Like us on Facebook

Inaendeshwa na Blogger.

Tafuta katika Blogu Hii

Kumbukumbu la Blogu

Instagram

visitors

display number of visitors

Popular Posts

Pages

Flickr Images

Jumatatu, 27 Novemba 2017

TAHADHARI YA MATAPELI




AMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA
WIZARA YA AFYA, MAENDELEO YA JAMII, JINSIA, WAZEE NA WATOTO
  

TAARIFA KWA UMMA
TAHADHARI YA MATAPELI

Wizara ya Afya,Maendeleo ya Jamii, Jinsia,Wazee na Watoto inapenda kuutahadharisha Umma dhidi ya matapeli wanaopita maeneo mbali mbali wakiwaeleza watu kwamba wanauwezo wa kuwapatia Ajira za Afya, huku wakiwataka kutoa rushwa, kitu ambacho si kweli na ni kinyume na sheria na taratibu za nchi. Katika watu hao kuna mtu anayetumia jina la Godfrey Nyami  anaejifanya ni mtumishi wa Idara ya Utawala Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto na huchukua fedha kiasi cha shilingi 100,000/ kwa ahadi ya kuwapatia kazi.
Kama kuna mtu yoyote anafanya hivyo na unamfahamu tafadhari  toa taarifa katika vyombo vya dola, kwani kufanya hivyo ni kosa kisheria na hatua kali zitachukuliwa.

Imetolewa na ,

Kitengo cha Mawasiliano Serikalini-Afya
27/11/2017.

0 on: "TAHADHARI YA MATAPELI"