Like us on Facebook

Inaendeshwa na Blogger.

Tafuta katika Blogu Hii

Kumbukumbu la Blogu

Instagram

visitors

display number of visitors

Popular Posts

Pages

Flickr Images

Jumatano, 6 Februari 2019

MAAMBUKIZI YA UGONJWA TRACHOMA YAPUNGUA KWA ASILIMIA 75 NCHINI





Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Ummy Mwalimu akihutubia wageni waliofika katika uzinduzi wa mpango wa kudhibiti magonjwa yaliyokua hayapewi kipaumbele hususan Vikope (Trachoma) katika ukumbi wa Hotel ya Morena jijini Dodoma.

Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Ummy Mwalimu akimkabidhi cheti Harran Mkocha ambaye ni Mkurugenzi wa Kongwa Trachoma Project kutambua mchango katika mapambano dhidi ya kutokomeza ugonjwa wa Trachoma nchini. Kushoto ni Mkurugenzi wa The Queen Elizabeth Diamond Trust Fund Dkt. Astrid Bonfield na kulia ni Balozi wa Uingereza Nchini Sarah Cooke.
Wataalamu mbalimbali kutoka Taasisi ya The Queen Elizabeth Diamond Trust Fund na SightServers Tanzania pamoja na wawakilishi kutoka Wizara ya Afya wakiwa katika picha ya pamoja katika kijiji cha Bahi-Makulu Wilaya ya Bahi Mkoani Dodoma kulipokua na zoezi la upimaji na matibabu ya ugonjwa wa Trachoma kwa wananchi mbalimbali wa maeneo hayo.
Madaktari wakimfanyia upasuaji mgonjwa wa Vikope (trachoma) ambaye alifikia hatua ya kuelekea upofu katika zahanati ya Bahi-Makulu wilaya ya Bahi mkoani Dodoma.

Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Ummy Mwalimu akipiga picha ya pamoja na Mkurugenzi wa Taasisi ya SightServers Tanzania Bw. Gosbert Katunzi (Katikati), . Kushoto ni Mkurugenzi wa The Queen Elizabeth Diamond Trust Fund Dkt. Astrid Bonfield na kulia ni Balozi wa Uingereza Nchini Sarah Cooke.



NA WAMJW-DODOMA

Maambukizi ya ugonjwa wa vikope (Trachoma) yameonekana kupungua kwa zaidi ya aslimia 75 katika maeneo mbalimbali nchini.

Hayo yamesemwa leo na Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Ummy Mwalimu wakati wa uzinduzi wa mpango wa taifa wa kudhibiti magonjwa yaliyokua hayapewi kipaumbele katika Ukumbi wa Hotel ya Morena jijini Dodoma.

Waziri Ummy amesema ugonjwa wa Vikope unawapata watu wa jamii ya kimasikini hasa wafugaji na pia jamii yenye changamoto ya upatikanaji wa maji safi.

“Trachoma ni ugonjwa ambao kwa kiasi fulani unahusiana na umaskini na unawapata watu wa jamii ya wafugaji lakini pia wakiwa na changamoto ya upatikanaji wa maji”. Alisema Waziri Ummy.

Aidha, waziri Ummy amesema katika kipindi cha miaka mitano serikali imekua ikishirikiana na serikali ya Uingereza kupitia taasisi ya UK aid na Queen Elizabeth Diamond Jubilee Trust katika kuhakikisha wagonjwa wa Vikope wanafikiwa na kupata huduma za matibabu pamoja na kufanyiwa upasuaji kwa wale ambao wanakaribia kupata upofu.

Waziri Ummy amesema bado kuna changamoto ya maambukizi katika wilaya nane ambazo ni Mpwapwa, Chemba, Kalambo, Songwe, Ngorongoro, Longido, Kiteto, na Simanjiro.

Hata hivyo katika kipindi cha miaka mitano wagonjwa wa Trachoma waliofanyiwa upasuaji wamepungua kutoka 160,000 mwaka 2010 hadi wagonjwa 17,000 mpaka mwezi Oktoba 2018, ambapo inatajwa kuwa ni hatua kubwa katika mafanikio ya kukabiliana na maambukizi ya ugonjwa huu.

Waziri Ummy amesema serikali iko katika hatua nzuri ya kuhakikisha inatokomeza maambukizi mapya ya Trachoma kwa kuendelea kutoa dawa katika wilaya nane zilizotajwa na kuwafanyia upasuaji wagonjwa ambao wamefikia hatua ya kupata upofu.

Naye balozi wa Uingereza nchini Bi. Sarah Cooke amesema serikali ya Uingereza kupitia taasisi ya Queen Elizabeth Diamond Jubilee Trust na shirika la SightServers itaendelea kushirikiana na serikali ya Tanzania kusaidia kutokomeza ugonjwa wa Trachoma nchini.

MWISHO

0 on: "MAAMBUKIZI YA UGONJWA TRACHOMA YAPUNGUA KWA ASILIMIA 75 NCHINI"