Like us on Facebook

Inaendeshwa na Blogger.

Tafuta katika Blogu Hii

Kumbukumbu la Blogu

Instagram

visitors

display number of visitors

Popular Posts

Pages

Flickr Images

Jumamosi, 5 Januari 2019

SERIKALI YAAHIDI KUTOA GARI LA KUBEBEA WAGONJWA KATIKA HOSPITALI YA RUFAA YA MKOA RUVUM

Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Faustine Ndugulile akikagua hali ya upatikanaji wa Dawa kwenye chumba cha kuhifadhia Dawa katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Ruvuma.

Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. faustine akimjulia hali mtoto aliyepelekwa kupata matibabu katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Ruvuma, ikiwa ni ziara yake ya kukagua ubora wa huduma za Afya katika Hospitali hiyo.

Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Faustine Ndugulile akikagua miguu bandia katika chumba cha kuhifadhia vifaa mbali mbali vya Hospitali, ikiwa ni ziara yake ya kukagua ubora wa huduma za Afya katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Ruvuma.


 Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. faustine Ndugulile akikagua Dawa alizoandikiwa mgonjwa katika Wodi ya wanawake katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Ruvuma, ikiwa ni ziara yake ya kukagua ubora wa huduma za Afya katika Hospitali hiyo. Kulia kwake ni Mkurugenzi wa Tiba kutoka Wizara ya Afya Dkt. Dorothy Gwajima
Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. faustine Ndugulile akikagua karatasi ya idadi ya wagonjwa waliofika kupata matibabu katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Ruvuma, ikiwa ni ziara yake ya kukagua ubora wa huduma za Afya katika Hospitali hiyo.


Na WAMJW - SONGEA

Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Faustine Ndugulile ametembelea Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Ruvuma, akiwa katika ziara ya kukagua hali ya utoaji huduma za Afya bora kwa Wananchi.

Katika ziara hiyo Dkt. Ndugulile ameuagiza uongozi wa Hospitali hiyo kuhakikisha vifaa vyote vilivyoharibika vinatengenezwa na kuanza kufanya kazi mara moja.

Kwa upande mwingine ameutaka uongozi wa Hospitali hiyo kuhakikisha wanatumia Fedha vizuri katika kufanya maboresho ya majengo ya Hospitali hiyo, ikiwemo kutumia Forced account katika ujenzi huo.

Pia, Dkt. Ndugulile ameuagiza uongozi wa Hospitali hiyo kuhakikisha kila mtoa huduma za Afya anaandika muda kwa usahihi aliomuhudumia mgonjwa kuanzia anapopokelewa, anapofanyiwa matibabu mpaka anapoandikiwa dawa jambo litalorahisisha kubaini mtenda kosa endapo mgonjwa atapata tatizo.

Aidha, Serikali imeahidi kuwapa gari la kubebea wagonjwa katika  Hospitali hiyo ili kupunguza vifo vinavyoweza kuzuilika endapo gari hilo litakuwepo ikiwemo vifo vya mama na mtoto.

Mbali Na hayo Dkt. Ndugulile amewapongeza Watoa Huduma za Afya katika Hospitali hiyo kwa kazi nzuri wanayofanya huku akiwatia moyo kuwa Serikali inafahamu mchango wao na itaendelea kuboresha mahitaji yao.

#TunaboreshaAfya

0 on: "SERIKALI YAAHIDI KUTOA GARI LA KUBEBEA WAGONJWA KATIKA HOSPITALI YA RUFAA YA MKOA RUVUM"