Like us on Facebook

Inaendeshwa na Blogger.

Tafuta katika Blogu Hii

Kumbukumbu la Blogu

Instagram

visitors

display number of visitors

Popular Posts

Pages

Flickr Images

Alhamisi, 21 Februari 2019

UJENZI WA VIWANDA VYA DAWA KUOKOA MABILION YA SHILINGI NCHINI

Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu (Wapili kushoto)  akiongozana na Mkuu wa Wilaya ya Kibaha Mhe. Assumpter Mshama (wakwanza kushoto), pamoja na Wataaalamu wa masuala ya ujenzi, wakiendelea na ukaguzi wa kiwanda cha Dawa cha Kairuki Pharmaceutical Ltd katika Wilaya ya Kibaha Mkoa wa Pwani

Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu (Wapili kushoto) akimueleza jambo Mwekezaji wa Vista Pharmaceutical Ltd, wakati wa ziara ya kukagua Maendeleo ya ujenzi wa Viwanda vya Dawa katika unaoendelea katika Mkoa wa Pwani.

Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu akisistiza jambo, kulia kwake ni Mwekezaji  wa kiwanda cha dawa Vast Pharma Ltd.

Picha ya pamoja ikiongozwa na Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu baada ya ziara ya kutembelea Viwanda vya Dawa vya  Vista Pharma Ltd na Kairuki pharmaceutical Ltd vinavyojengwa katika Wilaya ya Kibaha Mkoa wa Pwani.

(Picha 1) Muonekano wa Kiwanda cha Kairuki Pharmaceutical Ltd na na Ofisi yake (Picha 2) unaoendelea kujengwa katika Wilaya ya Kibaha Mkoa wa Pwani.


UJENZI WA VIWANDA VYA DAWA KUOKOA MABILION YA SHILINGI NCHINI
Na WAMJW - PWANI

WAZIRI Wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu leo amefanya ziara ya kukagua Maendeleo ya ujenzi wa kiwanda vya Dawa cha Vista Pharma Ltd na Kairuki Pharmaceutical Ltd  vinavyoendelea kujengwa kwa kasi katika Mkoa wa Pwani.

Katika ziara hiyo Waziri Ummy alilenga kujionea na kutatua Changamoto zinazowakumba Wawekezaji nchini hususani katika Viwanda vya Dawa ili kuokoa kiasi kikubwa cha fedha kinachoendelea kupotea kutokana na kuagiza Dawa nje ya nchi.

Waziri Ummy amesema kuwa katika kila Shilingi 100 ambayo Serkkali inatumia kununua Dawa, Vifaa na Vifaa Tiba, Shilingi 94 inapotea nje ya nchi, ambapo kumalizika kwa Viwanda hivi kutasaidia pesa hiyo kubaki ndani ya nchi na kutumika katika shughuli nyingine za  Maendeleo kwa Wananchi. 

"Katika kila Shilingi 100 ambayo Serikali inatumia kununua Dawa, Vifaa na Vifaa Tiba, Shilingi 94 tunaipeleka nje ya nchi kununua Dawa, Vifaa na Vifaa Tiba, na ndiomaana nimefanya ziara hii pamoja na viongozi wa Mkoa na kutoka Wizara ya Viwanda na Biashara na Kituo cha uwekezaji ili kuokoa fedha hiyo inayopotea nje ya nchi" alisema Waziri Ummy.

Waziri Ummy aliendele kusema kuwa kumalizika kwa Viwanda hivi kutasaidia kwa kiasi kikubwa upatikanaji wa Dawa za kutosha na kwa bei rahisi, jambo litalosaidia kuimarika kwa huduma za Afya nchini.

 " Dawa kupatikana kwa wingi na kwa bei rahisi na kwa haraka zaidi, kwasababu kuagiza Dawa nje ya nchi MSD anatumia mpaka miezi 6  mpaka ifike Tanzania" alisema Waziri Ummy.

Aidha, Waziri Ummy amewaagiza Tanesco ndani ya Mkoa kuhakikisha wanaleta huduma ya umeme ndani ya wiki moja ili hatua za mwanzo za ufungaji wa mashine katika Viwanda hivyo uanze Mara moja. 

Pia, Waziri Ummy amewaagiza Mamlaka ya Maji Mkoani Mkoa wa Pwani kuhakikisha wanaleta huduma ya maji ndani ya Machi 15 katika eneo hilo la Viwanda ili kuharakisha shughuli za ujenzi.

Mbali na hayo, Waziri Ummy amewashukuru wawekezaji hao wa Ndani kwa maamuzi mazuri aliyochukua ya kuwekeza katika Viwanda vya Dawa ili kuisaidia Jamii ya Watanzania ambao Dawa bado imekuwa ni changamoto licha ya Jitihada kubwa zinazofanywa na Serikali katika kukabikiana na changamoto hiyo.

#TunaboreshaAfya

1 on: "UJENZI WA VIWANDA VYA DAWA KUOKOA MABILION YA SHILINGI NCHINI"
  1. A completely new and crisp feel with fiery letters and lovable flames that pop up lifeless of night|at 메리트카지노 midnight} background. This elegant theme in dark colours is soothing to the eyes, and the color selection units the temper for a fiendishly fun time. You can log in and utilize the bank button to make your preliminary deposit after your account has been reconciled.

    JibuFuta