Like us on Facebook

Inaendeshwa na Blogger.

Tafuta katika Blogu Hii

Kumbukumbu la Blogu

Instagram

visitors

display number of visitors

Popular Posts

Pages

Flickr Images

Jumanne, 22 Januari 2019

HALI YA HUDUMA ZA AFYA NCHINI KATIKA KIPINDI CHA MWAKA 2018

 
 
HALI YA HUDUMA ZA AFYA NCHINI KATIKA KIPINDI CHA MWAKA 2018

1. Afya ya Uzazi,Mama na Mtoto

#Katika mwaka 2018, jumla ya wajawazito 2,086,930 walihudhuria na kuandikishwa kliniki, ikilinganishwa na wajawazito 2,009,879 mwaka 2017. Mwongozo wa utoaji huduma za afya ya uzazi na mtoto unaelekeza wajawazito kuanza huduma mapema kabla ya majuma 12 ya ujauzito na kuhudhuria kliniki angalau mara nne katika kipindi cha ujauzito ili waweze kupata huduma zote muhimu.

#Asilimia 25 ya wajawazito nchini waliweza kufanya *hudhurio la kwanza kliniki kabla ya majuma 12* ikillinganishwa na asilimia 18 mwaka 2017.

#Ongezeko la *wajawazito kujifungulia katika vituo vya kutolea huduma za afya* Mwaka 2018 asilimia 73 ya wajawazito walijifungulia katika vituo vya kutolea huduma za afya ikilinganishwa na asilimia 70 mwaka 2017.

#Huduma ya *kuzuia maambukizi ya VVU kutoka kwa mama kwenda kwa mtoto* imeendelea kutolewa ambapo mwaka 2018 asilimia 97 ya wajawazito walipima VVU ikilinganishwa na asilimia 95 mwaka 2017. 

#Katika wajawazito waliopima VVU, asilimia 3.9 waligundulika kuwa na VVU na kati ya hao waliogundulika asilimia 99 walianzishiwa dawa za ART. Katika mwaka 2017, Asilimia 4.2 ya wajawazito waligundulika kuwa na maambukizi ya VVU na kati yao asilimia 99 walianza dawa za ART. 

#Hali ya upatikanaji wa chanjo kwa watoto nchini imeendelea kuwa katika kiwango cha juu kwa asilimia 85 katika kipindi cha mwaka 2018 na mwaka 2017

Imetolewa na ;
Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii,Jinsia,Wazee na Watoto
Chanzo: District Health Information System 2 (DHIS2).

0 on: "HALI YA HUDUMA ZA AFYA NCHINI KATIKA KIPINDI CHA MWAKA 2018"