengo ambalo litabeba jumla ya vitanda 150 kwaajili ya mama na mtoto ili kupambana na changamoto hiyo ya msongamano


0 on: "SEKTA YA AFYA ISIWE KIKWAZO KWA WANANCHI KUPATA MATANGAZO YAO MAPEMA"