Like us on Facebook

Inaendeshwa na Blogger.

Tafuta katika Blogu Hii

Kumbukumbu la Blogu

Instagram

visitors

display number of visitors

Popular Posts

Pages

Flickr Images

Ijumaa, 3 Novemba 2017

TFDA IMETAKIWA KUBORESHA UDHIBITI WA UINGIZAJI WA VYAKULA NA DAWA KIHOLELA





Na WAMJWW
Mamlaka ya Chakula , Dawa na Vipodozi TFDA imetakiwa kuboresha udhibiti wa uingizaji wa  Dawa, Vipodozi na Chakula nchini  kiholela ili kulinda afya ya Watanzania .
Hayo yamesemwa  na Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Faustine Ndugulile wakati wa kuzindua CHETI CHA MFUMO WA UHAKIKI UBORA WA HUDUMA KATIKA KIWANGO CHA KIMATAIFA CHA ISO 9001-2015 leo jijini Dar es Salaam.
“Dawa ni kitu nyeti sana, hatuwezi kuruhusu dawa feki kuingia nchini, mnafanya kazi nzuri sana katika nyanja hii  na muendelee na mpango huu ili kudhibiti uingizaji wa vyakula visivyokidhi viwango na mahitaji ya watanzania, ” alisema Dkt.  Ndugulile.
Aidha Dkt. Ndugulile amesema kuwa TFDA wanatakiwa kuzingatia muongozo wa kupitisha vyakula na vipodozi kwenye mipaka ya nchi kwa kuzingatia ubora na viwango vilivyoweka katika kudhibiti uingizaji mbovu wa vyakula.
Kwa upande wake Mkurugenzi Mkuu wa TFDA Bw. Hiiti Silo amesema kuwa ili kuendelea kukidhi matakwa ya wateja na mahitaji yao wameamua kuendana na kiwango cha kimataifa na kuwaita ISO kuja kuhakiki ambapo wamefanikiwa kukidhi na kupata cheti.
“Shirika la Viwango la Kimataifa ISO limehakiki ubora wa huduma zetu katika kukidhi mahitaji na matakwa ya watumiaji wa huduma zetu na kutupatia cheti kinachoturuhusu kutoa huduma nchini” alisema Bw. Silo.
Aidha Bw. Silo amesema kuwa wapo bega kwa bega na Serikali ya awamu ya tano ianyoongozwa na Rais Dkt. John pombe Magufuli katika kusogeza mbele gurudumu la afya hapa nchini kupitia taasisi  ya TFDA.

0 on: "TFDA IMETAKIWA KUBORESHA UDHIBITI WA UINGIZAJI WA VYAKULA NA DAWA KIHOLELA"