Like us on Facebook

Inaendeshwa na Blogger.

Tafuta katika Blogu Hii

Kumbukumbu la Blogu

Instagram

visitors

display number of visitors

Popular Posts

Pages

Flickr Images

Jumatano, 23 Januari 2019

HALI YA HUDUMA ZA TIBA NCHINI KATIKA KIPINDI CHA MWAKA 2018


Jengo la wagonjwa wa dharura katika Hospitali ya Rufaa Kanda ya Kaskazini KCMC.

Mwaka 2018 jumla ya mahudhurio ya wagonjwa ilikuwa 42,411,276 katika vituo vya kutolea huduma za tiba nchini ikilinganishwa na 54,478,926 kwa mwaka 2017 Kati ya hao wagonjwa wa wa nje (OPD) ilikuwa 41,052,012 na wagonjwa wa kulazwa (IPD) ilikuwa 1,359,264.

1. Wagonjwa waliohudumiwa katika Hospitali za Halmashauri, Vituo vya Afya na Zahanati katika ngazi ya msingi.
Ø Katika mwaka 2018 jumla ya wagonjwa wa nje (OPD) ilikuwa 36,376,967 walipatiwa huduma katika hospitali za Halmashauri, hospitali nyingine, vituo vya afya na zahanati ikiwa ni 18,194,619 hudhurio la kwanza na 18,182,348 mahudhurio ya marudio. Mwaka 2017, jumla ya wagonjwa wa nje (OPD) ilikuwa 47,650,158 ambapo 30,174,341 hudhurio la kwanza na 15,809,971 mahudhurio ya marudio.
Wakati huo huo wagonjwa wa Kulazwa mwaka 2018 walikuwa 404,659 ikilinganishwa na wagonjwa 523,587 mwaka 2017

2. Wagonjwa waliohudumiwa katika Hospitali za Rufaa za Mikoa mwaka 2018
Ø Kwa kipindi cha Januari hadi Desemba 2018 Hospitali za Rufaa za Mikoa zilihudumia jumla ya wagonjwa 3,526,503 ambapo wagonjwa wa nje walikuwa 3,054,318 na wagonjwa wa ndani walikuwa 472,185 ikilinganishwa na wagonjwa 4,781,999 waliohudumiwa kwa kipindi cha Januari hadi Desemba 2017.

3. Mahudhurio ya wagonjwa katika Hospitali ya Taifa, Hospitali Maalum na Hospitali za Rufaa za Kanda
Ø Katika kipindi cha Januari hadi Desemba 2018, Hospitali hizi zilihudumia jumla ya wagonjwa   2,103,147 ambapo wagonjwa wa kulazwa walikuwa 482,420 na wagonjwa wa nje walikuwa 1,620,727. Ikilinganishwa na idadi ya wangonjwa 2,046,769 kwa kipindi cha Januari hadi Desemba 2017. Ambapo idadi ya wagonjwa wa kulazwa ilikuwa 711,766 na wagonjwa wa nje 1,335,003. 


Imetolewa na;
Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto.

0 on: "HALI YA HUDUMA ZA TIBA NCHINI KATIKA KIPINDI CHA MWAKA 2018"