Like us on Facebook

Inaendeshwa na Blogger.

Tafuta katika Blogu Hii

Kumbukumbu la Blogu

Instagram

visitors

display number of visitors

Popular Posts

Pages

Flickr Images

Ijumaa, 24 Novemba 2017

UPASUAJI WA KIHISTORIA WA UPANDIKIZAJI WA FIGO WAFANYIKA.

 Waziri wa Afya, Maendeleo ya jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Ummy Mwalimu akisisitiza jambo mbele ya jopo la madaktari bingwa wa Upasuaji wa upandikizaji wa figo kutoka Tanzania na India pamoja na Waandishi wa habari (hawapo kwenye picha), katika uzinduzi rasmi wa huduma za upasuaji wa upandikizaji wa figo uliofanyika katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili.

 
 Madaktari  Bingwa kutoka Hospitali ya Taifa ya Muhimbili  walioshiriki katika Upasuaji wa upandikizaji wa figo kwa kushirikiana na Jopo la madaktari bingwa kutoka Hospitali ya BLK ya New Delhi, India.

 Prof. Lawrence Museru akimueleza jambo Waziri wa Afya, Maendeleo ya jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Ummy Mwalimu wakati wa uzinduzi rasmi wa huduma za upasuaji wa upandikizaji wa figo uliofanyika katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili .

 Mkuu wa Kitengo cha Upandikizaji wa Figo kutoka India Dkt. H.S Bhatyal akimtambulisha Mkurugenzi Mkuu wa Nephroway Dkt. Sunil Prakash  mbele ya  Waziri wa Afya, Maendeleo ya jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Ummy Mwalimu.

Picha ya pamoja ikiongozwa na Waziri wa Afya, Maendeleo ya jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Ummy Mwalimu katika uzinduzi rasmi wa huduma za upasuaji wa upandikizaji wa figo uliofanyika katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili.




Na WAMJWW, DSM
Hospitali ya Taifa ya Muhimbili ikishirikiana na wataalam kutoka Hospitali ya BLK ya New Delhi, India, wamefanikiwa kufanya upasuaji wa kihistoria wa upandikizaji wa figo (Renal Transplant).
Hayo yamesemwa na Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Ummy Mwalimu wakati wa uzinduzi rasmi wa upandikizaji wa figo uliofanyika katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili jijini Dar es salaam.
“Kupitia hadhara hii nipende kutumia fursa hii kuwafahamisha rasmi Watanzania kwamba sasaivi Hospitali yetu ya Taifa ya Muhimbili kwa kushirikiana na Hospitali ya BLK ya New Delhi, nchini India wamefanikiwa kufanya upasuaji wa upandikizaji wa figo” alisema Mh. Ummy
Pia Waziri Ummy amesema kuwa kuanzishwa kwa huduma hizi zakibingwa za kupandikiza figo hapa nchini ambazo awali zilikua hazipatikani kutaleta nafuu katika gharama ambazo zingetumika, hii inatokana na ongezeko kubwa la wagonjwa wa figo huku wengi wao wakihitaji huduma ya utakasishaji damu (Renal Dialysis).
Kwa upande mwingine Mh. Ummy ameongeza kuwa Serikali imeanzisha vituo vya utakasishaji damu katika hospitali za Mbeya Rufaa, Chuo Kikuu cha Dodoma, KCMC na Bugando kwaajili ya  wagonjwa wanaohitaji huduma za dialysis. Vile vile, huduma hii inapatikana katika hospitali za binafsi hapa Dar es Salaam zikiwemo za Kairuki, TMJ, Regency, Aga Khan, Access na Hindu Mandal.
Mh. Ummy  Mwalimu amewahasa Watanzania kuendelea kuiamini Hospitali ya taifa ya Muhimbili kutokana na huduma bora zinazotolewa na amewahakikishia serikali itaendelea kuboresha huduma zaidi katika vituo vyote vya Afya nchini.
Aidha Mh. Ummy Mwalimu (MB) ameendelea kuwakumbusha na kuwahasa Watanzia kujiunga na mifuko ya Bima ya Afya ili kupunguza gharama kubwa inayoweza kuwakumba pindi watakapopata magonjwa.
Pia Mh. Ummy (MB) hakusita kumpongeza Raisi wa awamu ya Tano Dkt. John Pombe Magufuli kwa kwa kuwa karibu sana na sekta ya Afya kwa  kuboresha huduma za matibabu yakibingwa,
“Wakati Mh. Raisi anaingia madarakani Muhimbili walikuwa wana vitanda vya ICU 21 tu, leo Muhimbili wanavitanda 74, wagonjwa 74 wanaweza kuhudumiwa mara moja kwa wakati mmoja ambao wanahitaji huduma za dharura” alisema Mh. Ummy Mwalimu.
Nae Mkurugenzi Mkuu wa Hospitali ya Taifa ya Muhimbili Prof. Lawrence Museru amewashukuru Madaktari bingwa wa upandikizaji wa figo kutoka Hospitali ya BLK ya New Delhi India kwa kukubali kutoa mafunzo kwa madaktari wa Tanzania bila gharama yoyote.


0 on: "UPASUAJI WA KIHISTORIA WA UPANDIKIZAJI WA FIGO WAFANYIKA."