Like us on Facebook

Inaendeshwa na Blogger.

Tafuta katika Blogu Hii

Kumbukumbu la Blogu

Instagram

visitors

display number of visitors

Popular Posts

Pages

Flickr Images

Jumapili, 20 Januari 2019

SERIKALI YAIONGEZEA UWEZO JKCI





Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu akisisitiza jambo wakati alipofanya ziara ya kukagua maendeleo ya ujenzi wa jengo la watoto wenye magonjwa ya moyo katika Taasisi ya Moyo ya JKCI jijini Dar es salaam.

Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu akimjulia hali mtoto wakati alipofanya ziara ya kukagua maendeleo ya ujenzi wa jengo la watoto wenye magonjwa ya moyo katika Taasisi ya Moyo ya JKCI jijini Dar es salaam.



Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu akimjulia hali mtoto aliyefika kupata matibabu katika Taasisi ya Moyo JKCI wakati alipofanya ziara ya kukagua maendeleo ya ujenzi wa jengo la watoto wenye magonjwa ya moy.



SERIKALI YAIONGEZEA UWEZO JKCI

Na WAMJW-DSM

SERIKALI kupitia Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto imeiongezea uwezo wa kutoa huduma Taasisi ya Moyo ya JKCI kwa kuimarisha jengo la watoto wenye magonjwa ya moyo ambalo litakuwa na uwezo wa kubeba vitanda 32 kutoka vitanda 11 hapo mwanzo.

Ameyasema hayo Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu leo alipofanya ziara ya kukagua maendeleo ya ukarabati na ujenzi wa jengo la watoto wenye magonjwa ya moyo katika Taasisi ya Moyo ya JKCI jijini Dar es salaam.

“Katika jengo hili kulikuwa na msongamano mkubwa sana wa watoto, sasa hivi jengo hili likikamilika litakuwa na vitanda 32 kutoka vitanda 11, hivyo kulifanya jengo hilo kuwa na vitanda vya watoto tu” alisema Waziri Ummy.

Waziri Ummy amesema kuwa katika jengo hilo kutakuwa na Vyumba maalumu kwaajili ya Wagonjwa wanaohitaji huduma na uangalizi maalumu 15 (ICU) kwaajili ya watoto tu,  badala ya rika zote kupata huduma hiyo katika chumba kimoja, kama ilivyokuwa hapo mwanzo, jambo litalosaidia kuokoa maisha ya watoto wanaohitaji uangalizi maalum.

“kutakuwa na Vyumba maalumu kwaajili ya Wagonjwa wanaohitaji huduma na uangalizi maalumu 15 kwaajili ya watoto tu,  maana yake tutakuwa tumeokoa maisha ya watoto ambao wanahitaji uangalizi maalumu, kwasababu watoto wanaweza wakawa wanahitaji vyumba vya uangalizi maalumu lakini vyumba hivyo vikawa vimetumiwa na wakubwa” alisema Waziri Ummy.

Waziri ummy aliendelea kusema kuwa kutokana na ufinyu wa nafasi JKCI wanauwezo wa kuafanya upasuaji kwa watoto 20 kwa mwezi, hivyo kwa uwezo huu ambao umejengwa na Serikali kuu kwa kushirikiana na wafadhili Charity Baptism wataweza kufanya upasuaji kwa watoto 40 kwa mwezi kutoka watoto 20.

“Kutokana na ufinyu wa nafasi JKCI ilikuwa na uwezo wa kufanya upasuaji kwa watoto 20,  lakini kwa uwezo huu ambao tumeweza kujengewa na Serikali kuu kwa kushirikiana na wafadhili Charity Baptism wataweza kufanya upasuaji kwa watoto 40 kwa mwezi kutoka watoto 20” alisema Waziri Ummy.


Aidha, Waziri Ummy amemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli kwa kuhidhinisha kiasi cha Shilingi 500 milioni kwa ajili ya kukamilisha ujenzi huo ifikapo Januari 28.

Waziri Ummy aliendelea kusema kuwa, kitengo hicho kinachotarajiwa kukamilika mwishoni mwa mwezi huu, kimegharimu Sh2 bilioni ambazo fedha zingine Sh800 milioni zimetolewa na wafadhili Charity Baptism.

Mbali na hayo Waziri Ummy amewaagiza Waganga Wakuu wa Hospitali zote na Vituo vya Afya kujiongeza kwa kufanya maendeleo yao wenyewe kwa wadau mbali mbali wa masuala ya Afya badala yakusubili kila kitu kufanyiwa na Serikali.

Kwa upande mwingine Waziri Ummy amesema mwaka 2018 JKCI ilifanya  oparesheni nyingi zaidi kwa watoto hivyo anategemea mwaka huu zitaongezeka zaidi, “Hii itakuwa wodi ya kwanza kwa ajili ya watoto pekee kwa Afrika Mashariki walio wengi wanachanganya watoto na wakubwa.”

Mkurugenzi Mtendaji JKCI Profesa Mohamed Janabi amesema kitengo hicho kipya kilichoanzishwa pembeni mwa jengo hilo kitakuwa na vitanda 32 kutoka 11 vya awali.

“Watoto walikuwa na vitanda 11 pekee lakini kwa sasa tutakuwa navyo 32 na vitanda vya ICU vitakuwa 15,” amesema Profesa Janabi

MWISHO.

0 on: "SERIKALI YAIONGEZEA UWEZO JKCI"