Like us on Facebook

Inaendeshwa na Blogger.

Tafuta katika Blogu Hii

Kumbukumbu la Blogu

Instagram

visitors

display number of visitors

Popular Posts

Pages

Flickr Images

Jumatano, 13 Februari 2019

WANANCHI WATAKIWA KUJIUNGA NA MFUKO WA TAIFA WA BIMA YA AFYA

Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu akizungumza mbele ya wadau wa Bima ya Afya kwa wananchi walio katika Sekta zisizo Rasmi katika mkutano uliojumuisha wajumbe kutoka nchi mbalimbali uliofanyika leo Jijini Dar Es Salaam.

Mwenyekiti wa bodi ya Mfuko wa Taifa (NHIF) Bi. Anna Makinda akiongea mbele ya wadau wa Bima ya Afya kwa wananchi walio katika Sekta zisizo Rasmi katika mkutano uliojumuisha wajumbe kutoka nchi mbalimbali uliofanyika Jijini Dar Es Salaam.

Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu akizungumza na Wabunge wa Bunge la Tanzania katika kikao cha Wadau wa Bima ya Afya kwa wananchi walio katika Sekta zisizo Rasmi katika mkutano uliojumuisha wajumbe kutoka nchi mbalimbali uliofanyika leo Jijini Dar Es Salaam.


Wadau mbalimbali wa Bima ya Afya kwa wananchi walio katika Sekta zisizo Rasmi wakisikiliza kwa makini mjadala uliokua ukiendelea katika mkutano uliojumuisha wajumbe kutoka nchi mbalimbali uliofanyika Jijini Dar Es Salaam.

Balozi wa Uswisi nchini Tanzania Bi. Florence Tinguely akizungumza mbele ya wadau wa Bima ya Afya kwa wananchi walio katika Sekta zisizo Rasmi katika mkutano uliojumuisha wajumbe kutoka nchi mbalimbali uliofanyika Jijini Dar Es Salaam.

Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu akiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya wadau wa Bima ya Afya kwa wananchi walio katika Sekta zisizo Rasmi waliohudhuria katika mkutano uliojumuisha wajumbe kutoka nchi mbalimbali uliofanyika Jijini Dar Es Salaam.



Na WAMJW-DAR ES SALAAM

Wananchi wametakiwa kujiunga na mfuko wa Bima ya Afya ili kuondokana na adha wanayoipata pale wanapopata maradhi kwa kushindwa kugharamia matibabu na kusababisha madeni , umaskini na pengine kifo.

Hayo yamesemwa na Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu leo wakati alipohudhuria mkutano wa wadau wa Bima ya Afya kwa wananchi walio katika Sekta zisizo Rasmi uliojumuisha wadau kutoka nchi mbalimbali uliofanyika katika ukumbi wa Hoteli ya Serena jijini Dar Es Salaam.

“Tukiangalia hivi sasa asilimia 67 ya Watanzania wanalipa huduma za matibabu kwa kutoa hela mfukoni, maana yake ni kwamba Watanzania hawa wanapata changamoto pale ambapo wanapata maradhi kwa kutopata huduma nzuri kwa sababu hawana fedha lakini pia wanapata changamoto ya kuingia katika umaskini kwa sababu ya kugharamia matibabu”. Amesema Waziri Ummy.

Waziri Ummy amesema Wizara ya Afya kwa kushirikiana na Shirika la Afya Duniani (WHO) pamoja na Shirika la Kazi Duniani (ILO) imefanya tathmini mbalimbali na kugundua watu wengi hawana uelewa wa masuala ya Bima ya Afya lakini wana uwezo wa kulipa. Kufuatia hali hiyo Serikali imeamua kuboresha mfuko wa afya wa jamii “CHF Iliyoboreshwa” kwa gharama nafuu kwa watu watano kwa mwaka ili kuwawezesha wananchi wengi kujiunga na mfuko huo.

“Hivi sasa asilimia 67 ya wananchi hawana Bima ya Afya, hivyo wanatumia fedha taslimu kupata huduma. Hii ni changamoto kwa wengi kwa kuwa matibabu yana gharama kubwa na ugonjwa huja bila taarifa”. Amesema Waziri Ummy.

Kufuatia hali hiyo, Waziri Ummy ameeleza dhamira ya Serikali kukamilisha mchakato wa kupitisha Sheria ya Bima ya Afya kuwa ni lazima kwa kila mtu kabla ya mwisho wa mwaka huu 2019. Lengo la Serikali ni kuhakikisha kupitia utaratibu huu wananchi wengi hasa wa kipato cha chini wanapata huduma nzuri za matibabu na pia kuepuka kuingia kwenye umaskini kwa sababu ya ugonjwa.

Kikao hicho cha siku mbili kimejumuisha wajumbe kutoka nchi za Kenya, Congo, Ghana, Cameroon, Ethiopia, Ujerumani, Ufilipino, Chad, Zambia, Afrika Kusini, Uswisi pamoja na wenyeji Tanzania.

0 on: "WANANCHI WATAKIWA KUJIUNGA NA MFUKO WA TAIFA WA BIMA YA AFYA"