Like us on Facebook

Inaendeshwa na Blogger.

Tafuta katika Blogu Hii

Kumbukumbu la Blogu

Instagram

visitors

display number of visitors

Popular Posts

Pages

Flickr Images

Jumatatu, 14 Januari 2019

DKT. ZAINAB ATINGA OFISI KUU, WIZARA YA AFYA JIJINI DODOMA

Katibu Mkuu Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Zainab Chaula (Wakulia) akipokea nyaraka za makabidhiano kutoka kwa aliyekuwa Katibu Mkuu wa Wizara hiyo Dkt. Ulisubisya Mpoki leo katika Ofisi Kuu za Wizara ya Afya jijini Dodoma.

Katibu Mkuu Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Zainab Chaula (Wakulia) akiteta jambo na aliyekuwa Katibu Mkuu wa Wizara hiyo Dkt. Mpoki Ulisubisya leo katika Ofisi Kuu za Wizara ya Afya jijini Dodoma, katika kikao na Wakurugenzi, Wakuu wa Vitengo na Wakuu wa Idara Wizara ya Afya.

Kikao chaWakurugenzi, Wakuu wa Vitengo na Wakuu wa Idara Wizara ya Afya kikiongozwa na aliyekuwa Katibu Mkuu Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Mpoki Ulisubisya wakati wakimpokea Katibu Mkuu mpya Dkt. Zainab Chaula leo katika Ofisi Kuu za Wizara ya Afya jijini Dodoma,

Aliyekuwa Katibu Mkuu Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Mpoki Ulisubisya akiteta jambo na Mganga Mkuu wa Serikali Prof. Bakar Kambi baada ya Kikao cha kumkaribisha Katibu Mkuu Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Zainab Chaula.

Katibu Mkuu Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Zainab Chaula (Wakwanza Kushoto) akibadilishana mawazo na  Aliyekuwa Katibu Mkuu Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Mpoki Ulisubisya (Watatu kulia) pamoja na Mganga Mkuu wa Serikali Prof. Bakar Kambi.

Picha ya Pamoja ikiongozwa na Katibu Mkuu Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Zainab Chaula, Aliyekuwa Katibu Mkuu Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Mpoki Ulisubisya, Naibu Katibu Mkuu Afya TAMISEMI Dkt. Dorothy Gwajima na Mganga Mkuu wa Serikali Prof. Bakar Kambi, pamoja na Wakurugenzi, Wakuu wa Vitengo na Wakuu wa Idara Wizara ya Afya baada ya kikao kifupi cha ukaribisho wa Dkt. Chaula.

Katibu Mkuu Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Zainab Chaula, akiwaonesha namna ya ufuatiliaji ili kuboresha Ujenzi wa Mji mpya wa Serikali Ihumwa wakati alipotembelea ujenzi wa TAMISEMI ili kujifunza, Wakwanza kushoto ni Naibu Katibu Mkuu Afya TAMISEMI Dkt. Dorothy Gwajima, anaefuata ni Mganga Mkuu wa Serikali Prof. Bakar Kambi na Aliyekuwa Katibu Mkuu Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Mpoki Ulisubisya.
Katibu Mkuu Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Zainab Chaula akiteta jambo na Mganga Mkuu wa Serikali Prof. Bakar Kambi pamoja na Mkurugenzi wa Sera na Mipango Bw. Mbanga.

Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt.Faustine Ndugulile akimsikiliza kwa makini Katibu Mkuu Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Zainab Chaula pindi walipokutana kwenye ziara ya kutembelea ujenzi wa Wizara ya Afya katika Mji mpya wa Serikali Ihumwa, jijini Dodoma.

Ujenzi wa Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto ukiendelea kwa kasi katika Mji mpya wa Serikali Ihumwa, jijini Dodoma.

DKT. ZAINAB ATINGA OFISI KUU, WIZARA YA AFYA JIJINI DODOMA.

Na WAMJW - DODOMA
KATIBU Mkuu Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto-Idara kuu Afya Dkt. Zainab Chaula leo amekutana na Wakurugenzi wa idara na  Wakuu wa Vitengo wa wizara hiyo tangu alipoapishwa siku chache kushika nafasi hiyo, akitokea TAMISEMI.

Katika kikao hicho Dkt. Chaula amemshukuru Mhe. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli kwa kuendelea kumuamini na kumpa nafasi hiyo, huku akihimiza kila mmoja kufanya kazi kwa ushirikiano na kwa weledi ili kulinda taaluma zao. "Tujiandae kufanya kazi kama timu moja katika kutekeleza sera na miongozo ya sekta ya afya na kuhakikisha dhamana tuliyopewa tunaitumikia kadri inavyowezekana".Alisisitiza Dkt.Chaula

Hata hivyo Dkt.Chaula alimshukuru Katibu Mkuu aliyeondoka Dkt.Mpoki Ulisubisya kwa mifumo mizuri aliyoiweka na kuahidi kuendeleza kwa kuanza na changamoto zilizopo.

Aidha,aliwataka wakurugenzi hao kutimiza majukumu yao kwa kufanya kazi kwa kujituma, huku akiwatoa hofu kuwa ofisi yake iko wazi muda wote na yeyote mwenye wazo zuri la kujenga asisite kumuona, kwani lengo ni kuboresha Sekta ya Afya

"uwezo wa kufanya kazi tunao hivyo.mabadiliko ni vitendo, tufanye kazi kwa matokeo". Alisema Dkt. Chaula 

Wakati huo huo, Katibu Mkuu Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Zainab Chaula ametembelea ujenzi wa mji mpya wa Serikali Ihumwa na kujionea maendeleo ya ujenzi wa Wizara ya Afya.

0 on: "DKT. ZAINAB ATINGA OFISI KUU, WIZARA YA AFYA JIJINI DODOMA"