Like us on Facebook

Inaendeshwa na Blogger.

Tafuta katika Blogu Hii

Kumbukumbu la Blogu

Instagram

visitors

display number of visitors

Popular Posts

Pages

Flickr Images

Jumanne, 22 Januari 2019

TBA WAPEWA WIKI MBILI KUPELEKA FEDHA ZA UJENZI WA HOSPITALI YA RUFAA YA MKOA WA SIMIYU

Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu akitoa maelekezo kwa Injini mkuu wa TBA Simiyu Bw. Likimaitare Naunga wakati akipotembelea ujenzi wa Hospitali ya Rufaa ya mkoa wa Simiyu. Kulia ni Mkuu wa mkoa huo Bw. Anthony Mtaka.

Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu akimsalimia ndugu wa mgonjwa aliyelazwa (jina halijafahamika) katika hospitali teule ya Somanda alipotembelea hospitali kuona hali ya utaoaji huduma za afya. Kulia ni Mwenyekiti wa CCM wilaya Bi. Juliana Mahongo na Daktari zamu.

Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu akisisitiza jambo wakati alipotembelea wodi za Hospitali ya rufaa ya mkoa wa Simiyu. Kushoto ni Mganga Mkuu wa mkoa Dkt. Mageda Kihulya, Mbunge wa bunge la Afrika Mashariki Bi. Happines Lugiko na Mkuu wa Mkoa wa Simiyu Bw. Anthony Mtaka.




Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu akitembelea ujenzi wa jengo la uchunguzi na mama na mtoto katika Hospitali ya Rufaa ya mkoa wa Simiyu. Waliongozana nae ni viongozi waandamizi wa mkoa wakiongozwa na Mkuu wa mkoa huo Anthony Mtaka.



TBA WAPEWA WIKI MBILI KUPELEKA FEDHA ZA UJENZI WA HOSPITALI YA RUFAA YA MKOA WA SIMIYU


Na WAMJW-SIMIYU

Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu ameiagiza wakala wa ujenzi (TBA) kupeleka fedha za ujenzi zilizotolewa na Serikali katika ujenzi wa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Simiyu kuhakikisha zinafika ndani ya wiki mbili.

Agizo hilo limetolewa  leo wakati alipotembelea ujenzi wa jengo la Uchunguzi na jengo la Mama na Mtoto na kutoridhishwa na kasi ya ujenzi huo huku sababu kubwa inayopelekea kusuasua ikitajwa  ni fedha kidogo zilizopokelewa na wakala wa ujenzi wa mkoa wa Simiyu kiasi cha Shilingi Milioni 430 wakati serikali imetoa Bilioni 1.064 kwa ajili ya ujenzi huo.

“Ninawashngaa TBA kwanini wanakaa na fedha wakati wanajua mradi wa ujenzi unaendelea huku, serikali imetoa Bilioni 1.064 ili zitumike katika ujenzi wa Hospitali hii lakini TBA wameleta milioni 430 tu, hizo fedha zingine ziko wapi?”. Alihoji waziri Ummy.

Kufuatia hali hiyo Waziri Ummy ameahidi kushughulikia suala hilo na kuahidi fedha hizo zitafika katika mradi huo ndani ya wiki mbili ili ziweze kusaidia kuongeza kasi ya ujenzi wa majengo hayo ambapo yanatarajiwa kukabidhiwa na kuanza kutoa huduma kuanzia mwezi Juni mwaka huu.

Kwa upande wake Injinia mkuu wa TBA anayesimamia ujenzi huo Bw. Likimaitare Naunga amesema fedha zilizoletwa katika mradi huo hazitoshi na ndiyo sababu kubwa inayochangia kusuasua kwa mradi huo huku akitaka wakala wa ujenzi (TBA) kuhakikisha fedha hizo zinafika mapema ili zisaidie kuongeza kasi ya mradi na kufikia lengo.

Naye Mkuu wa Mkoa wa Simiyu Bw. Anthony Mtaka amemuahidi Waziri Ummy kuwa atasimamia kwa karibu upatikanaji wa fedha hizo zilizopo TBA zinafika katika mradi na kuhakikisha mradi unakamilika ndani ya muda uliopangwa ili huduma muhimu za kibingwa zianze kutolewa Hopitalini hapo.

Wakati huo huo waziri Ummy ametembelea Hospitali teule ya Somanda iliyopo wilayani Bariadi na kuonekana kutoridhishwa na huduma zinazotolewa katika jengo la Mama na Mtoto ambapo alishuhudia huduma mbaya zinazotolewa kwa akinamama wajawazito na watoto wachanga.

Pia Waziri Ummy ameshangazwa baada ya kuona hakuna chumba cha kuhifadhia watoto wenye uhitaji wa huduma maalum kama huduma za joto kwa watoto waliozaliwa kabla ya muda (Njiti) na kuitaka Hospitali hiyo kuwa na chumba hicho muhimu.

Aidha, Waziri Ummy ameshangazwa na kutokuwepo kwa huduma za upasuaji katika jengo hilo huku sababu ikitajwa kutokuwepo kwa Sinki, hali inayosababisha usumbufu mkubwa kwa akinamama wajawazito wanaofika kupata huduma hospitalini hapo.

Kufuatia hali hiyo waziri huyo ametoa siku tatu kwa uongozi wa Hospitali hiyo chini ya Mganga Mkuu wa Mkoa Dkt. Mageda Kihulya kuhakikisha wananunua sinki hilo na huduma za upasuaji zianze kutolewa mara moja katika jengo hilo.

Waziri Ummy yupo Mkoani hapa katika  ziara  ya kikazi ya kutembelea mikoa ya Simiyu, Geita na Shinyanga ili kuweza kuona hali ya miundombinu na utoaji huduma katika hospitali za rufaa za mikoa.

0 on: "TBA WAPEWA WIKI MBILI KUPELEKA FEDHA ZA UJENZI WA HOSPITALI YA RUFAA YA MKOA WA SIMIYU"