Like us on Facebook

Inaendeshwa na Blogger.

Tafuta katika Blogu Hii

Kumbukumbu la Blogu

Instagram

visitors

display number of visitors

Popular Posts

Pages

Flickr Images

Ijumaa, 17 Novemba 2017

SERIKALI YAPOKEA MSAADA WA VIFAA VYA KUFUNDISHIA WATOA HUDUMA ZA WATOTO NJITI NA WAMJW-DAR ES SALAAM

 Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya, Maendeleo ya jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Mpoki Ulisubisya akipokea vifaa vya kufundishia kutoka kwa Balozi wa Shirikisho la Jamhuri ya Ujerumani  Dr Detlef Wachter katika maazimisho ya siku ya mtoto njiti duniani inayoazimishwa kila Novemba 17.

 Picha ya pamoja ikiongozwa na Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya, Maendeleo ya jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Mpoki Ulisubisya katika maazimisho ya siku ya mtoto njiti duniani, ambapo shirika la GIZ kutoka Ujerumani lillikabidhi vifaa vya kufundishia watoa huduma jinsi ya kuwasaidia watoto njiti.

Mganga Mkuu wa Mkoa wa Mtwara Dtk. Wedson Sichalwe akiwasilisha taarifa fupi mbele ya Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya, Viongozi  na waandishi wa habari(hawapo kwenye picha) katika maazimisho ya siku ya mtoto njiti duniani.

 Meneja mipango wa Shirika la Giz kutoka Ujerumani  Dkt. Susanne Grimm akielezea baadhi ya mafanikio na mipango ya Shirika hilo wakati wakitoa msaada wa vifaa vya kufundishia watoa huduma jinsi ya kuwasaidia watoto njiti.

 Balozi wa Shirikisho la Jamhuri ya Ujerumani  Dr Detlef Wachter akitoa taarifa mbele ya mgeni rasmi na waandishi wa habari wakati  wa utoaji msaada uliofanywa na shirika la Giz katika Taasisi ya Saratani Ocean road jijini Dar es salaam, mgeni rasmi alikuwa Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya Dkt. Mpoki Ulisubisya.

 Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya  Dkt. Mpoki Ulisubisya akimpa mkono wa shukurani  Balozi wa Shirikisho la Jamhuri ya Ujerumani  Dr Detlef Wachter baada ya kupokea msaada wa vifaa vya kufundishia watoa huduma jinsi ya kuwasaidia watoto njiti.

Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya  Dkt. Mpoki Ulisubisya akifungua mkutano katika maazimisho ya siku ya mtoto njiti duniani, ambapo shirika la GIZ kutoka Ujerumani lillikabidhi vifaa vya kufundishia watoa huduma jinsi ya kuwasaidia watoto njiti.



 Na WAMJWW

SERIKALI kupitia Wizara ya Afya imepokea msaada wa vifaa vya kufundishia watoa huduma kwa watoto njiti vyenye thamani ya shilingi milioni 22. 19 kutoka shirika lisilo la kiserikali GIZ la Ujerumani ili kuweza kutoa huduma bora  katika kuwakuza watoto hao kwa uangalifu wa hali ya juu na kwenye mazingira mazuri.
Akizungumza wakati wa maadhimisho ya Siku ya mtoto njiti duniani yaliyofanyika katika Taasisi ya Saratani Ocean Road Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya Dkt. Mpoki Ulisubisya amesema msaada wa vifaa hivyo utaboresha huduma kwa watoto njiti.
“Kutokana na msaada wa vifaa hivyo naamini rufaa zitapungua kwa kiasi kikubwa na kufanya huduma hizo kutolewa kwenye zahanati zitazopelekewa vifaa hivyo “ alisema Dkt. Ulisubisya.
Aidha Dkt. Ulisubisya amesema kuwa watumishi wa afya ambao wamepata mafunzo wanatakiwa kuwaangalia wamama wanaotaka kujifungua ili kuweza kupunguza vifo vya wamama wajawazito na watoto nchini.
Mbali na hayo Dkt. Ulisubisya amesema kuwa wamama wajawazito wanatakiwa kuhudhuria kliniki mara kwa mara pindi wanapopata ujauzito ili kuweza kupata ushauri kutoka kwa wataalamu wa afya ili kuepuka kuzaa watoto njiti.
Kwa upande wake Mganga Mkuu wa Mkoa wa Mtwara Dkt. Wedson Sichalwe amesema kuwa anashukuru Shirika la GIZ kwa mafunzo pamoja na vifaa vya kutolea huduma kwa watoto njiti katika mkoa wake ili kutoa huduma bora kwa watoto hao.
“Tumepata msaada mkubwa sana kwa mkoa wetu kwani tulikua tunakabiliwa na changamoto za vifaa vya vya kuhudumia watoto njiti wanaozaliwa katika zahanati na hospitali mkoani kwetu” alisema Dkt. Sichalwe.

0 on: "SERIKALI YAPOKEA MSAADA WA VIFAA VYA KUFUNDISHIA WATOA HUDUMA ZA WATOTO NJITI NA WAMJW-DAR ES SALAAM"