Like us on Facebook

Inaendeshwa na Blogger.

Tafuta katika Blogu Hii

Kumbukumbu la Blogu

Instagram

visitors

display number of visitors

Popular Posts

Pages

Flickr Images

Jumamosi, 26 Januari 2019

5. HALI YA HUDUMA ZA AFYA NCHINI KATIKA KIPINDI CHA MWAKA 2018

Naibu Waziri wa Afya, ,Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Faustine Ndugulile akikagua vifaa vya kupima ugonjwa wa Ebola pindi alipotembelea uwanja wa ndege wa Mwalimu Nyerere jijini Dar Es Salaam.

5. Magonjwa ya Mlipuko

#Tanzania imeendelea kuwa salama licha ya tishio la kuwepo kwa Ugonjwa wa Ebola katika Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo.

#Wizara imechukua tahadhari za kulinda mipaka yake. Hivyo, hakukuwa na mgonjwa yeyote aliyegundulika kuwa na Ebola nchini kwa mwaka 2017 na 2018.

#Aidha, Serikali imeendelea na mapambano dhidi ya ugonjwa wa Kipindupindu ambapo Mwaka 2018 kulikuwa na wagonjwa 4,706 na vifo 84 ikilinganishwa na wagonjwa 4,626 na vifo 93 mwaka 2017.

#Ugonjwa wa Dengue watu 226 waliathirika mwaka 2018 ikilinganishwa na watu 65 mwaka 2017. Hakuna kifo kilichosababishwa na ugonjwa huu.

#Vilevile kulikuwa na wagonjwa 6 wa Chikungunya ambao walipatiwa matibabu mwaka 2018 na hakuna kifo kilichotokea.

Imetolewa na;
Wizara ya Afya,Maendeleo ya Jamii,Jinsia,Wazee na Watoto
26/01/2019

0 on: " 5. HALI YA HUDUMA ZA AFYA NCHINI KATIKA KIPINDI CHA MWAKA 2018"